Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,276
Chama cha mapinduzi (CCM) Zanzibar kinatoa indhari kwa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuhusiana na propaganda chafu, za uongo na upotoshaji zinazoendelea kusambazwa na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad ndani na nje ya nchi, dhidi ya Serikali mbili zilizoko madarakani chini ya chama cha mapinduzi na viongozi wake.
Taarifa ya CCM Zanzibar kwa vyombo vya habari iliyotelewa ofisi kuu ya CCM Zanzibar, inasema tokea kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa marejeo imekuwa ikishuhudia matukio mbalimbali ya hujuma ambazo chanzo chake ni kauli za uchochezi, uongo na upotoshaji zilizotolewa hadharani na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad katika ziara zake kwenye maeneo tofauti unguja, pemba na nje ya Zanzibar.
Wana CCM na viongozi na wananchi wa Zanzibar wameshuhudia kuchomwa kwa mshamba ya karafuu, kuharibiwa mazao ya wakulima, na watu hasa wanachama na wafuasi wa ccm, kuchomewa nyumba zao, wananchi kushawishiwa kutoitambua Serikali,halali iliyoko madarakani pamoja na matukio kadhaa yenye kuashiria uvunjifu wa amani.
Jumatano ya tarehe 15 juni 2016 katibu mkuu huyo wa CUF kupitia Televisheni ya "Voice of America" (VOA) alishtumu Serikali za Tanzania na viongozi wake kwa madai tofauti ya uongo ikiwemo kile alichodai kukosa uwajibikaji na ukiukwaji wa makusudi wa misingi ya utawala wa sheria.
Chama cha mapinduzi Zanzibar kinatoa wito kwa serikali zote mbili na vyombo vya ulinzi na usalama kuacha kufumbia macho vitendo vinavyofanywa na kiongozi huyo wa upinzani kwani athari za badae zinaweza kuwa kubwa kiuchumi, kisiasa, kijamii kwa jumla.
Kwa maoni ya CCM Zanzibar, jitihada za maalim Seif hazina lengo la kutaka kurejewa uchaguzi wa Zanzibar ambao umefanywa kwa mujibu wa sheria za nchi, bali zinalenga kujitafutia umaarufu alioupoteza kutokana na ubinafsi wake wa kuwakataza wafuasi wake kushiriki uchaguzi wa marudio, jambo ambalo limewanyima fursa muhimu kisiasa ya kutoa hoja za sheria ndani ya- Baraza la Wawakishi.
CCM inawaomba wananchi kutobabaishwa na kauli za uchochezi na uasi zinazolewa na maalim Seif Sharif Hamad, ambaye kuna kila dalili za chama chake kupoteza mwelekeo wa kisiasa badala yake wanatafuta mwelekeo mwingine ambao kamwe nchini Tanzania haukubaliki, hakuna historia ya vita wala uasi.
Chama cha mapinduzi kinawasisitiza wananchi kwamba hakuna uchaguzi kabla ya mwaka 2020 na hakuna Serikali nyingine itakayowekwa madarakani kwa kile kinachodaiwa kumaliza migogoro wa kisiasa Zanzibar.
Chanzo: Zanzibar yetu
Taarifa ya CCM Zanzibar kwa vyombo vya habari iliyotelewa ofisi kuu ya CCM Zanzibar, inasema tokea kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa marejeo imekuwa ikishuhudia matukio mbalimbali ya hujuma ambazo chanzo chake ni kauli za uchochezi, uongo na upotoshaji zilizotolewa hadharani na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad katika ziara zake kwenye maeneo tofauti unguja, pemba na nje ya Zanzibar.
Wana CCM na viongozi na wananchi wa Zanzibar wameshuhudia kuchomwa kwa mshamba ya karafuu, kuharibiwa mazao ya wakulima, na watu hasa wanachama na wafuasi wa ccm, kuchomewa nyumba zao, wananchi kushawishiwa kutoitambua Serikali,halali iliyoko madarakani pamoja na matukio kadhaa yenye kuashiria uvunjifu wa amani.
Jumatano ya tarehe 15 juni 2016 katibu mkuu huyo wa CUF kupitia Televisheni ya "Voice of America" (VOA) alishtumu Serikali za Tanzania na viongozi wake kwa madai tofauti ya uongo ikiwemo kile alichodai kukosa uwajibikaji na ukiukwaji wa makusudi wa misingi ya utawala wa sheria.
Chama cha mapinduzi Zanzibar kinatoa wito kwa serikali zote mbili na vyombo vya ulinzi na usalama kuacha kufumbia macho vitendo vinavyofanywa na kiongozi huyo wa upinzani kwani athari za badae zinaweza kuwa kubwa kiuchumi, kisiasa, kijamii kwa jumla.
Kwa maoni ya CCM Zanzibar, jitihada za maalim Seif hazina lengo la kutaka kurejewa uchaguzi wa Zanzibar ambao umefanywa kwa mujibu wa sheria za nchi, bali zinalenga kujitafutia umaarufu alioupoteza kutokana na ubinafsi wake wa kuwakataza wafuasi wake kushiriki uchaguzi wa marudio, jambo ambalo limewanyima fursa muhimu kisiasa ya kutoa hoja za sheria ndani ya- Baraza la Wawakishi.
CCM inawaomba wananchi kutobabaishwa na kauli za uchochezi na uasi zinazolewa na maalim Seif Sharif Hamad, ambaye kuna kila dalili za chama chake kupoteza mwelekeo wa kisiasa badala yake wanatafuta mwelekeo mwingine ambao kamwe nchini Tanzania haukubaliki, hakuna historia ya vita wala uasi.
Chama cha mapinduzi kinawasisitiza wananchi kwamba hakuna uchaguzi kabla ya mwaka 2020 na hakuna Serikali nyingine itakayowekwa madarakani kwa kile kinachodaiwa kumaliza migogoro wa kisiasa Zanzibar.
Chanzo: Zanzibar yetu