Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Katika harakati zangu za kuwahamasisha watu kuchagua kwa busara katika uchaguzi ujao, nilikuwa naongea na mkazi mmoja wa Dar kuhusu suala hilo. Nilimueleza umuhimu wa kutochagua chama kinachoongozwa na mafisadi wa nchi yetu. Aliniambia kuwa, pamoja na ufisadi huo, chama hicho kina asili ya Nyerere kwa hiyo kina mvuto kwake. Ilibidi nitumie kama nusu saa hivi kumuelimisha kuwa CCM ya Nyerere sio ccm ya leo. Mwalimu alikuwa anapigania maendeleo ya Watanzania wote, wakati ccm ya sasa inakumbatia ufisadi na kulimbikiza mali kwa njia ya wizi kwa watu wachache.
Ni muhimu watu watambue kuwa itikadi ya Nyerere imefutwa katika chama hicho, bali wanatumia jina lake tu kujitajirisha kupitia migongo ya Watanzania. Mwalimu angefufuka leo na kuona mambo yanavyoendelea, nina hakika angefoka sana na kuwatia jela wote wanaohusika na kuchafua jina lake.
Ni muhimu watu watambue kuwa itikadi ya Nyerere imefutwa katika chama hicho, bali wanatumia jina lake tu kujitajirisha kupitia migongo ya Watanzania. Mwalimu angefufuka leo na kuona mambo yanavyoendelea, nina hakika angefoka sana na kuwatia jela wote wanaohusika na kuchafua jina lake.