CCM Vs CHADEMA

CCM Vs CHADEMA

ili cdm iweze kuyafikia malengo yake ya kisiasa imapaswa kutafakari yafuatayo.
1.propaganda ya ukabila na ukaskazini inayoenea kwa kasi kubwa.
2.kashfa zinazo wakabili mbowe na slaa kwa ufujaji wa pesa za chama.
3.propaganda ya udini ambayo imekua ikikihusisha chama na kanisa katoliki.
USHAURI
Kwanza ni kuunda upya safu ya uongozi .ktk hili mwkt wa chama taifa anapaswa kua safari au saidi arfi.katibu mkuu awe kati ya mkumbo au mnyika. mbowe.slaa na zitto waendelee kua viongozi ktk kurugenzi za chama.hii itakua imezifuta propaganda zinazoenezwa kwa kasi nchini.pia itaondoa mgongano wa maslahi kati y zitto na slaa na hivyo wote kuunganisha nguvu kukijenga chama.na ccm itaku haima chake2015.
TANBIHI.wapo wanaojifanya radicals cdm na kutukana kila mawazo yenye nia njema kwa chama.tuwaangalie vizuri.huenda ni mashabiki wanaojazana mikutanoni halafu mwisho wa siku hawapigi kura halafu wanakaa vijiweni eti wamesubiri ushindi washangilie.
....... NAWASILISHA.....
 
MWOBHO

Join Date: 1st January 2013

Nina hofu nawe sana!

Hautumiki kweli????

Ngoja wadau waje!
 
Last edited by a moderator:
Hapa mnaongea kinyume au? manake maneno ya ccm imechokwa siyo ya leo ni tangu 1995, nadhani sasa CDM mnaona kama kwishne mnaanza kutapatapa, CDM mna jipya gani mpaka sasa?

Hivi mshikaji umeshaicheki ile movie ya Lincoln? I think you sound like one of those blood suckerz!!

Hauwaonei huruma hata watoto wako!!
 
mtajisafisha sana lakini haitabadilisha ukweli kuwa nyie ni waovu.

Salaam wana JF

Angalizo dogo kwa wana mageuzi.

CCM wanaihujumu CHADEMA kwenye level ya juu zaidi kuliko CHADEMA wanavyofikiria. Inaonekana intelijensia ya CHADEMA inai- underestimate intelijensia ya CCM, kitu ambacho si sahihi, na kinaweza kuigharimu CHADEMA.
Inavyoonekana CCM ina watu ndani ya CHADEMA, na ni watu ambao wanaaminika sana ndani ya CHADEMA, na hao watu wamefanikiwa ku pretend na kuonekana ni very loyal kwa uongozi wa juu wa CHADEMA. Na hawa watu pia huwazushia kashfa wenzao/watendaji ndani ya chama na kuwachongea kwa wakuu wa chama, ili wafukuzwe au wawe demoted. Na wanafanya haya yote na mengine mengi tusioyajua kukivuruga chama, huku wakuu wa chama wakidhani kwamba watu hao wana nia ya kukijenga chama. Na hawa watu kwa namna moja au nyingine watahusika siku za baadae kwenye uvujaji wa mipango ya ndani ya chama, na hii inaweza kuwapa CCM urahisi wa kujua ni jinsi gani ya kui-slow down CHADEMA.

Kitendo cha ile clip ya afisa usalama wa juu kabisa wa CHADEMA kuwafikia CCM, regardless imelishwa maneno au la, kimeonyesha udhaifu mkubwa uliopo ndani ya usalama wa chadema. Na bado hatujui pengine kuna vingine vinakuja.


Inachukua hata mwaka kumshawishi mtu kujiunga na chama, lakini inachukua sekunde moja tu kumpoteza mwanachama.

Ushauri wangu kwa uongozi wa juu, na kwa wanachama, na kwa wafuasi wa chadema ni kuwa makini sana na mbinu chafu za wapinga mageuzi, hawa watu kila siku wanatafuta mbinu mpya.

Tusiwape mwanya wakatupelekesha mchakamchaka mpaka tukaomba dakika ya 90(2015) ifike haraka kwa sababu tumechoka, ila tuwapeleke wao mchakamchaka na tufike dakika ya tisini bado tuko fit na wao wawe taabani.
 
Teh teh teh, CDM msitafute mchawi mnajihujumu wenyewe, mbona mnamkana kijana wenu Ludovick hadharani? Una taarifa kuwa LWAKATARE kakiri kuhusika na njma za kutaka kUmdhuru MSACKY? CCM inahusika vipi hapo? mtajikuna sana lakini mwishowe mtaumbuka.
Kumbe kakiri!Kakiri wapi mkuu maana sijaona sehemu yoyote ile akikiri kuhusika?
 
Back
Top Bottom