VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Baada ya mimi kuripoti humu JF jana kuwa CCM imeanza kujiandaa kwa Kampeni za Sumbawanga Mjini,jana kilifanyika kikao kingine. Nashukuru hawakunifahamu hivyo kutonitenga. Nikawepo tena kwenye Kikao cha pili cha dharura. Kikaoni,tukaanza kutemewa mkwara na 'Mwenyekiti' wa kikao ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM.
' Tumepokea taarifa kuwa yupo mtu humu anaweka mipango yetu wazi kwenye mitandao. Tumeshamjua. Tunamuonya asirudie. Na leo tumemtenga rasmi kwenye vikao vyetu vya kimkakati. Hatahudhuria hadi atakapotubu' alitamba 'Mwenyekiti' huyo. Nusura nicheke. Kweli CCM ni waongo na waliojaa propaganda. Mbona mimi nipo?! nilijiuliza kimoyomoyo.
Eti, taarifa ikatolewa kuwa mipango ya awali ya kumteua Mwigulu na timu yake ya Kampeni na nini sijui imesitishwa. Imesitishwa kwakuwa imevuja. Ikaundwa Kamati Ndogo itakayoshughulikia kisirisiri mipango hiyo ya Sumbawanga Mjini. Nami pia nimo. Raha ilioje! Mwaka huu,hadi kieleweke. Nilifundishwa jeshini enzi hizo kuwa ukitaka kumjua adui vyema,jiunge naye kwa juhudi zako zote. Ndivyo nilivyofanya. CCM hawatapata pakutokea.
' Tumepokea taarifa kuwa yupo mtu humu anaweka mipango yetu wazi kwenye mitandao. Tumeshamjua. Tunamuonya asirudie. Na leo tumemtenga rasmi kwenye vikao vyetu vya kimkakati. Hatahudhuria hadi atakapotubu' alitamba 'Mwenyekiti' huyo. Nusura nicheke. Kweli CCM ni waongo na waliojaa propaganda. Mbona mimi nipo?! nilijiuliza kimoyomoyo.
Eti, taarifa ikatolewa kuwa mipango ya awali ya kumteua Mwigulu na timu yake ya Kampeni na nini sijui imesitishwa. Imesitishwa kwakuwa imevuja. Ikaundwa Kamati Ndogo itakayoshughulikia kisirisiri mipango hiyo ya Sumbawanga Mjini. Nami pia nimo. Raha ilioje! Mwaka huu,hadi kieleweke. Nilifundishwa jeshini enzi hizo kuwa ukitaka kumjua adui vyema,jiunge naye kwa juhudi zako zote. Ndivyo nilivyofanya. CCM hawatapata pakutokea.