CCM yavunja upinzani Singida, CHADEMA 121 watimka

CCM yavunja upinzani Singida, CHADEMA 121 watimka

BigMan

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2007
Posts
1,096
Reaction score
135
mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida, Mgana Msindai ameisambaratisha kambi ya upinzani jimboni Mkalama, baada ya wanachama 182 wa vyama mbalimbali vya upinzani kurejea CCM. CHADEMA ndiyo iliyopata pigo zaidi baada ya wanachama wake 121 kukihama chama hicho na kurejea CCM.

Chanzo Gazeti la Mwananchi,Jumanne,Januari 8,2013
 
Unajua maana ya kuvunja? Unajua maana ya kusambaratisha?
 
Unajua maana ya kuvunja? Unajua maana ya kusambaratisha?

weka jina lolote lile upendalo cha msingi ni hao waliovua gwanda na kuvaa uzalendo
 
tatizo mtoa uzi hujui kuwa "mwanachi' hivi sasa iko kwenye 'payroll' ya magamba!!
 
Kwa hiyo baada ya kuivunja ChHADEMA huko Singida, Hao Wanyaturu na Wanyiramba wa Singida wameshushiwa bei za Mabati na Cement wajenge Nyumba Bora? ama wataendelea kubomokewa na Nyumba zao za Tembe kama tukio la tarehe 01.01.2013 huko huko Mkalama?

Kweli Watanzania wamelogwa na aliyewaloga alishafariki.
 
tatizo mtoa uzi hujui kuwa "mwanachi' hivi sasa iko kwenye 'payroll' ya magamba!!

kumbe mwanzo mwananchi ilikuwa kwenye payroll ya chadema? Sasa nimepata jibu kuwa huwa cdm wananunua waandishi wa habari!
 
Hongera kwa kutekeleza ahadi za jk kwa watu wa singida,!!!!...??
 
Mlitaka waripoti nin? Shughuli za maendeleo walizofanya? Hawana! Ndio maana wanapokea wanachama wao wenyewe wakiwabatiza majina ya WALIOHAMA CHADEMA, na Wadanganyika mnadanganyika na kuusahau Utanganyika! Huyo msanii wenu, sanaa yake inawapeleka pabaya CCM, wamesahau Too Much Is Harmful, mie yangu macho.
TUONANE 2015
 
Mbona ni kawaida! Siku Wakienda CUF, NCCR au CDM utashangaa
watu walewale wanasemwa wamekihama CCM na kuhamia chama hicho.
Kuna watu ndo biashara yao hiyo...
 
Chakushangaza watu wote 121 walikuwa na kadi mpyaaaaaa.....! Ni sawa na kuchukua pesa mfuko wa kulia, ukaziweka mfuko wa kushoto wa suruali then ukasema umepata pesa zaidi.
 
Msindai angoje M4C au vuguvugu la Mabadiriko wakiingia hapo wamepunguza hesabu sasa hivi mwanzo wangesema elfu nne
 
Join Date : 19th February 2007
Posts : 470
Rep Power : 702
Likes Received49
Likes Given9




Mtu wa siku nyingi post za kimbea Ndiyo maGT wa JF
 
Haya ndio ya Mwigulu kupokea wanachama 800 wakati mkutano watu hawazidi 600. Siasa za namna hiii ni mbaya sana unaweza kudedi siku ya siku.
 
weka jina lolote lile upendalo cha msingi ni hao waliovua gwanda na kuvaa uzalendo

hahahahaha KUVAAA UZALENDO KWANI GAMBA MLISHATOA??
KWELI UJINGA HAUNA KIPIMO HAAA!
 
nimetoka singida hiv karibun hususan kioboi kiukwel cdm wanaipeleka puta ccm kila wanapopita cdm,ccm wanafuatia kufuta nyao za cdm
 
mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida,mgana msindai ameisambaratisha kambi ya upinzani jimboni mkalama,baada ya wanachama 182 wa vyama mbalimbali vya upinzani kurejea ccm.chadema ndiyo iliyopata pigo zaidi baada ya wanachama wake 121 kukihama chama hicho na kurejea ccm.

Chanzo Gazeti la Mwananchi,Jumanne,Januari 8,2013

Hizo ni hadithi za kutunga. Jimbo la Mkalama lilikuwa ni sehemu ya jimbo la Iramba Mashariki, na CHADEMA hatujawahi kuwa na wanachama wanaofikia Idadi hiyo katika eneo unalolitaja. Na huyo aloandika hiyo habari ameandika kwa manufaa yake kujifurahisha. Ungezungumzia wanachama wengi kufikia Idadi hiyo maeneo kama ya Singida Magharibi, au Singida Mjini, au Singida Mashariki. Huko unapotaja umesema stori ya Uongo kabisa ili kuwafurahisha CCM wajione kuwa nao wapo. Kama kadi hizo zilifika Idadi unayotaja, basi ni zile za nyie kununua na kuwagawia ili mseme wamerudisha.
 
Watanganyika Bwana kazi kweli kweli ... Nasubiri kwa hamu sana tunawashukuru chama chamani mwisho kutuburuza kama nyoka imetosha sasa.
 
Hata wasira akijiangalia kwenye kioo ujiona yeye ni HB.So endelea kujipa moyo
 
Back
Top Bottom