Unajua nini. Lazima uwe fisadi ili kuaminisha watu kwamba Watanzania wamechoshwa na kelele za ufisadi. Afadhali ungesema kuwa serikali ya sasa imechukua juhudi makini kupambana na ufisadi na inaonekana hivyo, dhana yako ingekuwa na mantiki. Mnataka kusahaulisha watu ufisadi unaondelea ili muendelee kuifisidi nchi bila kukosa usingizi. Taa yenu tunayo na tunawamulika madirishani mnapolala.Mkuu Mkeshaji,
Huu ndio ukweli unajua kila siku unapiga kelele za ufisadi ufisadi, zimewachosha watanzania lazima Chadema kama chama ibuni falsafa mpya kutegemea kuhubiri ufisadi kama kete yake haitakisaidia Chadema huko tuendako.
Ukitaka kufahamu umaarufu wa CDM, fanya simple analysis hapa JF!
Analysis kama hizi zilikuwa zinatolewa na wagonjwa wa akili miaka ya utawala wa mwalimu...sitegemei mtu mwenye akili timamu aseme kuwa CDM umaarufu wake unashuka,au aseme CCM inapaa kwasasa..inahitaji uwe kichaa au mwendawazimu kutoa maoni kama hayo.....
Hivi Kikwete aliwaeleza Watanzania atawafanyia nini? Na amefanya mangapi mbali ya kuzurura?Watanzania tuamke, tujifunze kwa Wamarekani kila mtu anapaswa kueleza ataifanyia nini nchi yake na sio nchi itakufanyia nini.
Kitu usichokijua ni kama kiza nene.CHADEMA ni chama kisicho na sera kabisa, sera yao ni ufisadi tu hawana sera nyingine. Hebu cheki kipindi watu wanakufa mahospitalini kutokana na mgomo wa madr, hapakuwepo na hata ka mpango ka kuandaa maandamano nchi nzima kutoka kwao na hivyo serikali ikawa haina mtu/chombo cha kuishinikiza ili iharakishe kutatua madai ya madr. Ila kama ingekuwa kupinga kulipwa kwa dowanz, maandamano yangekuwa ni mapema sana, au kama ingekuwa ni mafuriko wangejidai kuwatembelea waathirika haraka sana, ila kipindi wagonjwa wanakufa hospitalini CHADEMA hawakuonekana mahosiptalini ili kuwafariji wagonjwa. Poor CHADEMA.
Ukitaka kufahamu umaarufu wa CDM, fanya simple analysis hapa JF!
2010 kabla na baada ya uchaguzi, thread za CDM zilikuwa na wachangiaji wengi sana, lakini hali imekuwa tofauti sasa! Hamna mtu yupo interested kuchangia au kusikia mambo ya CDM, mmebaki nyie wachache ambao hamna uelewa wa kutosha kwenye mambo ya siasa!
Mkuu Rejao,
Kumbe na wewe umeona ehee! Awa jamaa ndio wamechangia sana kuitangaza vibaya Chadema humu JF kwa kauli zao za kihuni.
Ndipo Chadema inapoelekea! Ni suala la muda tu.
Mkuu Mkeshaji,
Huu ndio ukweli unajua kila siku unapiga kelele za ufisadi ufisadi, zimewachosha watanzania lazima Chadema kama chama ibuni falsafa mpya kutegemea kuhubiri ufisadi kama kete yake haitakisaidia Chadema huko tuendako.
Bado sana mkuu ritz kusema CDM imedorora! kuna mambo mengi yanatisha ndani ya serikali na hakuna dalili za kuyapatia dawa. Watanzania wengi wanataka mabadiliko, na mabadiliko hayaji kama mvua ila kwa mipango yenye akili.
Wanabodi..
Mwenendo wa kisiasa, kati ya watani wa jadi CCM na Chedema sasa umeanza kuzua mijadala ndani ya jamii.
Wananchi wanahoji iko wapi kasi na upepo wa mabadiliko ilikuwa nao Chadema mwaka 2010 na mwaka jana ilikoyeyukia.
Huku CCM kilichokuwa kimeanza kudorora sasa kikionekana kupaa zaidi kuliko ilivyotarajiwa na wengi.
Mwamko wa Chadema ulianza kushika kasi mara baada ya Slaa, kuteuliwa kugombea Urais, mwamko huo uliendelea hata baada ya uchaguzi, na hasa baada ya chama hicho kuamua kufanya siasa zake kwa njia ya maandamo mikoa ya Kanda ya Ziwa hadi Nyanda za Juu Kusini.
Wadadisi wa mambo ya kisiasa wameanza kuhoji ni wapi kasi hiyo imeyeyeka ghafla na kukipa nafasi tena CCM kuanza kutamba katika maeneo mbali mbali nchini.
Hali hiyo ya kuanza kudorora kwa Chadema imelezwa pia kukikumba chama cha CUF kupoteza mvuto.
Chadema inatakiwa ibadili sera zake na falsafa mpya za kuendelea kuwashawishi Watanzania.
Siielewi falsafa ya CHADEMA. Inaelekea hawana fasafa. Kwa hiyo, itikadi yao huwa haieleweki.@ritz uchambuzi mzuri kuongezea tu ni kwamba; Chadema ina tatizo la mfumo na itikadi??
Mfumo wao uendeshaji hauna malengo ya muda mrefu ndio maana kila wakati kunapokuwa na issue lazima waweke consultancy aje na formula ya ku-solve issue..hawana mfumo wa uongozi..ndio maana kupendelewa na ubaguzi ni jambo la kawaida..sana; pamoja na kwamba wana advantage ya MEDIA coverage..especially mainstream media..
Tatizo la itikadi lina wasumbua sana ndio maana kuna wakati walinadi issue ya "kikanda" regional powers; naona hawaonglei tena habari hiyo; kuna wakati walisema wao ni wapebari wamenyamaza hawataki kuonglea ubepari utatusaidiaje? wananchi
Mkuu siku media attention ikihamia CCK ndio mwisho wake..
Hivi Kikwete aliwaeleza Watanzania atawafanyia nini? Na amefanya mangapi mbali ya kuzurura?