Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
- Thread starter
- #21
Hoja nimeipenda, nitairudia kuchangia lakini naomba kwanza nianze na huu wimbo. Mbona mmebadilisha maneno yake? Kwa kumbukumbu yangu huu wimbo ni wa kichaga, niliwasikia sana wakiuimba enzi tuko Moshi (wakati huo CCM ilikuwa na miaka miwili tu!). Enzi hizo watumishi wa serikali walikuwa wanalazimika kujiunga na mgambo ili wapate cheo kwenye CCM, tulikuwa tunawasikia wakiimba huu wimbo pale uwanja wa shule ya Msingi Muungano ambayo ilikuwa nyuma ya ofisi za RDD wa Moshi:
CCM kyaambalama kocheenyi,
CCM kyaambalama kocheenyi,
CCM kyaambalama kocheenyi CCM eeeh,
Kocheenyi CCM kyaambalama kocheenyi!
Sikuwahi kusumbuka kutaka kujua maana yake wakati huo, lakini kwa kuwa mmenikumbusha naomba wachaga walioko kwenye forum hii wanipe tafsiri yake.
Kithuku,
Miye nilisikia kwenye Mbiu za Mikoa, Asilia Salamu na vipindi vingine vilivyopiga muziki wa kilugha (kikabila). Sijui asili yake ni kabila gani wala maana yake. Nilivyouimba hapa ni jinsi nilivyojitahidi kukumbuka.
Lakini nia kubwa haikuwa kuimba wimbo, bali ni kuijadili CCM ambayo ilisifika enzi zileeee...na sasa unanuka uvundo na uozo!