Nengonengo
JF-Expert Member
- Jul 8, 2014
- 305
- 61
CCM haipo Mwanza,.
Leo tarehe 30/06/2015 katika mahakama ya Wilaya kulikuwa na hukumu ya kesi zilizofunguliwa mahakamani na CCM za kupinga matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika 14 Disemba 2015 ambapo CCM waliangukia pua,leo WAMEUMBUKA ile mbaya baada ya mahakama KUTUPILIA mbali kesi hizo na kuwafanya wenyeviti wa CHADEMA kutangazwa kuwa washindi halali.
Mbaya zaidi ni pale ambapo hata ile mitaa ambayo wao (CCM) walishinda KIBABE nayo matokeo yake yametenguliwa!
Pole sana ambao hamjajitambua na kutambua kuwa CCM mwisho wao umefika! Muda huu sisi tuliojitambua kwa kuchagua CHADEMA katika mtaa wetu wa KILELENI kata ya KITANGIRI tupo tunagonga moja baridi,moja moto na nyama choma tukisherehekea ushindi!