tzkwanza
JF-Expert Member
- Dec 27, 2018
- 1,567
- 3,611
Kuna watu wamekatwa majina kwa sababu tu ni marafiki wa Membe. Sasa hivi CCM hata uhuru wa kuongea na mtu asiyepatana na mwenyekiti haupo. Taifa linakwenda wapi?
Kuna watu walitoa rushwa hadharani kama Kingwangala, Waitara na Gambo ila majina yamepitishwa. Kuna wengine wamekatwa kwa kisingizio cha rushwa. RPC wa Arusha pamoja na mkuu wa TAKUKURU walitolewa kisa rushwa za Gambo ila mtoa rushwa karudi wao wamekwenda na maji. Na siku zote Gambo waliambia nimetumwa na mwenyekiti nimtoe Lema ndio maana wakamuacha, leo ukweli upo hadharani.
Kuna watu walitumbuliwa kisa urafiki na Lowasa leo wamerudishwa na chama kimechonga maadui wengine feki, eti marafiki wa Membe.
Polepole na Bashiru mlimshauri mwenyekiti anunue wabunge wa CHADEMA na CUF leo hii mnalazimisha kuwanadi. Hao watu upinzani hawatakiwi na CCM hawatakiwi. Mwambe, Gekul, Katambi na Silinde walipigwa chini na wajumbe ila nyie mnalazimisha kuwapa ubunge.
Patachimbika; hizo ni dharau kubwa sana. Polisi hawawezi kushindana na nguvu ya umma. Mliona kilichotokea Tunduma? au mmepanga kumwaga damu za watu ilimradi tu Silinde ashinde?
Kuna watu walitoa rushwa hadharani kama Kingwangala, Waitara na Gambo ila majina yamepitishwa. Kuna wengine wamekatwa kwa kisingizio cha rushwa. RPC wa Arusha pamoja na mkuu wa TAKUKURU walitolewa kisa rushwa za Gambo ila mtoa rushwa karudi wao wamekwenda na maji. Na siku zote Gambo waliambia nimetumwa na mwenyekiti nimtoe Lema ndio maana wakamuacha, leo ukweli upo hadharani.
Kuna watu walitumbuliwa kisa urafiki na Lowasa leo wamerudishwa na chama kimechonga maadui wengine feki, eti marafiki wa Membe.
Polepole na Bashiru mlimshauri mwenyekiti anunue wabunge wa CHADEMA na CUF leo hii mnalazimisha kuwanadi. Hao watu upinzani hawatakiwi na CCM hawatakiwi. Mwambe, Gekul, Katambi na Silinde walipigwa chini na wajumbe ila nyie mnalazimisha kuwapa ubunge.
Patachimbika; hizo ni dharau kubwa sana. Polisi hawawezi kushindana na nguvu ya umma. Mliona kilichotokea Tunduma? au mmepanga kumwaga damu za watu ilimradi tu Silinde ashinde?