CCM siyo ya Nape na Polepole

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Ili kuepuka mitandao na makundi maslahi ndani ya CCM kuvuruga ustawi wa chama na ili kutorudia makosa ya 2015 yaliyokipasua chama, ninashauri CCM imuue nyani bila kumuangalia usoni, ninamaanisha wote Nape na Polepole ni "madegenyanga" wachukuliwe hatua sawia ili ku-harmonize hali hii inayotishia mpasuko katika kipindi cha majaribu ya chama na kutoa funzo kwa wengine wenye tabia na nia kama zao. Ikumbukwe kwa CCM maandalizi ya uchaguzi mkuu mwingine yanaanza pale ambapo uchaguzi mkuu uliopita ulikoishia. Bila kujali Nape ana mizizi mirefu ya kihistoria kwenye chama kumzidi Polepole ambaye ni mtoto wa mkulima wa mihogo Tanga, vikao vifanye kazi ya msumemo ya kukata mbele na nyuma kwasababu wote wawili wana mtaji wa wanachama/wafuasi. Mwenye masikio na asikie, mwenye macho na aone, asomaye na afahamu.

1639639506906.png
1639639544815.png

Taswira zote kwa hisani ya google.
 
Wengine baba zao walikuwa waburudishaji kwenye vita wakati wanaume wanapigana.

Leo wanasema wao ndio pekee na vizazi vyao ndio wanastahili ulaji wa keki ya taifa
Mkuu,

To know the road ahead ask those coming back.

Polepole anatakiwa amuulize Nape njia mbeleni ikoje?

Namshauri Polepole hivi, kwa kuwa safu ya JPM imeondoka, ajifunze kuishi kwa ku-mutate kama kirusi cha Corona, kinyume na ushauri huu aandae nchi ya kukimbilia kama Lissu.
 
Eleza tuhuma za kila mmoja ambazo unadhani ni ukiukwaji wa kanuni za chama hicho.
 
polepole ni mwana CCM mwenzetu - tumjibu hoja zake !!
Mkuu,

Kuna majira hoja hazitakiwi hata kama ni nzuri. Membe aliomba asikilizwe hoja zake lakini kumbe ombi lake lilitoka majira ambayo hoja hazikutakiwa.

Polepole akubali tu kuwa cheo ni dhamana kama imani ya chama inavyosema.

Kosa la Polepole ni kutotumia dhamana ya cheo alichokuwa nacho kipindi hicho ambacho hoja hazikutakiwa (hawakutaka hoja) kujenga mfumo ambao kumbe ungekuja kumpa fursa ya hoja zake kusikilizwa leo ambapo dhamana yake imetanguka.
 
Polepole naye ni mmoja ya wasiojulikana. Wasiojulikana maana yake ni watu wanaofanya kazi kwa siri lakini tunaishi nao mtaani..
Kwahiyo ni UNKNOWN WHO IS KNOWN?

Mbona sasa hatumchukulii hatua za kisheria kama tunamjuwa kuwa anafanyakazi kwa siri na tunaye mtaani?

Mkuu, hii ya Polepole ni #agendasetting, yaani tuna strategize to Lowassalize 2025.
 
Silence is death, and you, if you talk, you die, and if you remain silent, you die. So, speak out and die. Tahar Djaout

Kwahiyo Polepole inabidi tu aongee au siyo?
Lakini mbona Makamba aliongea na yupo hadi leo? Mbona Warioba anaongeaga na yupo hadi leo? Kwahiyo tutarajie Polepole naye aongee na aendelee kuwepo hadi mtondogoo... CCM ina wenyewe.....
 
Kwahiyo ni UNKNOWN WHO IS KNOWN?

Mbona sasa hatumchukulii hatua za kisheria kama tunamjuwa kuwa anafanyakazi kwa siri na tunaye mtaani?

Mkuu, hii ya Polepole ni #agendasetting, yaani tuna strategize to Lowassalize 2025.
Mkuu kumbe ndo mpango mzima wa Lowassalize 2025? Kweli CCM wameanza kutusomesha namba za rangi nyingine basi.
 
Mkuu,

Kuna majira hoja hazitakiwi hata kama ni nzuri. Membe aliomba asikilizwe hoja zake lakini kumbe ombi lake lilitoka majira ambayo hoja hazikutakiwa.

Polepole akubali tu kuwa cheo ni dhamana kama imani ya chama inavyosema.

Kosa la Polepole ni kutotumia dhamana ya cheo alichokuwa nacho kipindi hicho ambacho hoja hazikutakiwa (hawakutaka hoja) kujenga mfumo ambao kumbe ungekuja kumpa fursa ya hoja zake kusikilizwa leo ambapo dhamana yake imetanguka.
Hili limekuwa kosa la viongozi wetu wengi. Wakiwa na madaraka hawayaoni mapungufu hasa ya katiba. Lakini once wanapotoka/kutolewa ndiyo huja na "KATIBA MBOVU". Na kulalamika

Nyerere alilalamikia ubovu huo , lakini ni baada ya kutoka madarakani. The same na Warioba, Lowassa, Sumaye, Polepole etc .

Polepole alikuwa na nafasi ya kuishauri serikali na Maghufuli juu ya ubovu wa katiba na ueñdeshaji wa serikali kwa ujumla wake. Leo nani atamuelewa wakati ubovu/uhuni huo ni masilahi kwa waliopo
 
Back
Top Bottom