nivoj.sued
JF-Expert Member
- Jul 14, 2009
- 221
- 190
....Kama Chadema na upinzani kwa ujumla mtazamo wao ni kuwa kuna uvunjwaji wa katiba katika eneo hilo na kuna kundi la watu wanakubaliana na mtazamo huo, basi wanayo haki kushirikiana na viongozi wa dini wenye mtazamo sawa na wao katika eneo hilo, ili kuzuia huo "uvunjaji wa katiba" kwa maana hao viongozi wa dini watakuwa wanatekeleza sehemu ya wajibu wao!Na mgongano huu wa kimtazamo sio dhambi!
Vyama vya siasa, vyama vya kidini, vyama vya kiuchuni, na makundi mengine katika civil society yanasajiliwa kwa mujibu wa sheria tofauti. Na hivyo, yanakuwa regulated kisheria. Sheria husika zina vifungu kwa ajili ya kutunza nidhamu ya vyama hivi. Kifungu kimojawapo ni kufuta chama. Kwa hiyo, hata kama "mgongano huu wa kimtazamo sio dhambi!" sio dhambi, lakini bado ni jinai. Jitahidi kutafakari vema kuhusu legal parameters husika.