Abdull Kazi
JF-Expert Member
- Dec 29, 2012
- 344
- 306
Leo jijini Dodoma,kunaendelea kufanyika mkutano was wadau was siasa utakaomalizika Disemba 17 mwaka huu.
Katika mkutano huo viongozi was vyama vilivyoshiriki wamepata kuongea mbele ya Rais kupitia mwenyekiti was TCD ndugu Zitto Kabwe,ambapo Jambo kubwa alilomuomba Rais ni kuiunganisha nchi kwa kile alichoeleza kuwa imeparaganyika.
Akitumia kauli ya Askofu Shoo,Zitto amesema kubwa kwa Sasa lililobeba madhila ya kisiasa moja kwa moja ni kesi inayoendelea ya Mwenyekiti wa chadema Mzee Freeman Mbowe.
Amemuomba Rais ikiwezekana kikombe hicho Cha kesi kimuepuke Mzee Mbowe na wengine wenye madhila Kama hayo kwa ajili ya maslahi mapana ya nchi.
Kutokana na kauli hiyo ya Zitto,Rais Samia akaeleza ni muhimu watu wafuate Sheria na kuheshimu mamlaka,Mimi sitaki kuingia kwenye mjadala huo.
Maoni yangu nitayaelekeza kwenye uamuzi wa Chadema kabla ya mkutano na baada ya mkutano.
Kabla ya mkutano huo chadema walisema hawatashiriki kwa namna yeyote kwa vigezo walivyoviainisha.
Wakaenda mbali na kupitia kwa wanaharakati rafiki wa chama hicho Maria Sarungi na wengine wakaeleza matokeo yoyote yatakayotoa unafuu kwenye mkutano huo ni kwa sababu ya shinikizo la Chadema wenyewe kuususia.
Baada ya ufunguzi wa kikao hicho Cha wadau wa siasa Chadema kupitia Makamu Mwenyekiti Lissu na wanaharakati rafiki,wameanza kunyooshea vidole na kukosoa kile kilichozungumzwa na walioshiriki Kimwili na kiakili katika mkutano husika.
Kwa kuwa wao hawakushiriki Kimwili,wamepinga Yale yaliyoainishwa na wenzao ambayo kwa sababu ya uwepo wao Rais amejibu,hata Kama jibu halina mwelekeo.
Kwa Sasa wamejikita mitamdaoni kukosoa na kueleza wao wangeongea Nini na wangeshinikiza Nini.
Wamekuwa vinara kweli kweli huko mitandaoni pasipo kujua Kama hoja zao zimefika moja kwa moja ama la
Kiufupi wameshiriki kiakili wakati mwili waliuacha ushughulike na Mambo mengine na usionekane kwenye kikao kwa ajili ya kuwananga walioshiriki moja kwa moja.
Nb MMM na kigogo nifungulieni huko Twitani tusiwe waoga wa kukosolewa
Katika mkutano huo viongozi was vyama vilivyoshiriki wamepata kuongea mbele ya Rais kupitia mwenyekiti was TCD ndugu Zitto Kabwe,ambapo Jambo kubwa alilomuomba Rais ni kuiunganisha nchi kwa kile alichoeleza kuwa imeparaganyika.
Akitumia kauli ya Askofu Shoo,Zitto amesema kubwa kwa Sasa lililobeba madhila ya kisiasa moja kwa moja ni kesi inayoendelea ya Mwenyekiti wa chadema Mzee Freeman Mbowe.
Amemuomba Rais ikiwezekana kikombe hicho Cha kesi kimuepuke Mzee Mbowe na wengine wenye madhila Kama hayo kwa ajili ya maslahi mapana ya nchi.
Kutokana na kauli hiyo ya Zitto,Rais Samia akaeleza ni muhimu watu wafuate Sheria na kuheshimu mamlaka,Mimi sitaki kuingia kwenye mjadala huo.
Maoni yangu nitayaelekeza kwenye uamuzi wa Chadema kabla ya mkutano na baada ya mkutano.
Kabla ya mkutano huo chadema walisema hawatashiriki kwa namna yeyote kwa vigezo walivyoviainisha.
Wakaenda mbali na kupitia kwa wanaharakati rafiki wa chama hicho Maria Sarungi na wengine wakaeleza matokeo yoyote yatakayotoa unafuu kwenye mkutano huo ni kwa sababu ya shinikizo la Chadema wenyewe kuususia.
Baada ya ufunguzi wa kikao hicho Cha wadau wa siasa Chadema kupitia Makamu Mwenyekiti Lissu na wanaharakati rafiki,wameanza kunyooshea vidole na kukosoa kile kilichozungumzwa na walioshiriki Kimwili na kiakili katika mkutano husika.
Kwa kuwa wao hawakushiriki Kimwili,wamepinga Yale yaliyoainishwa na wenzao ambayo kwa sababu ya uwepo wao Rais amejibu,hata Kama jibu halina mwelekeo.
Kwa Sasa wamejikita mitamdaoni kukosoa na kueleza wao wangeongea Nini na wangeshinikiza Nini.
Wamekuwa vinara kweli kweli huko mitandaoni pasipo kujua Kama hoja zao zimefika moja kwa moja ama la
Kiufupi wameshiriki kiakili wakati mwili waliuacha ushughulike na Mambo mengine na usionekane kwenye kikao kwa ajili ya kuwananga walioshiriki moja kwa moja.
Nb MMM na kigogo nifungulieni huko Twitani tusiwe waoga wa kukosolewa
. Na kuongea kwenu hata akipumua tu mccm mtaongea. Kwenu mada lazima iwafave. Ama sivyo itakuwa kinyume na Demokrasia. Mnahodhi Demokrasia. Jinga kabisa