CCM walibadilishwa na kardinali pengo - serikali 2

CCM walibadilishwa na kardinali pengo - serikali 2

Status
Not open for further replies.

fisi 2

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
3,284
Reaction score
4,652
Mimi ni mkristo mkatoliki nalijua kanisa langu kwa undani kabisa. Masimamo wa kuipinga tume ya WARIOBA ni shinikizo la KARDINALI Pengo kwa maslahi ya kanisa katoliki huko Zanzibar. Ni kweli matukio mabaya yamefanyika na serikali ya CCM kushindwa kuyashughulikia na hata kutoa majibu. Kumekuwa na juhudi ZA kuidhibiti zaidi Zanzibar. Tukumbuke JK alishawambia CCM wajiandae kisaikolojia kupokea serikali 3 na kusaini rasimu zote. Mnajiuliza maswali nini kimetokea na Watu kubadilika ghafla hata wale waliokuja pamoja mfano wajumbe wenye nguvu wa Zanzibar ? Nawapa jibu hapo. Binafsi nimewaelimisha viongozi wangu wa dini falsafa ya ukristu ya kwenda pole pole kama alivyoshauri Gamaliel kwenye kitabu cha matendo ya mitume. Kuikandamiza Zanzibar sio kuimarisha ukristu . Kama alivyolia LYatonga MRema 2005 kwa KIlaini na Mimi nalia Leo kwa Askofu wangu KARDINALI Pengo. Umeiharibu Tanzania. Amani kwanza serikali baadae.
 
Wenye macho na fikra watanzania ukweli , wewe ng'ang'ania upofu. Amani kwanza dini na serikali baadae
 
sishangai kwani nguvu ya kanisa na ushawishi wake nchini hauna mfano. napata wakati mgumu kuelewa kilichoibadilisha ccm ghafla kiasi hicho. yawezekana kabisa kanisa lahusika
 
Tukuamini tu kwa kuandika hizi sentensi? Nadhani ingekuwa vizuri kuthibitisha hili ndugu. Bila kufanya hivyo haya yatakuwa maneno yanayoweza kusemwa na yeyote. Madhara ya kutoa tuhuma nzito hivi kwa namna nyepesi ni kutaka kutugombanisha watz. Tafakari
 
Hii issue kwa wanaojua historia ya Nyerere kuitawala Tanzania baada ya kupata maelekezo kutoka Vatican(ambako alipata ile fimbo) ataielewa nini mtoa thread unamaanisha
Baada ya Nyerere kuwasaliti akina Mzee Skykes na kuendeleza strategy ya Vatican ,hadi alipokuja kum deceive Karume(ambaye alikua anahofia kupinduliwa na ZPP na ZNP baada ya yeye kumpindua Shekhe Mohamed Shamte)
 
Mimi ni mkristo mkatoliki nalijua kanisa langu kwa undani kabisa. Masimamo wa kuipinga tume ya WARIOBA ni shinikizo la KARDINALI Pengo kwa maslahi ya kanisa katoliki huko Zanzibar. Ni kweli matukio mabaya yamefanyika na serikali ya CCM kushindwa kuyashughulikia na hata kutoa majibu. Kumekuwa na juhudi ZA kuidhibiti zaidi Zanzibar. Tukumbuke JK alishawambia CCM wajiandae kisaikolojia kupokea serikali 3 na kusaini rasimu zote. Mnajiuliza maswali nini kimetokea na Watu kubadilika ghafla hata wale waliokuja pamoja mfano wajumbe wenye nguvu wa Zanzibar ? Nawapa jibu hapo. Binafsi nimewaelimisha viongozi wangu wa dini falsafa ya ukristu ya kwenda pole pole kama alivyoshauri Gamaliel kwenye kitabu cha matendo ya mitume. Kuikandamiza Zanzibar sio kuimarisha ukristu . Kama alivyolia LYatonga MRema 2005 kwa KIlaini na Mimi nalia Leo kwa Askofu wangu KARDINALI Pengo. Umeiharibu Tanzania. Amani kwanza serikali baadae.
Wewe ni mchochezi na unatumia style ya divide and rule but you wont make it
 
Kuna watu mnaicheza amani ya wananchi kwa njia zozote kwa sababu ya kutaka kutimiza malengo yenu maovu.

Mnadhani kuwagawa Watanzania ndiyo kutawafanya mpewe kura au ikishindikana basi mtawale kwa ncha ya upanga.

Haitatokea kwa sababu watanzania wanazipuuza hizi agenda zenu.
 
Ipo siku wewe utakuja kutembea uchi barabarani kama ulishaanza hivi!
 
Mkatoliki wa wapi wewe acha bange' unaikana dini yako unajibandika ukatoliki ili uchafue hali ya hewa na udini wako!
 
Wakatolic ni ma empire makubwa. Mambo ya ujasus wanayajua sana. Hiyo ndo sera yao. Mm ni mkristu nawajua sana. Hilo linalosemwa lipo ndo mana wenzetu waisilamu kila ckuhulia na mfumo kristo. Na hii itakuwa ivo daima. Mfumo kristo ndo upodunian nw so ni kweli lisemwalo.
 
Walianza akina Nape tangu kwenye mabaraza kutetea Serikali mbili, akina Mwigulu na makada wengine ndani ya CCM wamediriki kusema wazi kuwa wanaotetea Serikali tatu wajiandae kuihama nchi na kuwa wananchi watakaotetea Serikali tatu wajiandae kulipa kodi ya kichwa; hata Mkuu wa Nchi Mhe. Kikwete alitamka wazi kuwa Serikali tatu itakuja labda baada ya yeye kuondoka madarakani;

Iweje leo baada makada wa CCM kujikanyaga wenyewe kwa kauli zao watu wanataka kuhamisha mjadala mzima na lawama kwa WAKRISTU na kwa MUADHAMA KARDINALI PENGO. Ina maana wao CCM na watawala kwa ujumla hawana wanachosimamia ila ni kusubiri kuangalia watu fulani wanataka nini ili waweze kudandia?. Kama ni suala la Ukristu; KIKWETE, SHEIN, BILALI, SHIVJI na wawakilishi wote wa CCM kutoka Zanzibar ni Wakristu?

Tufike mahali tutumie akili zetu tulizopewa na maulana kwa busara hata kama ni finyu na sio kila mara tuwe tunatafuta sababu na visingizio kwa minajili ya kuficha udhaifu na ujinga uliotujaa vichwani mwetu.
 
Mkatoliki wa wapi wewe acha bange' unaikana dini yako unajibandika ukatoliki ili uchafue hali ya hewa na udini wako!

Pengo nae aachane na mambo ya siasa bhana yeye ni chanzo.kama ameshindwa kuchunga mapadre wake aende zake huko kwao.mimi nimkatoliki pure.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom