CHADEMA ifanye nini kujiandaa kwa uchaguzi ujao?

The hammer

JF-Expert Member
May 17, 2011
2,381
1,760
Una wazo gani ili kuhakikisha chama cha CHADEMA kinajiwekea mazingira mazuri ya ushindi kwa chaguzi zijazo hasa kwenye mikoa isiyo na wanachama wengi kama mikoa yote ya ukanda wa pwani na kanda ya kati na maeneo yote ya vijijini kwa ngazi zote i.e... SERIKALI ZA MITAA, UDIWANI,UBUNGE NA URAIS..

Na ni kasoro gani(kisera na kimkakati)zilizojitokeza ktk uchaguzi uliopita ktkt eneo ulilokuwepo zilizotokana na wagombea wake au ujanja uliofanyika nakudhoofisha CHADEMA kutokupata kura nyingi ili ziweze kuepukwa ktkt chaguzi nyingine zijazo ktk ngazi zote.

NAANZA NA:
1:Operation Sangara ianze kuvunja ngome zote za CCM ktk mikoa tajwa hapo tu na wilaya nyingine zenye usumbufu.

2:Ishiriki kikamilifu kuhakikisha inashinda viti vingi ktk ngazi za SERIKALI ZA MITAA(vitongoji) ili kujitanua zaid vijijni.

endelea......
 
Utakapofika wakati wakujiandikisha kupiga kura watoe Elimu ya uraia kwavijana wajitokeze kwa wingi kujiandikisha pia Uanzishwe mkakati madhubuti wakuhamasisha chama ktk mikoa ya Lindi,Mtwara,Ruvuma,Tanga na pwani Ili njia yakuingia magogoni iwe nyeupe....kuna mtaji mwingine viongozi wa chadema wanausahau nao ni kuwasemea askari wa vikosi vya ulinzi na usalama watu hawa wana matatizo mengi lkn miongozo na sheria za nchi yetu haziwaluhusu kugoma au kuongea kwenye vyombo vya habari matatizo na mapungufu yanayo wakabili,,,kwayanayojitokeza sasa serikalini wananchi wanaamini mkombozi pekee ni CHADEMA.
 
Back
Top Bottom