tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,995
- 25,392
Kuna taarifa za chini chini kwamba serikali ya CCM imeuagiza uongozi wa TBC kusitisha kurusha matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni Dodoma ili kuwanyima fursa wananchi kufuatilia mjadala wa utunzi wa katiba utakaoanza ngwe ya pili kesho Jumanne. Lengo kubwa ni kuwafanya wananchi wasijue kinachoendelea ndani ya ukumbi wa bunge. Imeazimiwa kwamba TBC Taifa (RTD) warekodi kipindi hicho na kukihariri kwa kadri watakavyoona inafaa na kisha kukirusha kupitia redioni saa 4 usiku.
Aidha wamekipiga marufuku kituo cha Star TV kurusha mjadala huo moja kwa moja kama walivyokuwa wakifanya katika ngwe ya kwanza. Mkuu wa mkoa wa Dodoma Bi Rehema Nchimbi na wakuu wengine wa mikoa wameagizwa kuwazuia watu kujadili katiba hiyo katika mji wa Dodoma na mikoa mingine kwa kisingizio cha ‘kuwavuruga' wajumbe watakaoukuwa wakijadiliana bungeni. Baadhi ya vyombo vya habari, hasa vya binafsi, vimepigwa marufuku kusogelea ukumbi wa bunge wakati mijadala itakapokuwa ikiendelea. Wameelekezwa wasubiri mjadala ukiisha watakuwa wanapewa taarifa na katibu wa bunge mara moja kwa kila siku.
Ndugu zangu, huu ni udikteta. Naona sasa CCM inakaribia kabisa kuiingiza nchi hii katika machafuko. TBC inaendeshwa kwa kodi za umma. Sasa iweje wananchi wazuiwe kupata habari na kufuatilia michango ya utunzi wa katiba mpya? Hili jambo halikubaliki hata kidogo. Kama CCM wameamua kuwanyanyasa wananchi namna hii, nchi hii sasa itakuwa imegeuza kuwa ya kidikteta.
:israel:
Aidha wamekipiga marufuku kituo cha Star TV kurusha mjadala huo moja kwa moja kama walivyokuwa wakifanya katika ngwe ya kwanza. Mkuu wa mkoa wa Dodoma Bi Rehema Nchimbi na wakuu wengine wa mikoa wameagizwa kuwazuia watu kujadili katiba hiyo katika mji wa Dodoma na mikoa mingine kwa kisingizio cha ‘kuwavuruga' wajumbe watakaoukuwa wakijadiliana bungeni. Baadhi ya vyombo vya habari, hasa vya binafsi, vimepigwa marufuku kusogelea ukumbi wa bunge wakati mijadala itakapokuwa ikiendelea. Wameelekezwa wasubiri mjadala ukiisha watakuwa wanapewa taarifa na katibu wa bunge mara moja kwa kila siku.
Ndugu zangu, huu ni udikteta. Naona sasa CCM inakaribia kabisa kuiingiza nchi hii katika machafuko. TBC inaendeshwa kwa kodi za umma. Sasa iweje wananchi wazuiwe kupata habari na kufuatilia michango ya utunzi wa katiba mpya? Hili jambo halikubaliki hata kidogo. Kama CCM wameamua kuwanyanyasa wananchi namna hii, nchi hii sasa itakuwa imegeuza kuwa ya kidikteta.
:israel: