Hapa Lumumba,ofisi ndogo za CCM Dar, sasa ni vikao mfululizo. Kamati mbalimbali zinaundwa na kupewa majukumu mbalimbali lakini yenye lengo moja:kuiadhibu Mtwara. Kwanini waandamane kupinga kuisafirisha gesi toka huko Mtwara hadi Dar es Salaam? Kwanini wamsaliti Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa nchi? Wapo Wajumbe wenzangu wanawaita Mtwara wahaini na wasaliti.
CCM imeapa kuidhibu Mtwara. Wanakamati tumepewa kazi ya kutafuta adhabu mujarabu na kuishauri Serikali. Nitakuja kuwaambia adhabu husika baada ya Kikao cha Jumatatu. Hali ni tete hapa Lumumba.Tutaonana siku hiyo.Jadilini lakini mjue hivyo
Wenu,
VUTA-NKUVUTE aka
Mzee Tupatupa