Naukumbuka wimbo mzuri wa Kihehe,
"Nige nene ngwalala, nige nene ngwalala, nige nene ngwalala ngwalala baba singumuwona x2
Ngwenda bee, Ee ngwenda ndimuwonage X2
MAANA YA WIMBO KIMAELEZO:
Jamaa analia kwa kufiwa na baba yake anasema "hakika mimi namtafuta baba yangu kwasababu napenda niwe namuona muda wote lakini, simuoni"
Mytake:
Watanzania wengi sasa hivi tunamkumbuka Baba wa Taifa, hata hao wanaotudanganya na kupaa mabegani mwetu kisha wanaanza kuchuma utajiri wetu na kuupeleka nje ya nchi wanajitahidi sana kutumia jina la Baba wa Taifa kupata kura zetu. Tuanze sasa kuwaogopa hawa jamaa kama ukoma. Wamekuwa wakijiita ni matajiri wa watu na kamwe hawawezi kufilisika hii ni kutukejeli sisi masikini. Tafisri ya kauli ya Lowassa kuwa yeye si tajiri wa fedha bali watu ni kwamba katufanya sisi ni rasilimali kwa ajili yake binafsi. Kwa maana nyingine kwa tafsiri ya kiingereza anasema "We are his property thus he will never get poor, our existence is his wealth our disappearence is poverty and of course never shall we see his povery for we are dead."