Wana wazimu!! Tutakula nao sahani moja kwani wengi wao tuna account zao za social media, namba za simu nk nk, labda waende kuzimu tu; tunao sambamba. tutatumia BBC na sauti ya ujerumani na VOA, magazeti ya ndani na nje ya nchi, makanisa na mpaka vikao vya harusi na mazishi kutoa maoni yetu na watayasikia hata wakiyapuuza ujumbe utakuwa umefika na hilo ndilo tunalotafuta na kwa kitendo cha kutaka kufanya black out ni kwa sababu ujumbe umefika na wanaugwaya!
BMK ni batili no matter the outcome; katiba ya CCM haitakuwa endelevu na haina uhalali katika jamii nzima ya Kitanzania, wakishamaliza kazi tutaanza upya kudai Katiba mpya na bora mpaka kieleweke; Aluta continua
Komandoo Salimin Amour aliwahi kuyafungia magazeti fulani ya huku bara; alipoambiwa yanasomeka online je atafanyaje kuhusu Inernet! akajibu; Hapo chacha!! hiyo itakuwa ngumu.
CCM hii ni karne ya 21, ya sayansi na tekelinalokujia, Serikali 3 hazikwepeki mnazichelewesha tu na ujumbe huo wataendelea kuupata.
bora mtu -------- anayejitambua kwamba hajui kuliko mtu mjinga asiyejua kwamba hajui!