CCM yawa rasmi Chama Cha Mafisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Date::8/18/2009
CCM yawafunga midomo vinara wa kupinga ufisadi
Na Habel Chidawali, Dodoma
Mwananchi




HALMASHAURI Kuu ya CCM juzi ilifikia uamuzi wa aina yake baada ya kuunda kamati maalumu ya kuwashughulikia wabunge wake wanaoikosoa serikali ya chama hicho tawala, huku ikimwekea kinga rais wa serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.


"Bunge limeanza kuwa kama mchezo wa (kikundi cha televisheni cha vichekesho) The Comedy," alisema katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, John Chiligati wakati akizungumza na waandishi wa habari jana.


"Yaani kila mtu anafanya mambo yake mwenyewe, hali ambayo inaweza kusababisha watu kurushiana hata viatu ndani ya Ukumbi wa Bunge, sasa hali hii maana yake nini?

"Kwa hiyo tumesema inatosha, hapo tulipofikia tusiendelee mbele. Wanaoropoka ovyo ni walevi na tumeona kuna kundi dogo ambalo limejiona kama ni wateule wa kuzungumzia sakata hilo (la ufisadi) bila ya kujua wabunge wote wana haki ya kuzungumzia suala hilo, lakini kwa utaratibu tena kwa kupitia katika vikao vya kamati za wabunge."


Tamko hilo la Chiligati limetolewa mwishoni mwa kikao cha Nec ambacho imeripotiwa kuwa kilimweka kitimoto Spika Samuel Sitta kwa madai kuwa analiendesha Bunge kwa kuwapa upendeleo wabunge walio katika kundi lake ambao wamekuwa wakipiga vita ufisadi.


Katika kikao hicho cha Nec, wachangiaji wengi walitaka Spika anyang'anywe kadi ya CCM kwa madai kuwa amekuwa akiruhusu na kushabikia mijadala inayoichafua serikali na chama hicho kikongwe.


Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maazimio ya kikao hicho, Chiligati alisema uamuzi wa kuunda kamati hiyo umefikiwa ili kurudisha nidhamu ndani ya chama hicho tawala.


Kwa mujibu wa Chiligati, kamati hiyo ya watu watatu itaongozwa na rais wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, spika wa zamani, Pius Msekwa na waziri wa zamani, Abdulrahman Kinana.


Alisema kamati hiyo itawashughulikia wabunge wote wanaoibomoa serikali bungeni na adhabu yake kwa watakaopatikana na hatia ni kuondolewa madarakani au kufukuzwa kabisa uanachama.


Alisema kamati hiyo imepewa jukumu kuhakikisha wabunge wa CCM na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa chama hicho wanarudi katika nidhamu ya chama kwa kuacha malumbano yasiyokuwa ya msingi.


Alisema kitendo cha wabunge wa CCM kuwashambulia viongozi wa CCM, wakiwemo mawaziri, si cha kiungwana na kwamba kimekuwa kikidhalilisha chama na baadhi ya Watanzania.


Katika mkutano uliopita, wabunge wengi waliwashambulia mawaziri na Baraza la Mawaziri wakilituhumu kubariki mikataba ya kifisadi na ilifikia wakati mbunge mmoja aliomba Mungu alilaani kwa sababu ya ubinafsi.

Katika hali iliyoonyesha vita hiyo kuwa kubwa, wakati fulani Spika Sitta alisimama bungeni kushambulia magazeti yaliyoripoti tuhuma za ufisadi kwenye ofisi yake, akisema ni ya mafisadi na hivyo kuomba ulinzi zaidi kutoka kwa waziri mkuu kwa madai kuwa usalama wake sasa uko shakani.


Kabla ya kikao cha Nec, makamu mwenyekiti wa zamani wa CCM, John Malecela aliamsha mjadala wa nafasi ya wabunge wa chama hicho kwenye uchaguzi ujao aliposema kuwa, wengi watapoteza viti vyao kutokana na tuhuma za ufisadi, kauli ambayo ilichochea mjadala mkali.


Katibu wa CCM, Yusuf Makamba alimjibu kwa kusema kuwa, haoni kama kuna mafisadi wala kama chama hicho kitakuwa kwenye wakati mgumu mwaka 2010, lakini akatabiri ushindani mkubwa ndani ya chama hicho tawala.

Spika Sitta aliingia kwenye mjadala huo na kusema kukubaliana na Malecela kuwa wabunge wengi wa CCM watakuwa kwenye wakati mgumu.


Baadaye Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Makongoro Mahanga akaibuka na kukemea mjadala huo, akisema wale wanaodai wanapambana na ufisadi, hawana budi kuwataja; kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria au kuwaripoti kwenye chama na kwamba kupambana nje ya vikao ni kuichafua CCM, kauli ambayo imerejewa na Nec.


Chiligati pia alisema kuwa, CCM imewaonya viongozi wake, wakiwemo wabunge, wanaomshambulia rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na kuwataka kuacha tabia hiyo mara moja.


Mkapa, ambaye aliingia Ikulu akijulikana kama mtu safi (Mr Clean), amekuwa akituhumiwa kwa ufisadi na baadhi ya wabunge wa CCM na wa upinzani kutokana na kununua mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira kwa bei ndogo, kuanzisha kampuni ya ANBEN akiwa ikulu na kutumia ofisi hiyo ya serikali kuendesha shughuli zake binafsi za kibiashara.


Lakini jana Chiligati alisema mkutano wa siku mbili wa Nec umewakumbusha viongozi wa CCM na Watanzania wote umuhimu wa kudumisha utamaduni wa kuwaheshimu na kuwaenzi viongozi wastaafu hasa marais.

Chiligati alisema Nec imesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu kumshambulia kwa maneno makali na kejeli Rais Mkapa huku wakisahau mazuri yote aliyoyafanya katika kipindi chake cha uongozi.


Alisema Mzee Mkapa katika kipindi cha uongozi wake alifanya mambo makubwa, ikiwemo kuinua hali ya uchumi, kuendeleza miundombinu, huduma za kijamii, elimu pamoja suala la maji.


"Hayo yote ni mambo mazuri, lakini bado Watanzania wanaona kuwa alichokifanya Mkapa kilikuwa ni kazi bure, jamani sisi ni watu gani tusiokuwa na shukrani yaani kila jambo kwetu ni baya, tukumbuke kuwa nchi hii ilikuwa katika hali ya kuwa mufilisi; ilikuwa haikopesheki lakini sasa tunakopesheka," alisema Chiligati.


"Mkapa anastahili pongezi sio kejeli; anastahili heshima sio dharau na pia anastahili kuenziwa sio matusi." Kwa mujibu wa Chiligati Nec imewataka Watanzania wote na wana-CCM wenye nia njema na Tanzania kumwacha kiongozi huyo apumzike kwa amani bila ya kumbughudhi na kuongeza kuwa, inasikitisha zaidi pale wana-CCM wanaposhiriki kumkejeli.
 
Chama Cha Majambazi na Mafisadi (CCM) kinapokuja na maamuzi kama hayo ya kuwalinda, kuwatetea na kuwapongeza Majambazi na Mafisadi wenzao ni kitu ambacho kilitegemewa. CCM haipo kwa maslahi ya watanzania bali kundi la wachache wanaoihujumu Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Itikadi ya CCM ni Ujambazi, Ufisadi, Kuhujumu Uchumi, Kuiba Rasilimali za Nchi, Kutoheshimu Katiba ya Nchi, Kuiba kura wakati wa Chaguzi mbalimbali, Kutoheshimu haki za msingi za Watanzania na kuhakikisha maslahi ya Chama yanapewa kipaumbele huku wakipuuzia maslahi ya Taifa.
 
bha ndugu,

Umefika wakati sasa wa watu kuelimishwa kuhusu Katiba ya nchi na Sheria jamani,

Ivi ukiwa Raisi na ukafanya mazuri ndio unayo haki ya ku miander the Katiba ya nchi na sheria zake kwa kujineemesha???? Look back to CHILE what happened to Augustine Pinoche nakuitendea mema Chile kukuza uchumi wa nchi ile kumbuka kuingia kwake madarakani aliingia kwa mtutu sasa leo nchi inamafanikio lakini Katiba ilimgeuka akafunguliwa mashitaka, iwe leo sisi ati twajifanya ijua sheria, haya aliyo yaongea chiligate yatakuja mtokea hato amin aombe kwa mungu amchukuwe mapema maana mkono wa sheria ukijapita utawakumba wengi ngojeni.

Mr.GEEQUE ulisema Chama cha Majambazi na mafisadi au Complete Corrupted Members?? me nadhani hao ni wamekiingilia chama kwa kudandia wasomeni historia zao jamani kuna watu sio kama hao ndani ya CCM, ila hao baadhi ndio wakichafua chama ila dawa yao iko jikoni tulia "usiwashtue we waachetu watashtukia issue" watafurahi wenyewe siku ngoma ikibadiri mdundo kila mmoja atuona mlango wakutokea,ngoja muda unawadia
 
Sitta, Kilango, Kimaro, Selelii, Mwakyembe, Ole Sendeka, Eng Manyanya na wale wote wabunge wa CCM mnayofanya kazi yenu kwa ajili ya maslahi ya umma na Taifa zima la Tanzania....msitishiwe nyau....wakiwanyang'anya kadi chafu za CCM mtapata kadi safi za CHADEMA na 2010 mtaendelea kuwa wabunge wa majimbo yenu.

Aluta continua.....mafisadi mpaka waishe.
 
Nafikiri hapa ndipo kipimo cha utetezi wa wanyonge kinapoweza kutumika, nataka kuamini hawa wanaokusudiwa hapa kuheshimu maslahi ya Chama wanahesimu pia maslahi ya Taifa. Inaeleweka ni vigumu sana ku -balance the two,kwa vile km mwanachama wa chama na hasa kiongozi unapaswa kuwa tayari kulinda siri za chama. Lakini je? Hizi ni siri za chama? Haya ni maslahi ya chama? Huu ufisadi unajumuisha chama chote...ni mikakati ya chama? Hivi si watu fulani tu ndani ya chama ndio wanufaika wa shughuli hizi mbovu zinazoumiza mamilioni ya watanzania?

Tutasubiri kuona ni akina nani watakuwa na ujasiri wa Martha Karua! Call a spade by its name na kuachia madaraka kama hayawawezeshi kufanya kazi bila kujipaka tope walilojipaka mafisadi. Kiongozi wa kweli atasimamia maslahi ya Taifa hata akiwa nje ya Chama na atakumbukwa kwa mchango wake daima. Je wapo tayari kuachana na Uheshimiwa itakapolazimu?
 
Napata uchungu sana ,kwa mtindo huu Demokrasia imeshindwa Tanzania na sasa ili kuwe na uwiano sawa na mgawanyo sawa wa raslimali ni bora kurejea katika mbinu kongwe ya uanamapindui ili sasa tuanzie hapo.Ndiyo maana naendelea kuwaheshimu akina Fidel Castro,Che Guevara,Col.Muamar Gaddaffi,Evo Morales wa Bolivia,Hugo Chavez wa Carcas Venezuela na hata Yoweri Museven.....hawa ni ma-role model wangu kwa kusema kweli. Si mapinduzi yote ni haramu,hwa jamaa wote walifanya mapinduzi ambayo ukifutilia kwa makini uchumi katika nchi zao ulianza kuwa stable,sasa naona CCM watanifanya nibadili muelekeo wangu wa kisiasa.

Siwezi kuvumilia kuona watanzania wakiendelea kuwa maskini huku CCM wakiendelea ku-play Delay tactics zao ili wabakie madarakani huku majirani zetu wakiendelea kutukejeli kila siku,Ni Lazima Heshima ya Mtanzania irudi! Roho inaniuma sana,yaani hata fikra mbadala CCM wanazikemea,hwa ndiyo wanotulazimisha wengine kutumia njia haramu,potelea mbali.Taifa gani ambalo wananchi wake ni maskini,wanakufa kwa maradhi,huku tunakosa mbinu mbadala za kukuza uchumi kwa sababu ya wapuuzi wachache? Hili silo taifa walilopigania babu zetu kama akina Mkwawa,Mirambo,Mangi sina,kimweri au akina Jk Nyerere,Bibi Titi,mzee kizota na wengineo,Mungu awalaze Pema Peponi.Leo hii viongozi wetu wmegeuka kuwa mawakala wa unyonyaji,wanatumiwa na wahindi,wachina na wazungu mliowakataa kututawala.

CCM ILAANIWE! MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Asante kwa mjadala huo. Lakini tukiondoa jazba, CCM na serikali yake nadhani wanadhana mbaya juu ya wananchi. Huenda wanafikiri kila mtanzania kalala usingizi mzito kiasi kwamba haoni hawa jamaa wanachokifanya. They have a lot of negatives na wakiambiwa badala ya kujisafisha wapate nguvu zaidi wao hutumia ubabe zaidi.

Ikumbukwe hata Roma empire haikuwahi kudhania itakuja potea kwa jinsi walivyokuwa na nguvu. Anayekuambia juu ya uchafu wako anakupenda upeo. ni uungwana kukubali usafishike, au la utaishia pabaya. Kina Kingunge, Chiligati, na wengineo wanapaswa kuangalia sana. Kuhifadhi uozo sio neema. Mkataa pema pabaya panamwita.

Kuna wasafi sana ndani ya CCM, japo mimi sio wanachama, wasafi hao hawaropoki hovyo. Bahati mbaya waropokaji wote ni waganga njaa. Heri wao wanaopendwa na watu, maana hao 2010 ni yao. Ole wao mafisadi, maana hao wameshiba leo ili wajiondoe milele machoni pa watu.

Leka
 
Wafanye yote lakini ipo siku watakiona cha mtema kuni. Na nina hakika watakaoleta mabadiliko watatoka humo humo CCM. hakuna atakeyeweza shindana na muda.
 
WAKATI WA KUTISHANA NA KULINDANA UMEKWISHA WABUNGE MLIOTISHWA ACHIENI NGAZI NA WATANZANIA WALIO WENGI WATAWAUNGA MKONO ,SEIF SHARIF HAMADI NA WENZAKE WALIFUKUZWA KUTOKANA NA SABABU HIZO HIZO ZA KUPINGA NDANI YA CHAMA , HADI HII LEO wanakubalika ndani ya jamii na wanaungwa mkono 100% na ukweli waliokuwa wanao wa kuwatetea wananchi umepokelewa kwa mikono miwili na ndio leo hii tukaona msimamo wa Pemba ni kutokana na ukweli kuwa ndani ya CCM hakuna maendeleo kwa mwananchi wa kawaida na anapotokea mbunge kutetea haki basi anaambiwa atoke chama ,jamani tokeni kwenye hicho Chama ,CCM si Chama cha kumletea mwananchi wa kawaida maendeleo na mapigano yenu ndani ya Chama hicho yataishia njiani au kupoteza roho zenu kwa maradhi ya ghafla na ndio hivyo mshaundiwa kauli ya machinja chinja ,kazi kwenu kubaki huko au kuondoka na mapema maana kama ni watetezi wa kweli hamtanyamazishwa na kauli za vitisho hivyo kamati itabidi itumie njia mbadala za kuwanyamazisha ,sijui ni zipi ila wanasema wana njia kibao.
 
Bubu Umewajuaje? Kijani, Njano, Panga, Jembe, Nyundo sisi wote tunaamini ni CCM, Ila hawa wenzetu moyoni mwao, vitendo vyao na matamshi yao kweli yanaandika Mafisadi waliovaa nembo ya CCM
 
Huu ndo wakati wa kupambania yupi mkweli na yupi alitumia hii fimbo ya ufisadi kujifagilia mwenyewe.Si wote waniitao Bwana bwana wataurithi ufaulme wa mbinguni.
Mwakyembe na wenzake wachague moja ni nani watakayemtumikia kama ni wananchi au chama cha mafisadi a.k.a. CCM.
Historia inatukumbusha kuwa mwisho wa mafisadi siku zote ni pabaya mkumbukeni fisadi mkuu Mabutu alizikwa na watu 2.
CCM msifikiri nchi hii ni yenu hicho kiambaza cha ujinga kitakapo toweka machafuko mtayashuhudia. Hatuwezi kuvumila kuona kundi la watu wachache wakiishi maisha ya neema na wengine hata mlo mmoja ni shida acheni ujinga huo.
MUNGU BABA UISHIE MILELE UTAENDELEA KUONA TAIFA LA WATU WAKO LIKIENDELEA KUNYANYASWA NA KUONEWA HADI LINI? BABA IMETOSHA SASA. BABA TUNALAANI MIPANGO YOTE YA MAFISADI NDANI YA CCM BABA WAVURUGE WASIELEWANE ILI HATIMAYE TUISHI KWA AMANI NA UPENDO.Mungu Ibariki Tanzania
 
MUNGU BABA UISHIE MILELE UTAENDELEA KUONA TAIFA LA WATU WAKO LIKIENDELEA KUNYANYASWA NA KUONEWA HADI LINI? BABA IMETOSHA SASA. BABA TUNALAANI MIPANGO YOTE YA MAFISADI NDANI YA CCM BABA WAVURUGE WASIELEWANE ILI HATIMAYE TUISHI KWA AMANI NA UPENDO.Mungu Ibariki Tanzania

Kaka utamaliza data za dini hawa ni mapagani waliojificha ndani ya makanisa na misikiti hawana tofauti na mashetani,hivyo utawaona nao wakiingia wakitoka makanisani na misikitini ,yaani hata kuomba dua wao ndio wa mbele , wanaonekana wana dhiki ile mbaya.

Hebu watazame nyuso zao wengi wao zinaonekana kama waliopigwa na ukimwi au waliotoka kwenye nchi yenye njaa kali ,lakini sio ni ubaya ulio ndani ya roho zao ,wanajaribu kuvaa vizuri ili wapendeze na badala ya kupendeza wao zinapendeza nguo nyuso zao zinabaki na alama ya uovu.



"Binadamu wazima na fahamu zao, huishi kama wanyama wa mwituni, ambao uhai wa kila mmoja wao hutegemea ujanja wake wa porini, ukali wa meno yake na urefu wa makucha yake. Upebari ni unyama" - Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. ,Je mafiasadi ni nani ? Mtu anafikia kusema Mkapa anastahili pongezi,sio vibaya lakini vilevile useme alivunja Katiba ,hapo utaeleweka una nia njema na Taifa hili na unaweza baadae kuleta excuse ,Mkapa muuaji ambae siku zake kuitwa Tha Hague zinahesabika.
 
Last edited:
Sitta, Kilango, Kimaro, Selelii, Mwakyembe, Ole Sendeka, Eng Manyanya na wale wote wabunge wa CCM mnayofanya kazi yenu kwa ajili ya maslahi ya umma na Taifa zima la Tanzania....msitishiwe nyau....wakiwanyang'anya kadi chafu za CCM mtapata kadi safi za CHADEMA na 2010 mtaendelea kuwa wabunge wa majimbo yenu.

Aluta continua.....mafisadi mpaka waishe.

Na wish na Mungu asaidie Mpate Wafuasi kutimiza ndoto za Baba wa Taifa.

Get tight guys!!
 
wanandugu mi nimechoka na haya mambo, hivi toka lini mwanadamu mstaarabu tena aliyechguliwa na wananchi wake, leo hii anasahau kumtetea yule aliyempa huo ulaji na kutengeneza mipango madhubuti ya kumkandamiza huyo huyo mwananchi tena masikini anayepata mlo mmmoja kwa siku! ni hatari sana.
kibaya zaidi na kinachoniuma inapotokea watu fulani wanaamua kutetea masilahi ya watanzania tena sisi masikini, anaonywa na kutishiwa kuvuliwa wadhifa na uanachama, navyojijua mimi nisiyeogopa kufa, hao jamaa wa sisi em wangenikoma, maana ningeichana kadi yao mbele yao na kuondoka zangu. na waniueeee maake wanasifika kwa tendo hili tena pale wanapoambiwa ukweli, reference kombe, kolimba, na wengine wengi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom