CCM Pambalama!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
CCM Pambalama, CCM Pambalama, kocheleli CCM eee, kocheleli CCM Pambalama Kochelele...

Fukuto la fukuta, moshi wafoka, mapovu yanamwagika, CCM imefika njia panda! Ama isuke au inyoe!

Hili vurugu la Richmond, likizingirwa na BOT EPA, BOT CIS, BOT Minara, Rada, Kiwira, Buzwagi na moto kutoka Upinzani, unafanya mambo kadhaa tujiandee kutokea.
  1. Wabunge ambao si mtandao, wenye uchungu wa kweli wa CCM, kuendelea kusulubisha viongozi wao na Serikali yao iwe wazi. Hawa wabunge, mwokozi wao na nguzo yao ni Wastaafu Malecela, Kawawa, Mwinyi, Salim na Msuya. Huku wako hawa walioshupalia RDC;-Mwakyembe, Kilango-Malecela, Seleli, Kimaro, n.k.
  2. Team Mkapa; huku ni wale wajanja wa Che-Nkapa ambao bado wanatibu majeruhi ya mchakato wa kugombea Urais 2005 na kunyang'anywa tonge la Hatamu za Chama. Hapa kuna Mang'ula, Ngwilizi, Kigoda, Kinana, Warioba na Ruhinda. Katika kundi hili, pia wapo wale waliotajirika na mradi wa Ujasirimali Ikulu; Yona, Mramba, Mgonja, Mkono n.k.
  3. Mtandao; Kundi hili lina majeruhi wengi kutokana na kuvunjwa kwa baraza la mwazirina mwegemeo wa kashfa za ufisadi kuwa kwenye shingo zao. Kundi hili, limegawanyika katika sura mbili;
    1. Team Kikwete ambayo wamebakia Makamba, Chiligati, Membe, Migiro, Karume
    2. Team Rostwassa(Rostam/Lowassa); Karamagi, Msabaha, Nchimbi, Apson, Meghji, Kamala, Diallo, Chenge,
  4. Wasiofungamana lakini wana nguvu na ni tishio; Pinda, Mwandosya, Sumaye, Balali, Salmin, Magufuli, Msekwa na Sitta.
Kutokana na kuwepo makundi haya makubwa na utata unaotambaa angani hasa baada ya Lowassa kuangushwa na minong'ono kuwa naye Lowassa ana ushahidi wa kujikosha, linalobakia kwetu watazamaji ni kupima upepo na kuomba dua wapigane na wagawanyike ili tujue nani ni kwa manufaa ya Taifa na nani ni mnyonyaji.

Nanukuu baadhi ya mambo ambayo yanaashiria kuwa huko CCM si salama, na hata kama wakitoka nje ya ukumbi wakiwa wamekumbatiana, tusiwaamini.

 
Rev kishoka...lazima uanzishe thread kila ukisoma gazeti linakuvutia? si lazima kila mtu aanzishe thread...hata hujui ipi muhim...take time kusoma walichoweka wenzako, then weka mchango na sources zako.

Pia Muhimu kuweka the whole story? au http link inatosha..mnajaza space bila mpango ktk JF.
 

Kaka/Dada Chuma,

Mimi nimeanza mjadala kuijadili CCM na hata nikatoa mapendekezo na kuonyesha mgawanyiko. Je ni kosa gani nililofanya kuweka viambatanishi? je unayakupinga kuhusiana na mimi kuweka CCM katika kambi nne?

Je hukuona mchango wangu na maoni yangu yalikuwa juu ya viambatanishi? Kama hukuwa na la kuzungumza si ungekaa kimya basi kwa maana nawe umejaza nafasi bila mpango kwa kushindwa kujibu hoja na kuanza kupigia mawe nukuu!
 

Rev Kishoka,

Asante sana kwa hii thread!

Very well thought analysis!
 
Chuma,
Ukifika kwenye hiyo thread fumba macho, usiifungue, wala huwezi kuona nini kimeandikwa.
 
Unafahamu Rev Dec 2007 nilihudhuria maombi katika sehemu ya kijijini kabisaa. Lakini nikagundua watu wakichoka wanaunganisha nguvu kutafuta msaada. Miongoni mwa items za maombi zilikuwa. 1. Tuombee mfumo mzima wa serkali yetu Mungu aupindue kabisa na ili siasa za kihuni zikome na watu makini na waadilifu wavutiwe kuingia katika siasa. La ajabu maombi 2 yaliyofuata yalikuwa kuombea Takukuru iache kufanya kazi kisanii bali wapambane na rushwa kweli na jingine lilisema iombee Tanesco ili kongwa la madeni iliyobebeshwa ituliwe na bei za umeme zishuke. Naona kinachoendelea Tanzania na hata ndani ya CCM Mungu ameamua kujibu kilio cha wanyonge kama wana wa Israel walivyosikiwa walipokuwa utumwani Misri.
 
ccm PAMBALAMAAA!! POTELEELII..CCM PAMBALAMA POTELELII..CCM PAMBLAMA POTELELII..CCM PAMBALAMA POTELELI CCM EEEEEE ..POTELELI CCM PAMBALAMA POTELELIIIII!!!

UNANIKUMBUSHA NYIMBO ZA USHINDI ENZI YA MWALIMU!!!!
 
ccm PAMBALAMAAA!! POTELEELII..CCM PAMBALAMA POTELELII..CCM PAMBLAMA POTELELII..CCM PAMBALAMA POTELELI CCM EEEEEE ..POTELELI CCM PAMBALAMA POTELELIIIII!!!

UNANIKUMBUSHA NYIMBO ZA USHINDI ENZI YA MWALIMU!!!!
 
ccm PAMBALAMAAA!! POTELEELII..CCM PAMBALAMA POTELELII..CCM PAMBLAMA POTELELII..CCM PAMBALAMA POTELELI CCM EEEEEE ..POTELELI CCM PAMBALAMA POTELELIIIII!!!

UNANIKUMBUSHA NYIMBO ZA USHINDI ENZI YA MWALIMU!!!![/B
]
 

Nakuuliza kwa mara ya pili hivi wewe una cheo gani hapa mpaka uwasemee hovyo wana JF wanaotuma habari hapa ukumbini!?
Ni lini ulichaguliwa kuwa msemaji wa kuwakataza wanaJF watume article nzima na badala yake watume link tu!? Kama unakerwa basi anzisha forum yako na huko weka sheria unazozitaka hakuna atakayekuingilia, lakini hapa huna ubavu wa kuamua nini kitumwe na nini kisitumwe.
 
Rev kishoka, kudos kwa point zako.Pia umenikumbusha mbali sana, "Tumbuizo Asilia" kipindi nilikuwa nakichukia sana utotoni lakini sasa hivi ningependa sana kuzisikia nyimbo zilizokuwa zinapigwa.
 
Kama mwalimu alivyowahi kusema, kwamba upinzani serious utatokana na CCM yenyewe. So hopefully kundi moja la mafisadi litaamua kujiengua na kuanzisha chama chao ili kupambana na mafisadi wengine. But in that case, ni watanzania ndio watakuwa loosers, maana chama cha serikali na chama cha upinzani wote watakuwa ni mafisadi.
 
REV.sasa ni kuwa hawa jamaa wamegawanyika sana na kwa kweli huenda kuna kitu kikubwa sana kinaweza kutokea hapo mbeleni kwani hawa jamaa wanaonekana kujipanga upya na kuanza kudai ahadi zao walizokuwa wamejiwekea na JK kabla hajaingia ikulu.
 
CCM PAMBALAMAAA!! POTELEELII..CCM PAMBALAMA POTELELII..CCM PAMBLAMA POTELELII..CCM PAMBALAMA POTELELI CCM EEEEEE ..POTELELI CCM PAMBALAMA POTELELIIIII!!

Hii ni lugha ghani? au ndio kama zile nyimbo za halaiki,(sijui kilikuwa kisauzi au kimsumbiji kile)

angalu nimeongeza siku za kuishi kwa kucheka.

Mchungaji Kanyaga twende kwa amani ya bwana
 
KASANI wimbo huo ni kwa lugha ya kifipa. Nakumbuka uliimbwa wakati wa kutoa zawadi ya Trekta kwa best ujamaa village kwa kina majiyatanga.
 
Sasa ndio itakuwa ni vizuri sana kama vyama vyote vitakuwa ni vya wafisadi.

Tutakuwa na CCM-Fisadi nr.1
Na pia CCM-Fisadi nr.2

Vyama hivi vitashindana kama vile timu zetu za mpira. Tukumukeni YATAKIWA MWIZI ILI AWEZE KUMKAMATA MWIZI MWINZIE AU JAMBAZI.
Kwani mbinu ni zile zile tu.
 
Pamoja na kuhisi mtafuruku ndani ya safu ya uongozi, naffikiri kama uchaguzi ungekuwa kesho, CCM wangepoteza viti vingi.

Ili kujihami, wanaandaa maandamano nchi nzima kulipongeza Bunge "kwa kazi nzuri" kuhusu Richmond. Hivi kwa nini wasisubiri majibu ya EPA ndipo waone kama kweli maandamano ni muhimu?

Ni aibu sana ikiwa wanajimbo wnashangilika kuanguka kwa Mbunge wao ambaye alikuwa waziri (Ngasongwa)!
 
Ili kujihami, wanaandaa maandamano nchi nzima kulipongeza Bunge "kwa kazi nzuri" kuhusu Richmond. Hivi kwa nini wasisubiri majibu ya EPA ndipo waone kama kweli maandamano ni muhimu?

Labda wana mpango wa kuizima hiyo hoja ya kui-table report ya EPA Bungeni. Ngoja tusubiri keshokutwa watakuwa na agenda gani bungeni. Kitendo cha JK kumuweka Marmo kwenye uratibu wa Bunge ni dalili za kutaka kulidhibiti Bunge kikamilifu, nahisi Dr. Burian hawana imani nae sana kama anaweza kulidhibiti Bunge. Na kwa kuwa Mh. Mizengwe Pindamgongo amekiri kwamba yeye si mwana siasa ingekuwa ngumu kwa hao wawili (Burian na Pinda) kulidhibiti bunge kwa malengo ya kuilinda serikali.

Ngoja tuone sarakasi zitakavyochezwa, maana Sitta sijui kama atakubali chama chake kigalagazwe huku akikiona na yeye ni mjumbe wa CC.
 
Hoja nimeipenda, nitairudia kuchangia lakini naomba kwanza nianze na huu wimbo. Mbona mmebadilisha maneno yake? Kwa kumbukumbu yangu huu wimbo ni wa kichaga, niliwasikia sana wakiuimba enzi tuko Moshi (wakati huo CCM ilikuwa na miaka miwili tu!). Enzi hizo watumishi wa serikali walikuwa wanalazimika kujiunga na mgambo ili wapate cheo kwenye CCM, tulikuwa tunawasikia wakiimba huu wimbo pale uwanja wa shule ya Msingi Muungano ambayo ilikuwa nyuma ya ofisi za RDD wa Moshi:

CCM kyaambalama kocheenyi,
CCM kyaambalama kocheenyi,
CCM kyaambalama kocheenyi CCM eeeh,
Kocheenyi CCM kyaambalama kocheenyi!


Sikuwahi kusumbuka kutaka kujua maana yake wakati huo, lakini kwa kuwa mmenikumbusha naomba wachaga walioko kwenye forum hii wanipe tafsiri yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…