CEO mpya Simba utawezaje kuitumikia klabu na kampuni ya TBL kwa wakati mmoja?

Blasio Kachuchu

Senior Member
Sep 7, 2016
153
111
Moja ya Habari iliyotamba kwenye duru la michezo na kwenye mitandao ya kijamii nchini mwishoni mwa wiki ni klabu ya soka ya Simba kumpata Afisa Mtendaji Mkuu mpya mwanamke , Barbara Gonzalez.

Barbara Gonzalez, mbali na wadhifa huu mpya katika klabu hii kongwe ya soka nchini ni mfanyakazi wa kampuni ya bia Tanzania (TBL) akiwa anashikilia nafasi kubwa ya Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano (Legal & Corporate Affairs Director).

Kwa nafasi kama hii kwenye kampuni kubwa ambayo ina hisa za watanzania wenye itikadi na mapenzi kwa vilabu vya timu mbalimbali, kutumikia klabu ya Simba wakati huohuo kuwa Msemaji na Afisa wa ngazi ya juu wa kampuni anayeunganisha kampuni na Serikali,taasisi na wadau mbalimbali, kuna mgongano wa maslahi ambao unaweza kwa kiasi kikubwa kuathiri kampuni.

Natoa wito kwa watendaji wenye nyadhifa za juu kwenye makampuni ya umma na binafsi ambayo yameuza sehemu ya hisa zake kwa wananchi kuacha kujiingiza kwenye ajira za vilabu vya soka maana masuala ya michezo yana mambo mengi, mpaka wakati wengine kuna misukosuko ambayo kiongozi wa klabu akiipata inaweza pia kuhusisha mwajiri wake.

Barbara hongera kwa kujitoa mhanga kuongoza klabu ya soka ila acha kutumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja,chagua kuwa CEO wa Simba au Mkurugenzi kwenye kampuni ya TBL
 
Maslahi yanaweza kuingiliana kwenye masuala ya udhamini pengine. Yeye na waliopa uofisa wa klabu wanajua wanalofanya.
 
Barbara ni mrembo sana; tatizo mmezoea vilabu hivi kuongozwa na vigagula visivyo na exposure ya aina yoyote zaidi ya kwenda Mlingotini "kuweka mambo sawa". Ni wakati sasa vilabu vyetu vikaongozwa na wasomi, damu changa, na wenye uwezo wa kufikiri in 3D. Simba imeonesha mfano Barbara atiwe moyo badala ya mizingwe ya kichawi kama hii kujaribu kumkatisha tamaa.
 
Tena TBL ndo haswaa mahala pake.Simba ikishinda unapiga Kilimanjaro zako kisha unaenda kutafuna.
 
Wachawi kila sehemu wapo. Na walivyo na unafiki basi akikurogea mtoto wako litatoa machozi ya damu kujifanya nae kahuzunishwa!
 
Wachawi kila sehemu wapo. Na walivyo na unafiki basi akikurogea mtoto wako litatoa machozi ya damu kujifanya nae kahuzunishwa!
... sawa sawa kabisa Chief. Kwa dunia ya leo vilabu vinahitaji chairpersons na ma-CEO wasomi na wenye exposure ya kutosha. Tukiendelea kutegemea watu aina ya Mzee Akilimali (rip) karne (1934/1936) ya kuanzishwa kwa hivi vilabu inakaribia kuisha bila lolote la maana! It's time for new blood to take over.
 
... sawa sawa kabisa Chief. Kwa dunia ya leo vilabu vinahitaji chairpersons na ma-CEO wasomi na wenye exposure ya kutosha. Tukiendelea kutegemea watu aina ya Mzee Akilimali (rip) karne (1934/1936) ya kuanzishwa kwa hivi vilabu inakaribia kuisha bila lolote la maana! It's time for new blood to take over.
Ni ngumu sana kumuelewesha kipofu rangi nyeupe inafananaje ikiwa ni kipofu wa kuzaliwa na upofu wake.

Ila hawa wa kujitia uchizi wakati walikuwa hawafanyi lolote kabla tutaenda nao tu perpendicular
 
... sawa sawa kabisa Chief. Kwa dunia ya leo vilabu vinahitaji chairpersons na ma-CEO wasomi na wenye exposure ya kutosha. Tukiendelea kutegemea watu aina ya Mzee Akilimali (rip) karne (1934/1936) ya kuanzishwa kwa hivi vilabu inakaribia kuisha bila lolote la maana! It's time for new blood to take over.
mkuu na wewe umeludia kosa kumtaja mzee akilimali
 
mkuu na wewe umeludia kosa kumtaja mzee akilimali
Ni tofauti Mkuu. Kisichotakiwa ni ku-disclose anonymous ID kwamba ni fulani kwa jina lake halisi. Kwa mfano nikisema wewe kifinga ni "Maria Mhagama" nitakuwa nimeenda kinyume kwa ku-associate ID ya kifinga na "Maria Mhagama" (jina halisi) tena mbaya zaidi kama ni mtu maarufu kwenye jamii kama huyo uliyemtaja. Mimi sija-associate ID yoyote humu na Mzee Akilimali na wala hatufungwi kutaja watu humu as long as wahusika ni part of the issues being discussed. ID <===> Specific Person wrong!
 
Ni tofauti Mkuu. Kisichotakiwa ni ku-disclose anonymous ID kwamba ni fulani kwa jina lake halisi. Kwa mfano nikisema wewe kifinga ni "Maria Mhagama" nitakuwa nimeenda kinyume kwa ku-associate ID ya kifinga na "Maria Mhagama" (jina halisi) tena mbaya zaidi kama ni mtu maarufu kwenye jamii kama huyo uliyemtaja. Mimi sija-associate ID yoyote humu na Mzee Akilimali na wala hatufungwi kutaja watu humu as long as wahusika ni part of the issues being discussed. ID <===> Specific Person wrong!
sasa mbona uli draw conclusions kwangu mkuu unauhakika gani kama huyo alikua manara kweli
 
sasa mbona uli draw conclusions kwangu mkuu unauhakika gani kama huyo alikua manara kweli
... context! Mada inahusu klabu ya Simba wewe unataja jina la mtendaji rasmi wa Simba kwa kulinajisibisha na anonymous ID iliyoleta mada husika hapa Jukwaani unategemea audience ieleweje?
 
Uzuri wa Watanzania ni kelele za wiki tu linakuja lingine wanadandia maisha yanaenda. Hata waliomteua walijua mjadala wa huyo dada utakuwepo sana tu na wanajua litapoa maisha yataendelea
 
Vyeo vyote vinahitaji uwajibikaji na hizo sio part time job ni full time job inabidi achague mojawapo kuna kipindi inabidi afatilie maswala ya uhamisho wa wachezaji au kusafiri na timu inapobidi
 
Kalibu viongozi wote wa Simba sc, wanakazi nyingine wanazozifanya nje ya Simba sc.
Ndio maana unaona Simba imetulia.
Na wameajiriwa huko kama huyo Gonzales.

Ndio maana unayaona haya mafanikio.


Sent from my MI MAX 2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom