Hapa uchama haupo,kwani wanaccm hawana watoto?hawana ndugu? Hili ni tatizo limetokea lazima chama kijipange kutoa majibu ili kisiharibu image yake,hata bill clinton alipopata kashifa ya ngono democrats hawakukurupuka,angalia mkurugenzi mtendaji wa imf na kiongozi wa france socialist party bw. Claus khan chama hakikurupuka.
Kwa hili kapuya ni lazima atoswe,hapa hakuna tena mazingira ya kumbeba vinginevyo chama kikubali kubeba madhara ya ubakaji wake kwenye chaguzi zijazo, na kumbuka vijana wake kwa waume ndo wapiga kura wengi kwa sasa.
Nasi wanachama wa kawaida tunasubiri tuone,je tutaongezewa msalaba wa kuutetea na viongozi wetu au watautua na kutuachia iliyopo? Manake hili linalotokana na matamanio ya kimwili na roho mbaya ya uuaji alibebe mwenyewe.hii penati aidake mwenyewe na si kubebesha chama mzigo.