Niseme CCM ni chama nambari wani duniani kwa kufuga watu waovu na wasiofaa katika ujenzi wa taifa letu Tanzania
CCM wamepoteza dira kabisa na hawana hoja za kujitetea pale mbunge/mwanachama wao anapojiondoa na kusema madhaifu yote ya chama
CCM imekua na utaratibu wa kuibua kashfa za ufisadi,wizi wa Mali za umma na matumizi mabaya ya madaraka kwa mbunge/mwanachama wake anayekipa kisogo chama hicho
Lowassa alipohama CCM na kujiunga na upinzani wakamshambulia kwa vijembe na maneno ya kwenye khanga,eti chama hakiwezi kumpitisha fisadi kuongoza nchi,cha ajabu mwenyewe kawaambia hao CCM kama MNA ushahidi nipelekeni mahakamani ,hawajafanya hivyo hadi Leo
Juzi juzi kaondoka Lazaro Nyalandu ambaye alikua mbunge na mwanachama hai wa CCM wameanza kutoa povu Mara jamaa kaondoka kisa kanyimwa uwaziri,mara arudishe twiga wetu yani mambo mengi nonsense ambayo Nyalandu hakuyafanya kwa matakwa yake bali maagizo ya viongozi wake ndani ya chama juu ya hao twiga na dhuluma nyingine
CCM kumejaa wajinga ndo mana hata kujibu hoja za Nyalandu wameshindwa ,walichobaki ni kuongea porojo na maneno ya kwenye khanga na kushindwa kabisa kujitetea dhidi ya hoja madhubuti za Nyalandu
CCM kuna wala rushwa wengi na hakuna mwenye nia ya kuondoa rushwa kwa sababu viongozi wenyewe wakuu ni wala rushwa,mafisadi na wabadhirifu wa Mali za umma
Kwa mtindo huu wa CCM kumshambulia mtu anayehama chama kwa kutaja madhambi yake basi inaonesha ndani ya CCM hakuna msafi kuanzia Mwenyekiti wao hadi wana chama wengine.
Kitendo cha kukaa kimya wakati mwanachama yupo ndani ya chama na kushindwa kutaja maovu yake akiwa ndani ya chama na kuyataja pale tu anapokihama chama hicho basi hii ni kiashiria CCM wote ni wezi,mafisadi,wala rushwa
Shida zote za nchi hii chanzo ni CCM ,walisaini mikataba ya kilaghai na wazungu kuhusu madini CCM ikishirikiana na wazungu wameibaaaa weee madini yetu saa hivi yamebaki mashimo linatokea jitu moja nafiki la CCM na kujifanya kusema tumeibiwa sana wakati ye mwenyewe alikuwepo wakati wanasainishana hiyo mikataba mibovu,halafu saa hivi wanataka kujifanya hawajui na kutuona watanzania ni wajinga
CCM kumejaa wajinga wao kila kitu ndio hata kama kina madhara kwao na kwa kizazi chao mfano upitishaji wa sheria mbovu zisizo na tija huu ni ujinga wa wanaCCM
Tusitegemee mabadiliko na maendeleo ya nchi chini ya CCM na Magufuli ni ndoto CCM ni ile ile Magufuli hawezi kuondoa rushwa wala mafisadi kwa sababu chama chake ndo wamejaa watu hao hao,ni WAJINGA pekee wenye imani na CCM na Magufuli wao
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.