CHADEMA bila Dr. Slaa haina dira wala hamasa (CHADEMA without Slaa lacks vision and enthusiasm)

Stabilaiza

JF-Expert Member
Jul 11, 2012
1,843
1,143
Kitu ambacho kiko wazi ni kuwa CHADEMA ya sasa imekosa dira na hamana kabisa. Wengi tuliionya CHADEMA isithubutu kumchukua Lowassa kwa sababu kwa kufanya hivyo kilikuwa kinapingana na sera yake ya kupinga ufisadi.

Hatukuishia hapo, tukasema kuwa kumleta Lowassa kipindi cha uchaguzi ni kupuuza hazina ya viongozi wa CHADEMA wakiwemo wabunge machachali wa CHADEMA ambao kwa uongozi wa Dr. Slaa walipigana vema vita ya kupinga ufisadi. Walipendwa kiukweli na wananchi, na hata wana CCM waliwapenda sana wapiganaji wa CHADEMA.

Kwa kuwataja wachache ni Mnyika, Mdee, Vincent Nyerere, Mbowe, Tundu Lissu, Msingwa na Wenje. Kipindi hicho wakionekana hao bungeni au majukwaani unahamasika kunatega sikio vizuri.

Dr. Slaa kaondoka na dira ya chama imepotea. Sera endelevu iliyokuwepo ya kurudisha chama kwa wananchi kupitia sera ya ugatuzi imepotea. Mifano michache ni maamuzi ya ngazi ya chini kuamuliwa na viongozi wa juu moja kwa moja, hasa katika uchaguzi wa wagombea ubunge na viti maalum badala ya kuzingatia mchakato wa uchaguzi katika ngazi za chini. Kupotea kwa dira ya CHADEMA kumeenda sambamba na kupotea hamasa kwa wanachama na wananchi mashabiki walio wengi.

Watake wasitake lakini huu ndiyo ukweli wenyewe, CHADEMA imemtupa kiongozi aliyekuwa anaonyesha dira ya chama na kuhakikisha kuwa hamasa ya wananchi na wanachama inabaki juu na kuendelezwa.

Kwa kuonyesha kuwa CHADEMA wamepoteza mwelekeo, wanatengeneza chama ambacho kinazua maswali mengi kuliko majibu. Wakati wa uongozi wa Mwl. Nyerere aliwahi kuulizwa nadhani na mwandishi wa habari kutoka nchi za magharibi kuwa baraza lake la mawaziri limejaa wakatoliki. Kwa kuwa uteuzi wake haukuwa wa upendeleo akashangaa hilo limetoka wapi.

Akaagiza uchunguzi ufanyike kujua ukweli wa jambo hili. Akafikiri kuwa ili kujua ukweli waanze kwa kuwafahamu walioapa kwa biblia na wasioapa kwa biblia. Lakini njia hii isingewatofautisha wakristo wa madhehebu mbalimbali. Hivyo uchunguzi wa kina zaidi ukafanyika. Na akakuta kuwa wakatoliki alikuwa yeye na George Kahama ambaye yeye alikuwa amekwisha endelea zaidi kwa vile alikuwa na mke wa pili isivyotakiwa na imani ya kikristo.

Kioja sasa ni CHADEMA, pamoja na kutuhumiwa kuwa wanatakiwa wa-address taswira ya kusema kwamba chama kile kimejikita zaidi kaskazini, lakini wameleta maswali zaidi. Ukaribu wa Mboe, Lowassa, Sumaye na pia Mbatia ingawa hayupo CHADEMA lakini alikuwa katikati la vuguvugu la kumleta Lowassa kugombea urais, unaleta maswali ya jee hivi Mbowe, Sumaye, Lowassa na Mbatia ni madhehebu gani? Kwa kukosa dira na mwelekeo, CHADEMA hii ya bila Slaa haioni kwamba ni kitu muhimu kujiangalia kama hawakiletei chama taswira na mwelekeo wa dhehebu fulani.

Kwa kawaida mimi si kati ya mashabiki wa siasa za kibaguzi. Lakini kwa kuwa CHADEMA imekosa dira kwa sababu aliyekuwa anaonyesha njia (Dr Slaa) alitupiwa virago na kudhalilishwa, hawa CHADEMA wanaweza kufanya chochote. Wamekosa hisia, dira na wanachama na mashabiki wao nao wamekosa hamasa.
 
Hakika wewe ni mzalendo! Dr.W.Slaa iokoe chadema imekuwa pango la wanyang'anyi...!
 
Last edited by a moderator:
Hakika wewe ni mzalendo! Dr.W.Slaa iokoe chadema imekuwa pango la wanyang'anyi...!
Tatizo ni namna gani wakati Dr. Slaa alishatupiwa virago na kudhalilishwa sana na CDM?

Tahadhali, ufisadi uliokithiri nchini umeshamirishwa na CCM. Umefugwa, kuendelezwa na kufumbiwa macho na viongozi chama na serikali ya CCM.
 
Yanihawa magamba ni watu hatareee sana.. Leo slaa kwao anafaa kana mwamba wanaitamia mema sana cdm
Nimeshasema tujadili kwa utulivu, nani aliyekwambia kuwa Dr Slaa hafai. Dr. Slaa alifaa enz zile kabla ya Lowassa na anafaa hata sasa. Tatizo si CDM watamrudishaje baada ya kumdhalilisha?
 
Alipokuwa cdm mlikuwa mnadai babu,kachoka..

cdm tunaipenda vile vile

Mkuu, hawa watu wanashangaza sana, hivi ikitokea kibinadamu wanayemshadadia akatangulia mbele za haki maana hilo halikwepeki kwa binadamu bado watakuwa wanamtaja kuwa bila yeye CDM haiwezi kwenda?

Tatizo tulilonalo watanzania ni kutokuwa na mazoea na succession plans, kama Dr hakumtengeneza mrithi basi naye hafai kutolewa mfano, sasa hivi serikali inakazia kutengeneza succession plan ili kuepuka kuongezea mikataba wanaostahili kustaafu sasa kama nchi nzima tuna mtu mmoja tu anayefaa kuwa katibu mkuu wa chama basi huu ni ugonjwa mbaya sana
 
Yanihawa magamba ni watu hatareee sana.. Leo slaa kwao anafaa kana mwamba wanaitamia mema sana cdm

Leo Mh Mbowe akipinduliwa katika kitu chake watakuja hapa, na stories kibao, utawasikia "hakuna kamanda na mwanasiasa wa siasa za.kimageuzi kama Mbowe!"

Hawa ndio wanachama na wapenzi wa ccm ambao Leo wanamwona Mbowe kama adui wa demokrasia ndani ya chama, lakini akitoka anakuwa shujaa wa chama!
 
Team Lowasa hawataki kabisa kusikia habari za Dr Slaa. Hakuna anayeweza kuvifaa viatu vya Dr Slaa hata chembe. Labda Mbowe awe katibu mkuu wa CDM,au Masha
cc Ocampo four
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, hawa watu wanashangaza sana, hivi ikitokea kibinadamu wanayemshadadia akatangulia mbele za haki maana hilo halikwepeki kwa binadamu bado watakuwa wanamtaja kuwa bila yeye CDM haiwezi kwenda?

Tatizo tulilonalo watanzania ni kutokuwa na mazoea na succession plans, kama Dr hakumtengeneza mrithi basi naye hafai kutolewa mfano, sasa hivi serikali inakazia kutengeneza succession plan ili kuepuka kuongezea mikataba wanaostahili kustaafu sasa kama nchi nzima tuna mtu mmoja tu anayefaa kuwa katibu mkuu wa chama basi huu ni ugonjwa mbaya sana
Akienda mbele za hali tunasema ni mapenzi ya Mungu ikiwa tu siyo kuuawa kama alivyouawa Mawazo na wanaotuhumiwa kuwa ni CCM. Lakini kumtosa kiongozi mwenye dira na anayesimamia dira huku CDM inaenda kinyume na sera zake ni kupoteza dira na inaenda sawia na kukosa kuungwa mkono na wanachama na wananchi. Chama kinaendelea kuzua maswali mengi kuliko majibu. Imeiona hiyo?
 
Alipokuwa cdm mlikuwa mnadai babu,kachoka..

cdm tunaipenda vile vile

Kama matusi na majina yote mliyompa Lowasa .....nyie washabiki hamsaidii chama ....kila hoja zenu kidole kinarudi kwenu tofauti na CDM ya zamani .....ule ukamanda kwa wabunge wa Chadema unakufa kwa kasi .....inauma sana kuona kuna watu kupitia ushabiki wao bila kujua wanashiriki kuua upinzani badala ya kuwapa ukweli wa kuwajenga .....Chadema ya sasa ipo ipo tu ....
 
Team Lowasa hawataki kabisa kusikia habari za Dr Slaa. Hakuna anayeweza kuvifaa viatu vya Dr Slaa hata chembe. Labda Mbowe awe katibu mkuu wa CDM,au Masha
cc Ocampo four
Mbowe hawezi kuvaa viatu vya Slaa. Picha sasa ni wazi, Mbowe alikuwa anamtegemea Slaa kuonyesha njia ya kuongoza chama.
 
Kama matusi na majina yote mliyompa Lowasa .....nyie washabiki hamsaidii chama ....kila hoja zenu kidole kinarudi kwenu tofauti na CDM ya zamani .....ule ukamanda kwa wabunge wa Chadema unakufa kwa kasi .....inauma sana kuona kuna watu kupitia ushabiki wao bila kujua wanashiriki kuua upinzani badala ya kuwapa ukweli wa kuwajenga .....Chadema ya sasa ipo ipo tu ....
Kitu kibaya zaidi, ni kama wamekosa hisia. Sikio la kufa halisikii dawa.
 
Kitu ambacho kiko wazi ni kuwa Chadema ya sasa imekosa dira na hamana kabisa. Wengi tuliionya CDM isithubutu kumchukua Lowassa kwa sababu kwa kufanya hivyo kilikuwa kinapingana na sera yake ya kupinga ufisadi.

Hatukuishia hapo, tukasema kuwa kumleta Lowassa kipindi cha uchaguzi ni kupuuza hazina ya viongozi wa CDM wakiwemo wabunge machachali wa CDM ambao kwa uongozi wa Dr. Slaa walipigana vema vita ya kupinga ufisadi. Walipendwa kiukweli na wananchi, na hata wana CCM waliwapenda sana wapiganaji wa CDM.

Kwa kuwataja wachache ni Mnyika, Mdee, Vincent Nyerere, Mbowe, Tundu Lissu, Msingwa na Wenje. Kipindi hicho wakionekana hao bungeni au majukwaani unahamasika kunatega sikio vizuri.

Dr. Slaa kaondoka na dira ya chama imepotea. Sera endelevu iliyokuwepo ya kurudisha chama kwa wananchi kupitia sera ya ugatuzi imepotea. Mifano michache ni maamuzi ya ngazi ya chini kuamuliwa na viongozi wa juu moja kwa moja, hasa katika uchaguzi wa wagombea ubunge na viti maalum badala ya kuzingatia mchakato wa uchaguzi katika ngazi za chini. Kupotea kwa dira ya CDM kumeenda sambamba na kupotea hamasa kwa wanachama na wananchi mashabiki walio wengi.

Watake wasitake lakini huu ndiyo ukweli wenyewe, CDM imemtupa kiongozi aliyekuwa anaonyesha dira ya chama na kuhakikisha kuwa hamasa ya wananchi na wanachama inabaki juu na kuendelezwa.

Kwa kuonyesha kuwa CDM wamepoteza mwelekeo, wanatengeneza chama ambacho kinazua maswali mengi kuliko majibu. Wakati wa uongozi wa Mwl. Nyerere aliwahi kuulizwa nadhani na mwandishi wa habari kutoka nchi za magharibi kuwa baraza lake la mawaziri limejaa wakatoliki. Kwa kuwa uteuzi wake haukuwa wa upendeleo akashangaa hilo limetoka wapi.
Akaagiza uchunguzi ufanyike kujua ukweli wa jambo hili. Akafikiri kuwa ili kujua ukweli waanze kwa kuwafahamu walioapa kwa biblia na wasioapa kwa biblia. Lakini njia hii isingewatofautisha wakristo wa madhehebu mbalimbali. Hivyo uchunguzi wa kina zaidi ukafanyika. Na akakuta kuwa wakatoliki alikuwa yeye na George Kahama ambaye yeye alikuwa amekwisha endelea zaidi kwa vile alikuwa na mke wa pili isivyotakiwa na imani ya kikristo.

Kioja sasa ni CDM, pamoja na kutuhumiwa kuwa wanatakiwa wa-address taswira ya kusema kwamba chama kile kimejikita zaidi kaskazini, lakini wameleta maswali zaidi. Ukaribu wa Mboe, Lowassa, Sumaye na pia Mbatia ingawa hayupo CDM lakini alikuwa katikati la vuguvugu la kumleta Lowassa kugombea urais, unaleta maswali ya jee hivi Mbowe, Sumaye, Lowassa na Mbatia ni madhehebu gani? Kwa kukosa dira na mwelekeo, CDM hii ya bila Slaa haioni kwamba ni kitu muhimu kujiangalia kama hawakiletei chama taswira na mwelekeo wa dhehebu fulani.

Kwa kawaida mimi si kati ya mashabiki wa siasa za kibaguzi. Lakini kwa kuwa CDM imekosa dira kwa sababu aliyekuwa anaonyesha njia (Dr Slaa) alitupiwa virago na kudhalilishwa, hawa CDM wanaweza kufanya chochote. Wamekosa hisia, dira na wanachama na mashabiki wao nao wamekosa hamasa.
mm nadhani kupoteza dira kwa cdm ndiyo faeaja kwa ccm kumbe ni majonzi pia au unafiki Tu?
 
Huna hata aibu ww gamba ya Lumumba yanawashinda ya ufipa utayaweza wapi??
Hapa sasa umeandika nini ndugu yangu Habari ya hapa. Hebu soma tena ulichoandika. umeandika hivi nanukuu "Huna hata aibu ww gamba ya Lumumba yanawashinda ya ufipa utayaweza wapi??" Nilisema mwanzo kuwa tujadili kwa utulivu. Ungenisikia usingenadika hivi. Pole lakini.
 
Chama ni taasisi sio mtu.Dr Slaa aliikuta Chadema nikweli anamchango mkubwa lakini kuondoka kwake sio mwisho wa chama.
 
Back
Top Bottom