Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
*Polisi yakiri kuwashikilia viongozi
Wakati jihudi za kuliokoa Jimbp la Bukombe liko katika hatihati za za kunyakuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zikipamba moto, viongozi wawili wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa wakinunua shahada kutoka kwa wapiga kura.
Habari kutoka Bukombe ambazo zimethibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Seleman Nyakipande, zinasema viongozi hao ni Juma Mhoja na Shadrack Paul, ambao ni makatibu wa Tawiu la Ushirombo na Msonga.
Alisema viongozi hao walikamatwa katika Kijiji cha Msonga, Kata ya Runzewe wakiwa tayari wamenunua shahada 185 za kupiga kura kutoka kwa wananchi ambao walikuwa wanarubuniwa na baadhi ya makada wa CCM ambao wako katika mkakakati wa kuliokoa jimbo hilo.
Viongozi hao walikuwa wakinunua shahada hizi kwa bei ya kati ya Sh 2,000 na 5,000 huku lengo likionekana kuwalenga zaidi wafuasi wa Chadema ili kudhoofisha nguvu iliyopo.
Kamanda Nyakipande alisema polisi inaendelea kuwafanyia uchunguzi watuhumiwa hao kwa kushirikiana na TAKUKURU kwa madai kuwa tukio hilo linaingiliana na Sheria ya Gharama za Uchaguzi.
Hali ya siasa katika jimbo hilo iko tete kutokana na upinzani mkali uliopo kati ya CCM na Chadema, sababu kubwa ni kutokana na kuwapo makundi katika CCM baada ya kura za maoni zilizoibua malalamiko mengi.
Chanzo: Tanzania Daima
Wakati jihudi za kuliokoa Jimbp la Bukombe liko katika hatihati za za kunyakuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zikipamba moto, viongozi wawili wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa wakinunua shahada kutoka kwa wapiga kura.
Habari kutoka Bukombe ambazo zimethibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Seleman Nyakipande, zinasema viongozi hao ni Juma Mhoja na Shadrack Paul, ambao ni makatibu wa Tawiu la Ushirombo na Msonga.
Alisema viongozi hao walikamatwa katika Kijiji cha Msonga, Kata ya Runzewe wakiwa tayari wamenunua shahada 185 za kupiga kura kutoka kwa wananchi ambao walikuwa wanarubuniwa na baadhi ya makada wa CCM ambao wako katika mkakakati wa kuliokoa jimbo hilo.
Viongozi hao walikuwa wakinunua shahada hizi kwa bei ya kati ya Sh 2,000 na 5,000 huku lengo likionekana kuwalenga zaidi wafuasi wa Chadema ili kudhoofisha nguvu iliyopo.
Kamanda Nyakipande alisema polisi inaendelea kuwafanyia uchunguzi watuhumiwa hao kwa kushirikiana na TAKUKURU kwa madai kuwa tukio hilo linaingiliana na Sheria ya Gharama za Uchaguzi.
Hali ya siasa katika jimbo hilo iko tete kutokana na upinzani mkali uliopo kati ya CCM na Chadema, sababu kubwa ni kutokana na kuwapo makundi katika CCM baada ya kura za maoni zilizoibua malalamiko mengi.
Chanzo: Tanzania Daima