mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,422
- 1,790
Kuna taarifa nimezipata muda huu kwa njia ya simu, kuwa CCM wameamua kuchakachua maoni ya Katiba Mpya kwa kusambaza Fomu kwa Wanachama ambao wanajua wataficha siri hasa viongozi katika matawi ya CCM, ili wazijaze na kisha kurudisha ofisini kwa ajili ya kukusanywa.
Kwa mujibu wa taarifa niliyoipata nikwamba katika ile fomu kuna mambo ambayo wanayahitaji yawepo, mfano Suala la Muungano, na madaraka ya Rais ikiwemo ya kuwa awe ndiye amiri jeshi mkuu.
Ukipewa hiyo fomu unatakiwa kutoa photocopy zisizopungua tano kisha unajaza na kuandika majina tofauti katika kila fomu na kurudisha ofisi ya chama.
Nimemuomba aliyenipa taarifa kuwa aniletee hiyo fomu aliyonayo kisha nitawawekea hapa. Ni mtu wa uhakika aliyenipa taarifa hii, ambaye pia ni kiongozi wa UWT katika tawi fulani.
Naomba kama kuna mwenye taarifa kuhusu suala hili na hiyo fomu kama ipo naomba atuwekee lakini na mimi nikiipata tu itakuwa hewani hapa.
MYTAKE: kama taarifa ikiwa ni hii, je, Tanzania tutapata Katiba Mpya kweli au itabadilishwa jina tu na kuwa ni ileile???????
MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
Kwa mujibu wa taarifa niliyoipata nikwamba katika ile fomu kuna mambo ambayo wanayahitaji yawepo, mfano Suala la Muungano, na madaraka ya Rais ikiwemo ya kuwa awe ndiye amiri jeshi mkuu.
Ukipewa hiyo fomu unatakiwa kutoa photocopy zisizopungua tano kisha unajaza na kuandika majina tofauti katika kila fomu na kurudisha ofisi ya chama.
Nimemuomba aliyenipa taarifa kuwa aniletee hiyo fomu aliyonayo kisha nitawawekea hapa. Ni mtu wa uhakika aliyenipa taarifa hii, ambaye pia ni kiongozi wa UWT katika tawi fulani.
Naomba kama kuna mwenye taarifa kuhusu suala hili na hiyo fomu kama ipo naomba atuwekee lakini na mimi nikiipata tu itakuwa hewani hapa.
MYTAKE: kama taarifa ikiwa ni hii, je, Tanzania tutapata Katiba Mpya kweli au itabadilishwa jina tu na kuwa ni ileile???????
MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!