Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
CCM taabani kifedha
Friday, 31 December 2010 20:56
Katibu wa chama cha mapinduzi,Yusuph Makamba
Hussein Issa na Habel Chidawali, Dodoma
MAMBO si shwari ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana taarifa kwamba kiko taabani kifedha, kiasi cha kulazimika kusitisha kutoa ruzuku kwa baadhi ya watendaji wake kwenye ngazi za mkoa, wilaya na kata.
Usitishwaji wa ruzuku unadaiwa kuzikumba pia taasisi zilizopo chini ya chama hicho vikiwemo vyombo vyake vya habari ambavyo ni Uhuru Publications Ltd, wanaozalisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani pamoja na Radio Uhuru.
Habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa hali hiyo inatokana na chama hicho kupunguziwa ruzuku kufuatia kupata idadi ndogo ya wabunge wa kuchaguliwa katika Uchaguzi Mkuu uliomalizika Oktoba 31 mwaka huu ikilinganishwa na idadi ya wabunge hao katika miaka mitano iliyopita.
Kwa mujibu wa habari hizo, kabla ya Uchaguzi Mkuu CCM ilikuwa inapokea ruzuku ya Sh1.2 bilioni kwa mwezi, lakini baada wabunge wake kupungua kwenye uchaguzi wa Oktoba 31, mwaka jana, sasa chama hicho kinapokea ruzuku ya Sh 800 milioni.
Mmoja wa makatibu wa CCM wa wilaya mojawapo mkoani Dodoma aliliambia Mwananchi kuwa: "Hali sasa ni mbaya na kimsingi mambo mengi yamekwama kufanyika kwa wakati".
Habari za uhakika kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa CCM kimekata ruzuku hiyo kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kupungua kwa fedha kulikotokana na idadi ndogo ya kura za wabunge kufutia kufanya vibaya katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31 jana.
Idadi ya wabunge wa CCM katika Bunge la sasa imepungua kwa zaidi ya asilimia kumi ililinganishwa na idadi kiliyokuwa nayo katika Bunge lililipota.
Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa chama hicho kina wabunge 258 katika Bunge la Kumi sawa na asilimia 75.3 ya wabunge 343 waliopo, wakati katika Bunge lililopita kilikuwa na wabunge 271 ambao ni sawa na asilimia 85.7 ya wabunge 316 wa Bunge hilo la tisa lililomaliza muda wake mwishoni mwa mwaka jana.
Wakati CCM kikipoteza asilimia zaidi ya kumi ya nafasi za uwakilishi bugeni, vyama vya upinzani vilifanikiwa kuongeza idadi ya wawakilishi wake ambapo hivi sasa vina wabunge 84 sawa na asilimia 24.7 ikilinganishwa na Bunge lililopita ambalo lilikuwa na wabunge wa upinzani 45 sawa na asilimia 14.3.
Kutokana na hali hiyo ni dhahiri kwamba kiasi cha ruzuku kinachotolewa na Serikali kwa CCM kimepungua kutokana na wabunge wake kupungua huku kiasi kinachokwenda kwa vyama vya upinzani kikiongezeka.
Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, alisema kuwa kupuguzwa kwa ruzuku hakuwarudishi nyuma kwa sababu chama chao ni kikongwe hivyo hakiwezi kutetereka kama vyama vingine.
Makamba kuwa chama hicho hakiishi kwa ruzuku hivyo kitaendelea kama kawaida kwani kimeanza tangu mwaka 1954, kinajua nini maana ya kuongoza na hakibahatishi.
"Wewe kijana nani kakuambia CCM kinaishi kwa kutegemea ruzuku, hiki ni kikongwe yaani chama kianze tangu mwaka 1954 leo hii uniambie suala la ruzuku, wewe vipi bwana?"alisema Makamba huku akicheka
Aliongeza kuwa kuna watu walifikiri chama kinakufa, lakini wamekosea kufikiri hivyo na kwamba CCM hakiwezi kufa na kitaendelea kukua hata pasipo ruzuku.
Hata hivyo, uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa viongozi wa ngazi za mikoa, wilaya, kata na matawi wa CCM, walikuwa wakipata fedha hizo kwa ajili ya kukiimarisha chama kwenye ngazi hizo, lakini sasa hawapewi tena.
CCM ilikuwa ikitoa ruzuku ya Sh 5000 kila mwezi katika ngazi za matawi, Sh10,000 ngazi ya kata na Sh50,000 ngazi ya wilaya.
Wajumbe wengine katika wilaya ambao walikuwa wakipewa posho hizo ni na Katibu wa Itikadi na Uenezi na Katibu wa Uchumi na Fedha ambao walikuwa wakipewa Sh20,000.
Kwa nafasi ya mkoa, Mwenyekiti alikuwa akipewa posho ya Sh75,000 na Katibu Mwenezi wa Mkoa na Katibu wa Uchumi na Fedha walikuwa wakilipwa Sh50,000.
Chanzo hicho cha habari kimeeleza kuwa kutokana na kukatwa ruzuku hiyo, watendaji hao sasa wanatakiwa kuanza kujitegemea.
Yaani sisi tunashangaa kwa kuwa mbali na fedha wanazokatwa wabunge wetu katika mishahara yao, lakini bado kuna ruzuku ya zaidi ya Sh800 milioni ambazo tunalipwa kutoka serikalini, lakini, wanabaki nazo wao hii inatuumiza sana, alisema kiongozi mmoja wa CCM mkoani Dodoma.
Alisema kuwa wabunge wamekuwa wakikatwa fedha nyingi ambazo badala ya kubaki katika wilaya na majimbo wanakotoka fedha hizo zimekuwa zikipelekwa moja kwa moja makao makuu ya chama jambo ambalo wengi wamekuwa wakihoji.
Kitu kingine ambacho kiongozi huyo amekilalamikia ni kitendo cha CCM kuwakata katika mishahara yao madiwani wote wa CCM, lakini pia fedha hizo zinapelekwa makao makuu ya chama.
Katika kipindi cha mchakato wa Uchaguzi Mkuu CCM ilitoa posho kwa viongozi wote wa chama hicho kuanzia ngazi ya tawi hadi taifa ambapo viongozi wa matawi, Mwenyekiti, Katibu, Katibu wa Uchumi na Katibu Mwenezi walikuwa wakilipwa Sh 5000 kila mmoja.
Kwa upande wa kata, viongozi wa nafasi hizo walilipwa sh 10,000 kila mmoja na kwa upande wa wilaya kila mmoja alilipwa zaidi ya 100,000 kiwango ambacho kilipanda kwa ngazi ya mkoa pia.
Haikufahamika mara moja mbunge mmoja wa CCM anakatwa kiasi gani, lakini kwa upande wa madiwani kila mmoja anakiachangia chama hicho Sh 10,000 kila mwezi katika posho yake jambo linalofanya CCM kuvuna fedha nyingi kwa madiwani pekee.
Katika utaratibu wa Chama hicho hivi sasa viongozi hao watategemea kupata posho kutokana na makusanyo ya ada za wanachama ambazo watakuwa wakilipia kadi zao.
Kila mwanachama wa CCM analipia kadi yake Sh1200 kwa mwaka ambapo makato yake ni pamoja na asilimia 50 kubaki kwenye tawi, asilimia 30 hupelekwa kwenye kata, asilimia 15 hupelekwa wilayani na zinazobaki hupelekwa makao makuu.
Awali Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Kapteni George Mkuchika alisema pamoja na kulifahamu suala hilo hawezi kuzungumzia kwa sasa kwa sababu hataki kuhojiwa na waandishi wa Mwananchi.
"Halo samahani sana nyie si mmesema mnatoka gazeti la Mwananchi, sitaki kabisa kulizungumzia suala hilo pamoja na kulifahamu kwaheri, "alisema Mkuchika na kukata simu.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa alisema kuwa halifahamu suala hilo kabisa na wala hajasikia tetesi kama kuna kitu kama hicho kutoka ndani na nje ya chama.
Friday, 31 December 2010 20:56
Hussein Issa na Habel Chidawali, Dodoma
MAMBO si shwari ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana taarifa kwamba kiko taabani kifedha, kiasi cha kulazimika kusitisha kutoa ruzuku kwa baadhi ya watendaji wake kwenye ngazi za mkoa, wilaya na kata.
Usitishwaji wa ruzuku unadaiwa kuzikumba pia taasisi zilizopo chini ya chama hicho vikiwemo vyombo vyake vya habari ambavyo ni Uhuru Publications Ltd, wanaozalisha magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani pamoja na Radio Uhuru.
Habari zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa hali hiyo inatokana na chama hicho kupunguziwa ruzuku kufuatia kupata idadi ndogo ya wabunge wa kuchaguliwa katika Uchaguzi Mkuu uliomalizika Oktoba 31 mwaka huu ikilinganishwa na idadi ya wabunge hao katika miaka mitano iliyopita.
Kwa mujibu wa habari hizo, kabla ya Uchaguzi Mkuu CCM ilikuwa inapokea ruzuku ya Sh1.2 bilioni kwa mwezi, lakini baada wabunge wake kupungua kwenye uchaguzi wa Oktoba 31, mwaka jana, sasa chama hicho kinapokea ruzuku ya Sh 800 milioni.
Mmoja wa makatibu wa CCM wa wilaya mojawapo mkoani Dodoma aliliambia Mwananchi kuwa: "Hali sasa ni mbaya na kimsingi mambo mengi yamekwama kufanyika kwa wakati".
Habari za uhakika kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa CCM kimekata ruzuku hiyo kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kupungua kwa fedha kulikotokana na idadi ndogo ya kura za wabunge kufutia kufanya vibaya katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31 jana.
Idadi ya wabunge wa CCM katika Bunge la sasa imepungua kwa zaidi ya asilimia kumi ililinganishwa na idadi kiliyokuwa nayo katika Bunge lililipota.
Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa chama hicho kina wabunge 258 katika Bunge la Kumi sawa na asilimia 75.3 ya wabunge 343 waliopo, wakati katika Bunge lililopita kilikuwa na wabunge 271 ambao ni sawa na asilimia 85.7 ya wabunge 316 wa Bunge hilo la tisa lililomaliza muda wake mwishoni mwa mwaka jana.
Wakati CCM kikipoteza asilimia zaidi ya kumi ya nafasi za uwakilishi bugeni, vyama vya upinzani vilifanikiwa kuongeza idadi ya wawakilishi wake ambapo hivi sasa vina wabunge 84 sawa na asilimia 24.7 ikilinganishwa na Bunge lililopita ambalo lilikuwa na wabunge wa upinzani 45 sawa na asilimia 14.3.
Kutokana na hali hiyo ni dhahiri kwamba kiasi cha ruzuku kinachotolewa na Serikali kwa CCM kimepungua kutokana na wabunge wake kupungua huku kiasi kinachokwenda kwa vyama vya upinzani kikiongezeka.
Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, alisema kuwa kupuguzwa kwa ruzuku hakuwarudishi nyuma kwa sababu chama chao ni kikongwe hivyo hakiwezi kutetereka kama vyama vingine.
Makamba kuwa chama hicho hakiishi kwa ruzuku hivyo kitaendelea kama kawaida kwani kimeanza tangu mwaka 1954, kinajua nini maana ya kuongoza na hakibahatishi.
"Wewe kijana nani kakuambia CCM kinaishi kwa kutegemea ruzuku, hiki ni kikongwe yaani chama kianze tangu mwaka 1954 leo hii uniambie suala la ruzuku, wewe vipi bwana?"alisema Makamba huku akicheka
Aliongeza kuwa kuna watu walifikiri chama kinakufa, lakini wamekosea kufikiri hivyo na kwamba CCM hakiwezi kufa na kitaendelea kukua hata pasipo ruzuku.
Hata hivyo, uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa viongozi wa ngazi za mikoa, wilaya, kata na matawi wa CCM, walikuwa wakipata fedha hizo kwa ajili ya kukiimarisha chama kwenye ngazi hizo, lakini sasa hawapewi tena.
CCM ilikuwa ikitoa ruzuku ya Sh 5000 kila mwezi katika ngazi za matawi, Sh10,000 ngazi ya kata na Sh50,000 ngazi ya wilaya.
Wajumbe wengine katika wilaya ambao walikuwa wakipewa posho hizo ni na Katibu wa Itikadi na Uenezi na Katibu wa Uchumi na Fedha ambao walikuwa wakipewa Sh20,000.
Kwa nafasi ya mkoa, Mwenyekiti alikuwa akipewa posho ya Sh75,000 na Katibu Mwenezi wa Mkoa na Katibu wa Uchumi na Fedha walikuwa wakilipwa Sh50,000.
Chanzo hicho cha habari kimeeleza kuwa kutokana na kukatwa ruzuku hiyo, watendaji hao sasa wanatakiwa kuanza kujitegemea.
Yaani sisi tunashangaa kwa kuwa mbali na fedha wanazokatwa wabunge wetu katika mishahara yao, lakini bado kuna ruzuku ya zaidi ya Sh800 milioni ambazo tunalipwa kutoka serikalini, lakini, wanabaki nazo wao hii inatuumiza sana, alisema kiongozi mmoja wa CCM mkoani Dodoma.
Alisema kuwa wabunge wamekuwa wakikatwa fedha nyingi ambazo badala ya kubaki katika wilaya na majimbo wanakotoka fedha hizo zimekuwa zikipelekwa moja kwa moja makao makuu ya chama jambo ambalo wengi wamekuwa wakihoji.
Kitu kingine ambacho kiongozi huyo amekilalamikia ni kitendo cha CCM kuwakata katika mishahara yao madiwani wote wa CCM, lakini pia fedha hizo zinapelekwa makao makuu ya chama.
Katika kipindi cha mchakato wa Uchaguzi Mkuu CCM ilitoa posho kwa viongozi wote wa chama hicho kuanzia ngazi ya tawi hadi taifa ambapo viongozi wa matawi, Mwenyekiti, Katibu, Katibu wa Uchumi na Katibu Mwenezi walikuwa wakilipwa Sh 5000 kila mmoja.
Kwa upande wa kata, viongozi wa nafasi hizo walilipwa sh 10,000 kila mmoja na kwa upande wa wilaya kila mmoja alilipwa zaidi ya 100,000 kiwango ambacho kilipanda kwa ngazi ya mkoa pia.
Haikufahamika mara moja mbunge mmoja wa CCM anakatwa kiasi gani, lakini kwa upande wa madiwani kila mmoja anakiachangia chama hicho Sh 10,000 kila mwezi katika posho yake jambo linalofanya CCM kuvuna fedha nyingi kwa madiwani pekee.
Katika utaratibu wa Chama hicho hivi sasa viongozi hao watategemea kupata posho kutokana na makusanyo ya ada za wanachama ambazo watakuwa wakilipia kadi zao.
Kila mwanachama wa CCM analipia kadi yake Sh1200 kwa mwaka ambapo makato yake ni pamoja na asilimia 50 kubaki kwenye tawi, asilimia 30 hupelekwa kwenye kata, asilimia 15 hupelekwa wilayani na zinazobaki hupelekwa makao makuu.
Awali Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Kapteni George Mkuchika alisema pamoja na kulifahamu suala hilo hawezi kuzungumzia kwa sasa kwa sababu hataki kuhojiwa na waandishi wa Mwananchi.
"Halo samahani sana nyie si mmesema mnatoka gazeti la Mwananchi, sitaki kabisa kulizungumzia suala hilo pamoja na kulifahamu kwaheri, "alisema Mkuchika na kukata simu.
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa alisema kuwa halifahamu suala hilo kabisa na wala hajasikia tetesi kama kuna kitu kama hicho kutoka ndani na nje ya chama.