Phillemon Mikael
Platinum Member
- Nov 5, 2006
- 10,535
- 8,620
Askofu Bagonza amewahi kuandika Makala yake ya kifalsafa juu ya Haki ya binadamu kulia,
CCM wamekiri wenyewe kuwa walimuonea Lowassa na kuumiza roho na mwili hadi Ikafikia kumkata kwa kashfa ya kubuni ya Richmond, hadi akaamua kuhamia upinzani.
Lowassa aliamia upinzani hakuwa na madaraka lakini akawa na Faraja kubwa sana kuanzia kugombea Urais (na kushinda ambako hakutangazwa), mnakumbuka kimya kilichotawala nchi mwaka 2015 wakisubiri neno moja tu kutoka kwa Lowassa, akasema "Sitaki kuingia madarakani kwa kukanyaga dame“, mnakumbuka Magufuli hakuwa na confidence wala furaha alikuwa anajua hakushinda, hadi akaja kasisi Kutoka Nigeria TB Joshua.
Pamoja na kuwa hakushinda Lowassa alibaki na Amani na mara zote wapenzi wake walimpa Faraja kwa kumshangilia kila alipopita, huku naye akiwapungia kwa tabasamu, ndio Faraja iliyokua imebaki kwaka na mara kadhaa hata kwenye taa za barabarani akisimama vijana walikuwa wakimuona tu wanamfurahia.
Magufuli hakuwa na Amani kuona Lowassa pamoja tayari alikuwa amedhoofu anashangiliwa kila anakopita. Akaona ni lazima arudi CCM ili kuja kumuongezea nguvu, alitumia mbinu chafu ya kumkamata mdogo wake Rostam aitwaye Akram na kumpa kesi ngumu sana ambazo hazina dhamana ikiwemo kumiliki silaha za moto.
Familia ya Rostam ilichanganyikiwa ilikuwa ni kama kumteka nyara na kutaka ransom, ilibidi Rostam arudi haraka kuja kuhanghaika mdogo wake asifungwe maisha, sasa mchezo ulianzia hapo.
Magufuli alimdai price tag moja hadi nyingine na akatimiza baada ya kufanya kila kitu akamdai “Kichwa cha Lowassa“, mahojiano anayotoa Rostam kuwa yeye ndiye aliyemrudisha Lowassa CCM yana Siri kuu ambayo yeye anaongea Leo kwakuwa lowassa hayupo kusema ukweli
Lowassa alichukuliwa nyumbani kwake kirafiki na Rostam akaibukia kwa magufuli na akashangaa sana anatoka nje anakutana na waandishi wa habari wanamuuliza anajionaje kurudi CCM (watu wa karibu waliokuwapo pale Lumumba wanasema Lowassa hakutaka kumjibu kuwa amekubali bali alitumia mbinu ya kidiplomasia kumuambia Magufuli kuwa anaoamba apewe muda kidogo wa tafakari ikiwemo kushirikisha familia, lakini haikuwa hivyo alijikuta anatoka mlangoni waandishi wa habari wamemzonga na yeye alijua ni kikao cha siri tu, alijibu maneno mawili tu, ”Nimerudi nyumbani“ , na kuanzia siku hiyo akaingia kwenye maisha ya ukimya.
Hali ilikuwa mbaya zaidi nyumbani kwake alirudi akakuta mkewe na watoto wanalia kwa kitendo cha yeye kuchukua Maamuzi Magumu sana kwa watu waliomtesa hata kiafya bila hata kuwashirikisha, akabaki na kazi ya kuanza kuwabembeleza, walikuwapo watu nyumbani kwake na wanakumbuka hiyo hali.
Maisha ya lowassa baada ya kurudishwa ccm yakawa ya upweke mkuu , wapenzi wake ambao walikuwa wakimfurahia kila walipomuona nao kama familia wakaona amewacha bila hata kauli ….Lowassa akaanza kujitenga , akawa hata akifika sehemu zenye vijana waliokuwa wakimpa Faraja ya kumtia Moyo kwa kumshangilia anafunga kiooo hataki tena wamuone …atawaambia nini ….kavuliwa nguo ….simanzi hii ikamuweka mbali na watu akaanza kuugua hadi kifo ….watu wake walibaki kumpenda walitaka tu kumsikia Aawaambie mbona aliondoka bila kuwaaaga na hakuwahi Kufungua mdomo wake hadi alipokata kauli ….kafa na MENGI moyoni .
Lowassa sasa amefariki na wale waliomsababishia maamuzi wameamua kuwachagulia wanafamilia hadi watu wa kulia nao, leo amekua mtu wa maana sana na hawataki yeyote asogelee kwenye kipaza sauti kutoa pole ambaye hawamtaki.
Msibani waliomtesa na kumdhihaki ndio wakawa wamejipa haki ya kulia machozi ya simba, huo ni usaliti mwingine. Huyu aliyelala hakuwa mtu wa kubagua, hata alipokua CCM alikuwa anakaribisha nyumbani kwake watu wa vyama vyote kula na kufurahi nao, hakuwahi kumbagua mtu yeyote.
Hata kanisani Askofu Mkuu naye amejeuka kuwa sehemu ya wabaguzi, alifikia kumtambua hadi msemaji wa CCM wa mkoa kwa jina na heshima huku asiwaone wale ambao hawatakiwi kuonekana wala kutajwa.
Lowassa hajatendewa Haki akiwa hai na sasa akiwa ni Marehemu.
Pumzika kwa amani Edward Ngoyai Lowassa, umeteseka na kusalitiwa sana. Pumzika Baba.
CCM wamekiri wenyewe kuwa walimuonea Lowassa na kuumiza roho na mwili hadi Ikafikia kumkata kwa kashfa ya kubuni ya Richmond, hadi akaamua kuhamia upinzani.
Lowassa aliamia upinzani hakuwa na madaraka lakini akawa na Faraja kubwa sana kuanzia kugombea Urais (na kushinda ambako hakutangazwa), mnakumbuka kimya kilichotawala nchi mwaka 2015 wakisubiri neno moja tu kutoka kwa Lowassa, akasema "Sitaki kuingia madarakani kwa kukanyaga dame“, mnakumbuka Magufuli hakuwa na confidence wala furaha alikuwa anajua hakushinda, hadi akaja kasisi Kutoka Nigeria TB Joshua.
Pamoja na kuwa hakushinda Lowassa alibaki na Amani na mara zote wapenzi wake walimpa Faraja kwa kumshangilia kila alipopita, huku naye akiwapungia kwa tabasamu, ndio Faraja iliyokua imebaki kwaka na mara kadhaa hata kwenye taa za barabarani akisimama vijana walikuwa wakimuona tu wanamfurahia.
Magufuli hakuwa na Amani kuona Lowassa pamoja tayari alikuwa amedhoofu anashangiliwa kila anakopita. Akaona ni lazima arudi CCM ili kuja kumuongezea nguvu, alitumia mbinu chafu ya kumkamata mdogo wake Rostam aitwaye Akram na kumpa kesi ngumu sana ambazo hazina dhamana ikiwemo kumiliki silaha za moto.
Familia ya Rostam ilichanganyikiwa ilikuwa ni kama kumteka nyara na kutaka ransom, ilibidi Rostam arudi haraka kuja kuhanghaika mdogo wake asifungwe maisha, sasa mchezo ulianzia hapo.
Magufuli alimdai price tag moja hadi nyingine na akatimiza baada ya kufanya kila kitu akamdai “Kichwa cha Lowassa“, mahojiano anayotoa Rostam kuwa yeye ndiye aliyemrudisha Lowassa CCM yana Siri kuu ambayo yeye anaongea Leo kwakuwa lowassa hayupo kusema ukweli
Lowassa alichukuliwa nyumbani kwake kirafiki na Rostam akaibukia kwa magufuli na akashangaa sana anatoka nje anakutana na waandishi wa habari wanamuuliza anajionaje kurudi CCM (watu wa karibu waliokuwapo pale Lumumba wanasema Lowassa hakutaka kumjibu kuwa amekubali bali alitumia mbinu ya kidiplomasia kumuambia Magufuli kuwa anaoamba apewe muda kidogo wa tafakari ikiwemo kushirikisha familia, lakini haikuwa hivyo alijikuta anatoka mlangoni waandishi wa habari wamemzonga na yeye alijua ni kikao cha siri tu, alijibu maneno mawili tu, ”Nimerudi nyumbani“ , na kuanzia siku hiyo akaingia kwenye maisha ya ukimya.
Hali ilikuwa mbaya zaidi nyumbani kwake alirudi akakuta mkewe na watoto wanalia kwa kitendo cha yeye kuchukua Maamuzi Magumu sana kwa watu waliomtesa hata kiafya bila hata kuwashirikisha, akabaki na kazi ya kuanza kuwabembeleza, walikuwapo watu nyumbani kwake na wanakumbuka hiyo hali.
Maisha ya lowassa baada ya kurudishwa ccm yakawa ya upweke mkuu , wapenzi wake ambao walikuwa wakimfurahia kila walipomuona nao kama familia wakaona amewacha bila hata kauli ….Lowassa akaanza kujitenga , akawa hata akifika sehemu zenye vijana waliokuwa wakimpa Faraja ya kumtia Moyo kwa kumshangilia anafunga kiooo hataki tena wamuone …atawaambia nini ….kavuliwa nguo ….simanzi hii ikamuweka mbali na watu akaanza kuugua hadi kifo ….watu wake walibaki kumpenda walitaka tu kumsikia Aawaambie mbona aliondoka bila kuwaaaga na hakuwahi Kufungua mdomo wake hadi alipokata kauli ….kafa na MENGI moyoni .
Lowassa sasa amefariki na wale waliomsababishia maamuzi wameamua kuwachagulia wanafamilia hadi watu wa kulia nao, leo amekua mtu wa maana sana na hawataki yeyote asogelee kwenye kipaza sauti kutoa pole ambaye hawamtaki.
Msibani waliomtesa na kumdhihaki ndio wakawa wamejipa haki ya kulia machozi ya simba, huo ni usaliti mwingine. Huyu aliyelala hakuwa mtu wa kubagua, hata alipokua CCM alikuwa anakaribisha nyumbani kwake watu wa vyama vyote kula na kufurahi nao, hakuwahi kumbagua mtu yeyote.
Hata kanisani Askofu Mkuu naye amejeuka kuwa sehemu ya wabaguzi, alifikia kumtambua hadi msemaji wa CCM wa mkoa kwa jina na heshima huku asiwaone wale ambao hawatakiwi kuonekana wala kutajwa.
Lowassa hajatendewa Haki akiwa hai na sasa akiwa ni Marehemu.
Pumzika kwa amani Edward Ngoyai Lowassa, umeteseka na kusalitiwa sana. Pumzika Baba.