CCM wanapenda namba lakini hawajui hesabu

CCM wanapenda namba lakini hawajui hesabu

mweusi asili
Unaona sasa thinking yako. . . . . .. watu wanaweka mawazo ya kuonesha mambo hayako sahihi we unaona kama wanalalamika. . . . . . .hiyo tu ni kasumba ya mabwanyenye uchwara.......

Sasa wewe ni decision maker, au think tank ya hii nchi, are you a policy maker, wewe unakaa kwenye baraza!!???
Wewe una influence gani katika kuwepo au kutokuwepo wa kiwanda "physically" ???!!! Hao ndio wanaotakiwa "wahakikishe uwepo wa viwanda" sio wewe, mimi wala raia mwingine mvuja jasho.......

Role yako wewe na mimi ni kununua bidhaa zenye ubora ili upate value for money wao wanahitajika kuhakikisha hizo bidhaa zinazalishwa humu nchini . . . . . . so badala ya kuungana nguvu na sie tunaotaka wenye madaraka wachukue wajibu wao we unaleta misemo ya J.F . Kennedy ambaye aliongelea kwenye industrialized country . . . . kwa watu wenye purchasing power na wanaojua standards na haki zao....

Halafu eti unataka watu watumie akili, ipi hiyo ambayo wewe unayo na watu wakitumia unaweza kwenda nao sambamba!!!!???


Wengi mmekuwa brain washed to an extent mna assume responsibilities za watu wengine na mnajilaumu kwa mapungufu yao. . .. . na vibaraka wengine mpo kwa ajili ya blame shifting kuwa kukosekana kwa viwanda ni mapungufu yetu wote.....waambie "people are up their senses".......
 
Last edited by a moderator:
Tulimumu nisihangaike kujaza seva kwa ku quot cmn.

Je una uhakika 2005 dolla iliuzwa kwa tsh 650?
Naomba uhakika juu ya hilo maana nikiangalia kumbukumbu zangu dolla ilkuwa inasimamia 1200

Ni 950 sio 650 naona kuna typing error.
 
Kwa hii nchi mkuu ni watu wachache sana watakuelewa yaani ndyo kwaanza wanashabikia Mafisad. na amin usiamin wanaweza kuchukua nchi hii tena Lo!
 
Achana na propaganda fanya maamuzi sahihi..kwa sababu sahihi.

Kuna watu wanapenda namba lakini hawajui hesabu. Kama na wewe ni mmoja wao tafadhali usisome makala hii.
Watanzania wengi na viongozi ni wagonjwa wa namba. Wanapenda namba lakini hawajui hesabu. Ukitaka wakushangilie we ongeza tarakimu tu kwenye namba. Wanapenda namba lakini hawajui hesabu!

Kama ulikua unamlipa mtumishi mshahara wa laki 5 mwaka jana mwaka huu mlipe laki 7. Atashangilia na kukushukuru. Kumbe hajui upande wa pili gharama za maisha zimeifanya hiyo laki 7 iwe sawa na laki moja ya mwaka jana. Yeye atakushukuru tu, kwa sababu anapenda namba lakini hajui hesabu.!

Naona wengi hamjanielewa. Ni hivi kuna faida gani kulipwa mshahara wa milioni mbili halafu ukauziwa sukari kilo moja sh.3000/=??? Si bora ulipwe laki 5 sukari uuziwe sh.500/= kwa kilo. Kama unapenda namba lakini hujui hesabu huwezi kunielewa.

Twende kwenye historia kidogo. Mwaka 2005 wakati Rais Mkapa anaondoka madarakani bajeti ya serikali ilikua Trilioni 7. Mwaka huu ni Trilioni 22. Wanaopenda namba lakini hawajui hesabu wameshaanza kushangilia eti "bajeti imekua"..

Ukweli ni kwamba bajeti haijakua ila imezidi kuporomoka. Lets calculate together.

Ni hivi. Mwaka 2005 bajeti ilikua Trilioni 7 na thamani ya dola moja ilikuwa sawa na Sh.950. So ukichukua Trilioni 7 ukigawanya kwa Sh.950/= utapata 10,769,230, yani Dola Bilioni kumi na milioni mia 7.

Mwaka huu bajeti ni Trilioni 22. Na thamani ya dola ni Sh.2250. Ukichukua Trilioni 22 ukigawanya kwa Sh.2250/= utapata 9,777,777 yani dola Bilioni 9 na milioni mia 7.

Hii ina maana kuwa bajeti ya mwaka huu (dola Bilioni 9) ni ndogo kuliko bajeti ya mwaka 2005 (dola Bilioni 10).

Maana yake ni kwamba kwa miaka yote 10 ya utawala wa JK tumepiga hatua 9 mbele tukarudi nyuma hatua 10. Halafu tunajipongeza.. Wanaopenda namba lakini hawajui hesabu hawawezi kunielewa.!

Haiwezekani bajeti ya mwaka 2005 iwe kubwa zaidi kuliko bajeti ya mwaka huu wakati mwaka huu mahitaji ni makubwa zaidi kuliko ya 2005. Watumishi ni wengi zaidi, miradi ya maendeleo ni mingi zaidi na hata population ni kubwa zaidi. So tulitegemea bajeti ya mwaka huu iwe kubwa zaidi. Kubwa maradufu kuliko ya mwaka 2005. Lakini cha ajabu imekua ndogo kuliko ya 2005. Halafu wabunge wa CCM wanaopenda namba bila kujua hesabu wanashangilia eti bajeti imepanda.

Tafsiri hii ya bajeti ina maanisha kuwa kwa miaka 10 ya utawala wa Kikwete tumeshindwa kwenda mbele japo hatua moja. Badala yake tumerudi nyuma kwa hatua moja (10-9).

Kwa lugha rahisi ni kuwa maisha ya leo yamekuwa magumu zaidi (in one decimal place) kulinganisha na maisha ya miaka 10 iliyopita.

Yani mtumishi aliyekuwa analipwa mshahara wa laki 3 mwaka 2005 aliishi maisha mazuri kuliko mtumishi anayelipwa milioni moja leo.

Unajua kwanini? Mwaka 2005 sukari kilo moja ilikua Sh.500. Kwa hiyo kwa mshahara wa laki 3 ulikua una uwezo wa kununua kilo 600 za sukari kwa mwezi. Leo sukari kilo moja ni sh.2200/= kwa hiyo kwa mshahara wa milioni moja unaweza kununua kilo 454 tu za sukari. Hapa tunasema purchasing power ya shilingi imeporomoka mara dufu. Wanaopenda namba lakini hawajui hesabu hawawezi kunielewa.!

Mwaka 2005 mfuko mmoja wa cement uliuzwa Sh.4500/= hadi 5000/=. Kwa maana hiyo mtumishi aliyelipwa mshahara wa laki 3 aliweza kununua mifuko 66 ya cement. Leo cement mfuko mmoja ni sh.20,000/= hadi 25,000/=. So mtumishi anayelipwa milioni moja ana uwezo wa kununua mifuko 40 tu ya cement. Laki 3 ya mwaka 2005 imekuwa kubwa kuliko milioni ya leo.

Mfumuko wa bei kuanzia mwaka 2005 hadi sasa ni wa kiwango cha asilimia mia nne (400/%). Maana yake ni kwamba bidhaa zimepanda mara 4 ya bei yake just for ten years.

Nyama iliyokua inauzwa kilo moja sh.1000/= sasa hivi inauzwa 4000/= hadi 6000/=. Mchele uliokua ukiuzwa Sh.350/= kwa kilo moja saivi ni 1500/=. Nauli ya daladala iliyokua sh.150 saivi ni 500/=. Mafuta ya taa lita ilikua sh.350/= saivi ni karibia sh.2000/=

Kimsingi kila bidhaa imepanda bei mara 4 au zaidi ya bei yake ya mwaka 2005. Tafsiri yake ni kwamba mfumuko wa bei (inflation rate) ni wa kiwango cha zaidi ya 400% (Hyper Inflation)

Katika uchumi inflation yoyote inayoanzia tripple digit na kuendelea ni "Hyper Inflation". Yani ni mfumuko wa bei wa kiwango kibaya zaidi unaoweza kuathiri uchumi wa nchi kabisa.

Nchi inapaswa kuwa na mfumuko wa bei wa kawaida (moderate inflation) ambao ni single digit. Yani mfumuko ukiwa wa kuanzia asilimia moja (1%) hadi tisa (9%) hiyo ni moderate inflation na haina athari kubwa kiuchumi. Hata nchi kama Marekani inflation rate yao ni moderate.

Lakini sisi tuna asilimia 400 za mfumuko wa bei. Hii ni hatari sana. Very soon tutawakaribia Zimbabwe au Somalia kuanza kutembea na hela kwenye matoroli. Hata wao walianza hivihivi.!

Thamani ya shilingi inaporomoka kila siku na watu wanashangilia. Huu ni "uzwazwa" wa kiwango cha Phd.

Jiulize embe lililokua likiuzwa sh.50 pale sokoni Buguruni leo linauzwa sh.50
 
Back
Top Bottom