Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema hawatalipa kisasi hata baada ya mahakama kumfutia kesi ya ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama hicho, Wilfred Lwakatare, kwa kigezo kuwa mashitaka hayo yalikuwa hayajitoshelezi kuitwa kuwa ni ya ugaidi.
Akizungumza na gazeti hili baada ya hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kuvutia hisia za watu wengi Dk. Slaa alisema: Tumesema toka mwanzo, tunaanza na Mungu, tunaendelea na Mungu na tutamaliza na Mungu, hujuma zozote dhidi ya CHADEMA kamwe hazitashinda kwa uwezo wa Mungu.
CHADEMA tunapigania ukombozi wa pili wa taifa letu, tunawapigania wanyonge, tunawapigania walalahoi. Hatukuwa, hatuna na hatutakuwa na sababu ya ugaidi.
Source:Tanzania Daima
Akizungumza na gazeti hili baada ya hukumu hiyo iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na kuvutia hisia za watu wengi Dk. Slaa alisema: Tumesema toka mwanzo, tunaanza na Mungu, tunaendelea na Mungu na tutamaliza na Mungu, hujuma zozote dhidi ya CHADEMA kamwe hazitashinda kwa uwezo wa Mungu.
CHADEMA tunapigania ukombozi wa pili wa taifa letu, tunawapigania wanyonge, tunawapigania walalahoi. Hatukuwa, hatuna na hatutakuwa na sababu ya ugaidi.
Source:Tanzania Daima