Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,735
Nape Nauye alituhakikishia kuwa Lowasa, Chenge na Rostam watangoka ndani ya siku 60
Mangula akatuambia watawangoa wote walioingia madarakani kwa rushwa hata kama ni kikwete lakini si siku 90 wala 60 wote kimya...maana ukweli ni kwamba ndani ya ccm hakuna aliye msafi wote ukoo wa panya ni kimbilio la mafisadi mfano kwenye sakata la Escrow Kikwete anahusika 100%, pesa za EPA ndizo zilizo mwingiza kikwete madarakani..
Mangula akatuambia watawangoa wote walioingia madarakani kwa rushwa hata kama ni kikwete lakini si siku 90 wala 60 wote kimya...maana ukweli ni kwamba ndani ya ccm hakuna aliye msafi wote ukoo wa panya ni kimbilio la mafisadi mfano kwenye sakata la Escrow Kikwete anahusika 100%, pesa za EPA ndizo zilizo mwingiza kikwete madarakani..
Kwa hakika sasa si siri tena siku za gamba kubwa CCM Edward Ngoyaye Lowassa a.k.a Fisadi wa Richmonduli ndani ya CCM zinahesabika.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba kifikia tar 12/02/2013 Kamati Kuu ya CCM itakuwa imeundwa na baada ya kupata pigo kubwa kwa Makamu Mwenyekiti Mzee Mangula, Katibu Mkuu Kinana na Kurudishwa kwa adui yake mkubwa Nape basi pigo la mwisho kwa EL ni uundwaji wa CC ambao kwa vyanzo vya jikoni kabisa..hakuna mtu wake hata mmoja.
Ikumbukwe vikao vitatu vya mwanzo vya uchujaji majina ya urais ni Sekretarieti chini ya Kinana na Nape, Kamati ndogo ya Maadili chini ya Mangula na Kamati Kuu chini ya JK...na kote huku hakuna kupiga kura ni mjadala tu then maamuzi..
Haya niyasemayo yalimkuta Lowassa mwaka 1995 aliondolewa kwenye kinyang'anyiro bila kura, yalimkuta pia Malecela aliondolewa bila kufilishwa kwenye kura...historia itajirudia 2015.
Mkuu Honey K,
1. Mbona Kinana naye ana tuhuma fulani hivi zinachukuliwaje na CCM!
2. Mbona JK amekalia tuhuma mbalimbali, yaani
a) Deep Green Finance,
b) Mwananchi Gold,
c) Meremeta,
d) Rada
e) EPA - hapa CCM imeshindwa kujibu alipo "Marehemu" Daudi Balali
f) Richmond, nk, na alipitishwa kugombea uchaguzi mkuu 2010 na sasa hivi ameendelea kulea rushwa ambayo imeendelea kuitafuna CCM hadi kwenye mifupa?
3. Wewe unafiliri CCM ilivyo kwa sasa ina "moral authority" ya kupambana na rushwa? Maana ikifika kwenye kura za maoni tunashuhudia jinsi CCM inavyotembeza rushwa kwa wapiga kura na viongozi WENGI kama si wote wa CCM wametokana na rushwa!
Haya ndiyo maelezo mapya ya Nape kuhusu ahadi yake kwetu ya kuwavua gamba mafisadi 3 vigogo ndani ya CCM ifikapo July 10;Nape alitamka maneno haya" hopeless" jana wakati anazungumza na wahariri wa magazeti ya Mwananchi Communication LTD.
Kuhusu watuhumiwa wa ufisadi na siku 90 walizopewa kujiondoa kwenye nyadhifa wanazoshikilia ndani ya chama, Nape alisema kuwa hakuna suala la siku 90 bali ni vikao vya chama vitakutana na kutoa maamuzi.
"Siku 90 zinazozungumzwa ni tafsiri ya watu pale mwenyekiti wa chama (Jakaya Kikwete) aliposema tutakutana baada ya miezi mitatu na watu wakatafsiri hivyo, lakini vikao vya NEC ndivyo vinatoa maamuzi,"alisema Nape.
Alisema kuwa hadi hivi sasa hajui makamu mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa alichozungumza na watuhumiwa hao wa ufisadi baada ya kukutana nao.​
"Sikuwepo kwenye kikao hivyo hadi sasa sijui walizungumza nini, na siwezi kwenda kumtaka Katibu Mkuu anieleze kilichozungumzwa kwani katika vikao vijavyo tutapata taarifa,"alisema Nape.
Source:Gazeti la Mwananchi June 29,2011
SI swala la kudai wala vikao kuamua upya bali vikao VILISHAFANYA UAMUZI NA UAMUZI NI WAJIPIME NA KUONDOKA WENYEWE WASIPOFANYA WATAFUKUZWA NA CHAMA.
SWALA LA LINI NI PERIOD KUTOKA KIKAO KILICHOPITA CHA NEC MPAKA KIKAO KIJACHO CHA NEC, AMBACHO KWA MUJIBU WA KATIBA HUWA KINAKUTANA KILA BAADA YA MIEZI MINNE. Lakini SI LAZIMA IWE MIEZI MINNE KAMILI,KATIBA YA CCM INARUHUSU KUWA NA VIKAO MAALUMU KATIKATI KABLA YA MUDA HUO,HIVYO NEC INAWEZA KUKUTANA KABLA YA MIEZI HIYO KATIKATI KAMA ITAONEKANA IPO HAJA. NA INWEZA IKAKUTANA BAADA YA MIEZI MINNE KUTOKANA NA MAZINGIRA,KWA MFANO NAFASI YA MKITI KAMA IMEBANA TUNAWEZA KUSOGEZA MBELE SO SI SWALA LA SIKU EXACTLY.
ANGALIA HATA BUNGE KUNA MUDA UMEPANGWA LAKINI LINAWEZASOGEZA SIKU ZA KUANZA AU KUMALIZA KUTEGEMEANA NA HAJA YA KUFANYA HIVYO.
Kikubwa hapa NI KUWA WAHUSIKA WAMEITWA NA KUJULISHWA UAMUZI WA NEC NA KUWA UPO MUDA WA WAO KUTEKELEZA WASIPOFANYA KIKAO KIJACHO CHA NEC NI KUWASILISHA RIPOTI YA UTEKELEZAJI WA MAAMUZI ITAKAYO ONYESHA IMETEKELEZWA KWA KIASI GANI NA KUTEKELEZA SEHEMU YA PILI YA UAMUZI.
KUMBUKA ILISEMWA HAPA JF KUWA UAMUZI HUU HAUTATEKELEZWA NA KUWA HAYO YALIKUWA MANENO (yalitumika maneno makali, machafu) YA NAPE NA CHILIGATI SI UAMUZI WA CHAMA, AKATOKA DR. KIKWETE MWENYEKITI WA CHAMA AKASEMA PALE DIAMOND ALIPOONGEA NA MAASKOFU KUWA ANACHOSEMA NAPE NI UAMUZI HALALI WA CHAMA, WATU WAKAFUMBA MACHO NA MASIKIO NA KUENDELEA KUDAI NI YA NAPE NA KUWA WATUHUMIWA HAWATACHUKULIWA HATUA ZOZOTE HATA KUJULISHWA TU. WAMEITWA NA KUPEWAA UAMUZI WA NEC, WATU WAKAKIMBIA JF, HATA WALE WALIONITUKANA NILIDHANI WATARUDI KUPONGEZA HATUA ILIYOFIKIWA, SIKUWAONA.
NINACHOWEZA KUHAKIKISHIA HAPA UAMUZI HUU WA KUWAWAJIBISHA BAADHI YA WATUHUMIWA HAUTABADILISHWA KWA KELELE ZA BARABARANI NA SARAKASI ZA WATUHUMIWA, TUMETHUBUTU KUAMUA, TUTATEKELEZA MAAMUZI.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
Safi, hii ndo tungependa mara nyingi ufanye hapa JF, always firm kwny unachoamini, tatizo 'vijana wako' hapa JF (you know what I mean) kama usingewahi kuyaandika haya mwenyewe wangei-spin hii habari na kusababisha watu kuhama hata hoja.
Kidumu?