Gagurito
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 5,600
- 803
Ndugu wanaJF wenzangu, natumai mu wazima wa afya jema na mpo tayari kubadilishana mawazo km kawaida yetu.
Napenda kuanza kwa kuwatakeni radhi pale mawazo yangu yatakapo contradict na uelewa wenu, Haya ni mawazo binafsi yatokanayo na uelewa wangu.
Ndugu wanaJF nitambuavyo mimi na ndivo ilivyo ni kwamba Chama cha Demokrasia na Maendeleo CDM kimapatwa kuungwa kwa wingi na wasomi, wanazuoni, wananchi na wafanyakazi wenye uelewa mkubwa wa mambo, isitoshe wabunge wake karibia wote ni wasomi walio na shahada katika fani na taaluma mbali mbali.
Ndugu wamaJF nadhani ninyi ni mashaidi, ktk siku za karibuni CDM kiliandaa Maandamano yaliyopokelewa vilivyo na wananchi hasa wale wa Kanda ya Ziwa, maandamano yaliyofanikiwa kuamsha hofu kwa Chama tawala pamoja na serikali yake, hofu iliyosambaa mpaka kwa Msajili wa vyama vya siasa na mpaka kutishia kukifuta chama cha CDM.
Swali langu kuu hapa wanaJF ni juu ya mwenendo wa siasa nchini, rafu zichezwazo na ushiriki wa wanachama na wananchi wa kawaida ktk siasa. Hata najaribu kuhuhisha wingi wa wananchi wajitokezao ktk mikutano, uhodari wa wanachama, wafuasi na wabunge wa CDM Kielimu na ktk ujengaji wa hoja u mkubwa, sasa inakuwaje washindwe? Na nini kifanyike wasishindwe? Na nin msaada wa wasomi ambao ni hazina ktk chama kwa CDM?.
Ndugu wanaJF nawasilisha hoja!
Napenda kuanza kwa kuwatakeni radhi pale mawazo yangu yatakapo contradict na uelewa wenu, Haya ni mawazo binafsi yatokanayo na uelewa wangu.
Ndugu wanaJF nitambuavyo mimi na ndivo ilivyo ni kwamba Chama cha Demokrasia na Maendeleo CDM kimapatwa kuungwa kwa wingi na wasomi, wanazuoni, wananchi na wafanyakazi wenye uelewa mkubwa wa mambo, isitoshe wabunge wake karibia wote ni wasomi walio na shahada katika fani na taaluma mbali mbali.
Ndugu wamaJF nadhani ninyi ni mashaidi, ktk siku za karibuni CDM kiliandaa Maandamano yaliyopokelewa vilivyo na wananchi hasa wale wa Kanda ya Ziwa, maandamano yaliyofanikiwa kuamsha hofu kwa Chama tawala pamoja na serikali yake, hofu iliyosambaa mpaka kwa Msajili wa vyama vya siasa na mpaka kutishia kukifuta chama cha CDM.
Swali langu kuu hapa wanaJF ni juu ya mwenendo wa siasa nchini, rafu zichezwazo na ushiriki wa wanachama na wananchi wa kawaida ktk siasa. Hata najaribu kuhuhisha wingi wa wananchi wajitokezao ktk mikutano, uhodari wa wanachama, wafuasi na wabunge wa CDM Kielimu na ktk ujengaji wa hoja u mkubwa, sasa inakuwaje washindwe? Na nini kifanyike wasishindwe? Na nin msaada wa wasomi ambao ni hazina ktk chama kwa CDM?.
Ndugu wanaJF nawasilisha hoja!