CCM wafanyia mkutano kituo cha polisi

CCM wafanyia mkutano kituo cha polisi

MADORO

Senior Member
Joined
Nov 12, 2011
Posts
198
Reaction score
117
Kile ambacho tunalalamika kila siku na kutoa ushahidi lakini serikali inapuuza.

Chama cha Mapinduzi wakiongozwa na Mbunge wa jimbo la Segerea na Naibu waziri Makongoro Mahanga wamefanyia mkutano kwenye mlango wa kituo cha Polisi kana kwamba hakuna viwanja vingine.

Polisi wakashindwa kufanya kazi zao magamba yamejaa mlangoni.

Hivi CHADEMA wangefanya vile mlangoni mwa polisi ingekuwaje? hebu wadau angalieni Picha mseme wenyewe
 

Attachments

  • MKUTANO POLISI KITUONI.jpg
    MKUTANO POLISI KITUONI.jpg
    326 KB · Views: 9,478
kwa wewe huwezi fanya mkutano kwenye shamba la ukoo??!!!??!!??!!??!!??!!
 
Watakuambia Polisi ni chombo cha Serikali; na Serikali inaongozwa na CCM! Usishangae, pengine kaka yetu Mahanga alienda hapo kuhakikisha agizo la Pinda la "Wapigwe tu" linatekelezwa barabara!!
 
Hii ni kweli mkuu?..

Hapa ndio pale 'upendeleo' unapoonekana, then vyama vingine kujaribu kufanya sawa na wao/zaidi ya wao (lakini wao kuonekana wabaya!

Inabidi ifike sehemu tuwe makini wenye kupenda Nchi zaidi ya chama. This is going to the extreme.
 
Magamba walikuwa na hofu kwamba wakifanyia eneo lingine watazomewa!
 
Hii ni kweli mkuu?..

Hapa ndio pale 'upendeleo' unapoonekana, then vyama vingine kujaribu kufanya sawa na wao/zaidi ya wao (lakini wao kuonekana wabaya!

Inabidi ifike sehemu tuwe makini wenye jupenda Nchi zaidi ya chama. This is going to the extreme.

'mnakimbiliaga wapi jupenda maana yake nini sasa...'
 
Kwenye cheti cha kuhitimu mafunzo yanayoendeshwa na JESHI LA CCM a.k.a GREEN GUARD kuna kipengele kinataja Mahusiano na Vyombo vya Dola, binafsi naona hayo ndiyo mahusiano yenyewe.
 
Huyu ndie aliyekimbia na masanduku ya kura na Polisi wakawa wanamwangalia tu. Na Leo anafanyia mkutano kituoni wanamwangalia tu, kesho hatujui atafanya nini
 
Kazi ipo kama hali ndio hivyo, Mikel Aweda hupo?
 
'mnakimbiliaga wapi jupenda maana yake nini sasa...'

Ukitaka kukosoa uwe msafi!

Of all the things, that is the best you can do!!...It was an error(typing error) unless someone persist in it to be a mistake.

Nilimaanisha Kupenda nchi na Si 'jupenda' nchi! Na kiswahili sanifu ni huwa 'mnakimbilia' wapi na si "MNAKIMBILIAGA" wapi.

Now, Back to the topic!
 
Lengo la kufanyia hapo ni nini mbona sielew au walienda kushitaki
 
Kile ambacho tunalalamika kila siku na kutoa ushahidi lakini serikali inapuuza.

Chama cha Mapinduzi wakiongozwa na Mbunge wa jimbo la Segerea na Naibu waziri Makongoro Mahanga wamefanyia mkutano kwenye mlango wa kituo cha Polisi kana kwamba hakuna viwanja vingine.

Polisi wakashindwa kufanya kazi zao magamba yamejaa mlangoni.

Hivi Chadema wangefanya vile mlangoni mwa polisi ingekuwaje? hebu wadau angalieni Picha mseme wenyewe

Nahisi kama haukuwa mkutano wa Polisi shirikishi; itakuwa mkutano wa WATUHUMIWA...
 
Mahanga kufanyia mkutano kituo cha Polisi si ajabu kwa mtu yeyote anayeishi maeneo hayo ya Tabata Shule kwani watu wengi wa maeneo hayo hawamtaki na zaidi ya 85% wazee kwa vijana hawakumpigia kura kwa hiyo kufanya hivyo ilikuwa ni njia mojawapo ya kujihami kwani uwezekano wa kuzomewa au kufanyiwa vurugu lazima ungejitokeza.
 
Back
Top Bottom