kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,214
Kama tukiendelea kutawaliwa (sio kuongozwa) na CCM, tunaelekea kuzimu kwani tukijashtuka hatuna madini tena (yote yamechukuliwa na "wawekezaji"), hatuna gesi tena, tumeua mbuga za wanyama (maana tumeanza kuzivamia na kutengeneza viwanda vya magadi na kupitisha barabara za kisiasa kufukuza wanyama), tumechakachua elimu kwa ngazi zote na kuishiwa wasomi, tumekausha mito yote kwa kutokuwa makini na utunzaji wa mazingira (kukosa umeme na maji safi kwa matumizi ya nyumbani) na mwisho ni kushamiri kwa umasikini, ujinga na maradhi na kushuka kwa life expectancy labda kufikia miaka 30, kwa kuwa watu watakufa kwa njaa, watakufa kwa maradhi na kwa kukosa huduma nyingine za jamii.
Eee Mungu baba, this time uwe Mungu wa Tanzania, utuepushe na CCM wanatuangamiza
Eee Mungu baba, this time uwe Mungu wa Tanzania, utuepushe na CCM wanatuangamiza