CCM; Wenzetu mnajisikiaje?

CCM; Wenzetu mnajisikiaje?

hapana mkuu. Mambo ya msituni sio.nataka maridhiano yanayozingatia haki, usawa, ubinadamu na uadilifu kamili. Napinga watu wanaojifaharisha kwa dhamana ya uongozi na kuwa na vyombo vyenye nguvu ambayo wanavitumia kinyume na inavyotakiwa.napinga kumlaumu anaejilinda na kumpigia kifua anaedhuru.natamani watanzania wote tuungane katika hili.

nikweli hata mimi natamani hivyo lakini kwa mijitu hii ya ccm mpaka kutoka madarakani wataua wengi na kuumiza wengi sana mkuu!
 
Mkuu betlehem, umejitahidi kufikisha ujumbe wako vizuri. Mwenye macho atakuwa ameona na mwenye masikio atakuwa amesikia. Umetimiza wajibu wako vizuri lakini binafsi naamini kabisa kwamba haya yote wanayafanya wakijua na kwa utashi wao kamili.
 
Last edited by a moderator:
Well said. So Sad. Wanajisikiaje ???. Sio kwamba hawajui ila siku zote mtawala anayeona wananchi hawamuungi mkono, hufanya mambo ya kishetani kana kwamba watatawala milele. Ipo siku watajuta na kuvuta hisia ya kile ulichokiandika baada ya kuwa wameondoka madarakani.


  • Mwaka 2011, pale Ubungo mataa, kuna mtu alipanda juu ya nguzo ya umeme ya msongo mkubwa huku akidai kuwa yeyote akijaribu kumshusha, basi atajidondosha na kufa hapo hapo.Askari walileta greda la kijiko, wakambembeleza akakubali kushuka, wakaondoka naye mpaka polisi na kumfungulia kesi.Ndugu zetu wana CCM; Kuna anayeweza kujua kwa nini mtu huyu alikamatwa?

  • Ikitokea mwanafamilia anavamia wanafamilia wenzake, na kuwashambulia; Ni nani (chombo gani) anaepaswa kumkamata? .Jaalia CHADEMA wamekuwa na tabia ya kujishambulia wenyewe (Kama mnavyodai) na kule Arusha wamejishambulia wenyewe (mwana familia kaamua kuwashambulia wanafamilia wenzake kwa sababu yeyote ile) ni nani alipaswa kumdhibiti? Je! aliepaswa kumdhibiti na hakumdhibiti ninyi mnamtafsiri je? Je; Mnadhani wanachadema walioshambuliwa (hata kama wameshambuliwa na mwanachedema mwenzao) hawapaswi kuchukua hatua?

Kama ni ninyi kwa mfano; Kuna Mtu anawavamieni ndani kwenu, anawashambulia na kuwaibia; na chombo kinachotakiwa kumdhibiti hakifanyi hivyo (kwa sababu zozote zile), mkikiuliza kinasema anayewavamia huwa ni mwanafamilia mwenzenu, ninyi mngechukua hatua gani? Mfano kama mkisema mtakuwa mnajificha nyuma ya mlango halafu mvamizi akifungua mlango tu mnamkamata; Halafu ikatokea chombo ambacho ndicho kilitakiwa kiwe kinamkamata (Japo hakifanyi hivyo) Kinaibuka na kusema "ole wenu muwe mnamvizia muhalifu nyuma ya mlango", (Huku kikisisitiza kuwa kitahakikisha kinawadhibiti kama mtachukua hatua ya kudhibiti uhalifu mnaofanyiwa), nyinyi mtakitafsiri vipi chombo hiki ? Je; Mnadhani wanaofanyiwa hivyo sasa nao wakijiwa na fikra/tafsiri inayokuja kichwani kwako sasa; watatakiwa kulaumiwa?
WENZETU WA CCM MNAJISIKIA JE?

1. Mnajisikiaje ikiwa mnashambuliwa (bila kujali mshambuliaji ni nani) kisha mshambuliaji hakamatwi halafu ukitaka kujilinda, alietakiwa kumkamata mhalifu (aliyeshambulia) anakukabili kwa nguvu zote?

2. Unajisikiaje siku umevamiwa ndani ya familia yako, ukashambuliwa, (mtoto wako mdogo akafariki kwa kupigwa) halafu ukaripoti kwa vyombo husika vikakuambia utakuwa umejishambulia mwenyewe ili upate misaada na huruma?Utajisikia je?

3.Utajisikia je siku ukiwa unaumwa pengine na malaria (Si unajua wanadamu tumeumbwa kwa nyama) halafu umelazwa muhimbili, Ghafla unasikia sauti ikikupa pole na kisha unafungua macho; mbele yako unamuona mtu asiye na meno ya mbele,anatembea anachehemea huku ana makovu mengi usoni.Mkononi kabeba sabuni na chupa ya uji. Kwa mbali unakumbuka ni miongoni mwa watu ambao wewe uliwatuma askari wampige na kumsababishia hali hiyo (eti tu kwa kuwa alikuwa na mawazo tofauti na yako) Unajisikia je? Hivi unajisikiaje?


4. Unajisikiaje unapotembea njiani, halafu ukakutana na watu; watu wanaojua kwamba kuna uhalifu unatokea hata kusababisha mauaji na wewe wakati wote hoja zako ambazo umekuwa ukizitoa zinakuwa za kuukadhamiza upande wa wahanga na kuwatetea upande wa wahalifu; Hivi unajisikia je? Unadhani wanaokuona na kukutizama nao wanajisikia je?

5. Unaonaje ukijikuta katia mazingira ambayo kuna watu watatu. Mmoja anahisi anaweza kudhuriwa (kwa kuwa alishawahi kudhuriwa mara kadhaa) na hivyo anafikiri kujilinda (defensive) na wa pili anataka kudhuru (offensive) Hivyo hataki wa kwanza ajilinde (ili asije akapata upinzani), Na huyu wa tatu yeye anapingana na wa kwanza na hivyo kuungana na huyu wa pili. Wewe utajisikia je? na utachukua upande gani hata kimoyo moyo tu?

Najua wahusika si rahisi wa comment hapa. Ila nina uhakika watakuwa wanapata majibu ya ninachozungumza hapa na wataweza kujipima wao ni binadamu wa aina gani.Elewa majibu unayoyapata kwenye kichwa chako ndio majibu wanayoyapata wale unao watenda hivi leo.

Mama Anna Tibaijuka ; Wewe ni member wa humu na sijawahi kukusikia ukijihusisha kwenye siasa za chuki.Wewe ni waziri na uweza kukutana na wahusika wa mambo haya. Naomba uwaulize (natanguliza shukurani);Waulize wanajisikia je! kwenye mambo haya?


Mambo haya kimsingi yanahitaji diplomasia kubwa sasa ya kisiasa kwa sasa (vinginevyo ni hatari sana) na hilo linawezekana tu, ikiwa kutakuwa na nia njema hasa kutoka kwa upande unaowatenda wenzao.Ndugu zangu; Tunajenga vizazi vyenye mafundo ya chuki, hasira na roho za visasi; Hivi nani anajua vizuri saikolojia ya mtu anaedhani anadhulumiwa, anaonewa anakandamizwa na akijaribu kujitetea anazimwa kwa nguvu? Kwa asiyejua, na awasiliane na Dr.Kitila Mkumbo, amuombe amuazimishie vitabu vya Saikolojia.(Naamini pale UDSM vipo vingi).

Hivi ninyi wenzetu wa CCM, kwa nini mnawafanyia wenzenu na mnapenda wenzenu wafanyiwe vile msivyovipenda kufanyiwa ninyi? Kwa nini mnapenda kuwa na vitu ambavyo hampendi wenzenu wawe navyo? Kwa nini mnapenda wenzenu wafanye vitu ambavyo ninyi hamfanyi na msingependa kufanya? Wakati fulani mnawasababisha watu wapate jazba na mimi naona jazba ishaanza kunivizia.Ngoja ni ache.....





 
Nasikitika kwamba huu uzi unawahusu wana CCM Lakini mpaka sasa hakuna mwana CCM aliechangia.Kila anayeuona haraka anaukimbia.Kwa nini lakini ? au ndo kusema nia njema imekosekana!
 
Bila kumun'gunya maneno serikali yetu ni dhaifu na waoga wa changamoto maana katika hali ya kawaida haiwezekani wewe uwe unapiga watu na wenzako wakiianza kuchukua zoezi la kujihami unalalamika. Huo ni woga wa wazi wazi na udhaifu uliokithiri
 
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania na uwajalie hawa viongozi kuwa na hofu yako kuu ili wakatende sawa sawa na maagizo yako.
 
Back
Top Bottom