CCM, Operation TUJISAHIHISHE irudiwe tena!

CCM, Operation TUJISAHIHISHE irudiwe tena!

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
17,563
Reaction score
28,524
Kwa machalii na dogo wengi, hawawezi kuijua hii Operation Tujisahihishe , ambao ulikuwa msimamo wa chama TANU, Mwaka 1976/77.

Mwalimu, a thinker, strategist na visionary, aliliona tatizo katika misimamo ya chama, misimamo ambayo ilileta utata na matatizo makubwa katika jamii.

Mojawapo ya matatizo ni msimamo wa chama cha TANU Operation Musoma, ambapo wanafunzi wote waliomaliza Form VI walitakiwa kwenda JKT kwa mwaka mmoja na kujajiriwa kwa mwaka ndipo waende Chuo Kikuu chochote.

Athari zake zilikuwa kubwa na mbaya sana, hasa kwa wanawake, waliopoteza nafasi za kusoma na kuishia kuolewa.

Operation TUJISAHIHISHE, ya 1976, ilikuja ondoa kabisa kadhia hii, kwa kujisahihisha wenyewe, na sasa CCM kusonga mbele.

CCM ya sasa na vikao vyake vya Kamati zKuu na Halmashauri Kuu hadi Mkutano Mkuu, havijaweza mpaka sasa kuwa na ujasiri wa kutamka wazi wazi madudu ya kutisha, ya kisiasa ya Awamu ya Tano.
Awamu ya Tano ni zao la CCM.

Hatuwezi kuwaachia wapinzani, kina Zito wa ACT, ndio watuonyeshe njia sahihi wakati nasi tulikuwepo na tuliona madudu na tunajua namna ya kuyasahihisha.

Naamini Komredi Kinana, na hata Kikwete miaka ya Operation Tujisahihishe walikuwa vijana wa TANU.
Hili ni somo ambalo chama, kwanza kikubali makosa makubwa yalitendeka , pili chama kitamke namna ya kuyasahihisha ili yasirudiwe tena.

Huo ndio utakuwa ukomavu wa kisiasa kwa chama CCM.
 
Ni ngumu kwa Sasa kuanzisha operation aina hiyo kwa sababu itakuwa kwa sehemu kubwa kuzungumzia madudu ya awamu ya tano. Tatizo ni kwamba masalia ya Magufulist bado wapo wengi na wanaweza kukiletea chama chao mtikisiko mkubwa sana.
Tayari Kuna tetesi ya kuanzishwa chama Cha masalia hao ingawa kwa ubabe wa CCM hakiwezi kusajiliwa aslan.
 
Hayo ni pamoja na madudu ya wizi .ambayo hayatokani na msimamo wa chama.
Uchaguzi wa Serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020 CCM ingeshindwa vizuri tu,

Mwendazake akataka kushinda kwa asilimia 99 ili aonekane ameipa CCM ushindi mkubwa kuliko Marais wote, mjinga Sana

Uchaguzi wa 2015 uliokuwa na ushindani mkubwa kuliko zote kuwahi kutokea CCM ilishinda bila wapinzani kuenguliwa, kuuawa Wala mitandao kuzimwa
 
Ni ngumu kwa Sasa kuanzisha operation aina hiyo kwa sababu itakuwa kwa sehemu kubwa kuzungumzia madudu ya awamu ya tano. Tatizo ni kwamba masalia ya Magufulist bado wapo wengi na wanaweza kukiletea chama chao mtikisiko mkubwa sana.
Tayari Kuna tetesi ya kuanzishwa chama Cha masalia hao ingawa kwa ubabe wa CCM hakiwezi kusajiliwa aslan.
Mkuu CCM, kwa muda mrefu tu ujao, kitakuwa ni chama kinachoonyesha dira ya mustakabali na muelekeo wa wananachi wa Tanzania.Na CCM ni chama kikubwa kuliko mtu yeyote.
CCM lazima iendeshwe na mawazo chanya, hakiwezi kujifungia na kutekwa katika pressure groups za ukabila, ubaguzi hata ukanda.

Kujisahihisha ni muhimu kwani chama kutakuwa kime preempt matatizo yake yenye athari mbaya katika jamii.

Vilevile kujisahihisha ndio guarantee kwamba makosa yaliyofanyika hayatarudiwa tena.
 
Hapo ndio pagumu kwa CCM, huo ni mfupa mgumu sana kwa CCM.

Kabla ya kuelekea kwenye tume huru ya uchaguzi ni lazima kufanya MARIDHIANO ya kweli kwa walioumizwa au watoe KATIBA MPYA.

KUNAHITAJIKA SANA UTASHI WA KISIASA vinginevyo CCM ya sasa itaitwa CCM ya MAFISADI
Hapo CCM watakuua mchana kweupe
 
Kwanini CCM ilipora uchaguzi mkuu?

Kwakuwa imeishiwa ushawishi na inaona aibu kukubali, na sana sana hofu yao kubwa watakapotoka madarakani wengi wao wataishia jela kutokana na wizi na unyama waliofanyia wananchi.
 
Tatizo kumpata wa kuwaweka pamoja awasahihishe ndo hayupo. Kabla ya Decemba tutakuwa tumeona mengiiiii!
 
Mkuu CCM, kwa muda mrefu tu ujao, kitakuwa ni chama kinachoonyesha dira ya mustakabali na muelekeo wa wananachi wa Tanzania.Na CCM ni chama kikubwa kuliko mtu yeyote.
CCM lazima iendeshwe na mawazo chanya, hakiwezi kujifungia na kutekwa katika pressure groups za ukabila, ubaguzi hata ukanda.

Kujisahihisha ni muhimu kwani chama kutakuwa kime preempt matatizo yake yenye athari mbaya katika jamii.

Vilevile kujisahihisha ndio guarantee kwamba makosa yaliyofanyika hayatarudiwa tena.

Kimsingi ccm sio chama cha kizazi cha sasa, na kwa bahati mbaya hawakubaliani na ukweli huu, kwani ccm kwao ni chaka la kutokea kimaisha. Ccm ya enzi hizo kabla hatujazaliwa iliweza kujisahihisha maana ilikuwa peke yake, na ilikuwa chama cha kizazi hicho. Kwasasa ccm haithubutu kujisahihisha maana solution yake ni yenyewe kutoka madarakani kwa amani, jambo ambalo walamba asali hawako tayari.

Namna pekee ya kutoa vyama vikongwe vya aina hii hasa vyenye mizizi ya ujamaa ni machafuko tu. Sioni tena wananchi wakijitokeza kupiga kura baada ya wizi wa hapo nyuma, na Magufuli alipoingia madarakani ndio akalinajisi wazi wazi box la kura. Na kwa hakika vitu Magufuli alivyofanikiwa ni kuua demokrasia ya kupiga kura, na siioni ccm hii iliyoishiwa ushawishi ikirejea kwenye nidhamu ya box la kura. Namna pekee ni machafuko maana hawawezi kujisahihisha kwani hawana ushawishi tena, na sio chama cha kizazi hiki.
 
Kimsingi ccm sio chama cha kizazi cha sasa, na kwa bahati mbaya hawakubaliani na ukweli huu, kwani ccm kwao ni chaka la kutokea kimaisha. Ccm ya enzi hizo kabla hatujazaliwa iliweza kujisahihisha maana ilikuwa peke yake, na ilikuwa chama cha kizazi hicho. Kwasasa ccm haithubutu kujisahihisha maana solution yake ni yenyewe kutoka madarakani kwa amani, jambo ambalo walamba asali hawako tayari.

Namna pekee ya kutoa vyama vikongwe vya aina hii hasa vyenye mizizi ya ujamaa ni machafuko tu. Sioni tena wananchi wakijitokeza kupiga kura baada ya wizi wa hapo nyuma, na Magufuli alipoingia madarakani ndio akalinajisi wazi wazi box la kura. Na kwa hakika vitu Magufuli alivyofanikiwa ni kuua demokrasia ya kupiga kura, na siioni ccm hii iliyoishiwa ushawishi ikirejea kwenye nidhamu ya box la kura. Namna pekee ni machafuko maana hawawezi kujisahihisha kwani hawana ushawishi tena, na sio chama cha kizazi hiki.
Nakubaliana na thinking behind , lakini solution ya machafuko ni hatari sana and you cant predict the outcome.
Zambia ya sasa uchumi ni matatizo makubwa baada ya miaka ya unpredictable changes.
 
Kwa machalii na dogo wengi, hawawezi kuijua hii Operation Tujisahihishe , ambao ulikuwa msimamo wa chama TANU, Mwaka 1976/77.

Mwalimu, a thinker, strategist na visionary, aliliona tatizo katika misimamo ya chama, misimamo ambayo ilileta utata na matatizo makubwa katika jamii.

Mojawapo ya matatizo ni msimamo wa chama cha TANU Operation Musoma, ambapo wanafunzi wote waliomaliza Form VI walitakiwa kwenda JKT kwa mwaka mmoja na kujajiriwa kwa mwaka ndipo waende Chuo Kikuu chochote.

Athari zake zilikuwa kubwa na mbaya sana, hasa kwa wanawake, waliopoteza nafasi za kusoma na kuishia kuolewa.

Operation TUJISAHIHISHE, ya 1976, ilikuja ondoa kabisa kadhia hii, kwa kujisahihisha wenyewe, na sasa CCM kusonga mbele.

CCM ya sasa na vikao vyake vya Kamati zKuu na Halmashauri Kuu hadi Mkutano Mkuu, havijaweza mpaka sasa kuwa na ujasiri wa kutamka wazi wazi madudu ya kutisha, ya kisiasa ya Awamu ya Tano.
Awamu ya Tano ni zao la CCM.

Hatuwezi kuwaachia wapinzani, kina Zito wa ACT, ndio watuonyeshe njia sahihi wakati nasi tulikuwepo na tuliona madudu na tunajua namna ya kuyasahihisha.

Naamini Komredi Kinana, na hata Kikwete miaka ya Operation Tujisahihishe walikuwa vijana wa TANU.
Hili ni somo ambalo chama, kwanza kikubali makosa makubwa yalitendeka , pili chama kitamke namna ya kuyasahihisha ili yasirudiwe tena.

Huo ndio utakuwa ukomavu wa kisiasa kwa chama CCM.
Ipo siku itafika mtasema bora ata awamu ya 5 tulikuwa tunaonanna kushika vitu kuliko sasa tunasikia maneno tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa machalii na dogo wengi, hawawezi kuijua hii Operation Tujisahihishe , ambao ulikuwa msimamo wa chama TANU, Mwaka 1976/77.

Mwalimu, a thinker, strategist na visionary, aliliona tatizo katika misimamo ya chama, misimamo ambayo ilileta utata na matatizo makubwa katika jamii.

Mojawapo ya matatizo ni msimamo wa chama cha TANU Operation Musoma, ambapo wanafunzi wote waliomaliza Form VI walitakiwa kwenda JKT kwa mwaka mmoja na kujajiriwa kwa mwaka ndipo waende Chuo Kikuu chochote.

Athari zake zilikuwa kubwa na mbaya sana, hasa kwa wanawake, waliopoteza nafasi za kusoma na kuishia kuolewa.

Operation TUJISAHIHISHE, ya 1976, ilikuja ondoa kabisa kadhia hii, kwa kujisahihisha wenyewe, na sasa CCM kusonga mbele.

CCM ya sasa na vikao vyake vya Kamati zKuu na Halmashauri Kuu hadi Mkutano Mkuu, havijaweza mpaka sasa kuwa na ujasiri wa kutamka wazi wazi madudu ya kutisha, ya kisiasa ya Awamu ya Tano.
Awamu ya Tano ni zao la CCM.

Hatuwezi kuwaachia wapinzani, kina Zito wa ACT, ndio watuonyeshe njia sahihi wakati nasi tulikuwepo na tuliona madudu na tunajua namna ya kuyasahihisha.

Naamini Komredi Kinana, na hata Kikwete miaka ya Operation Tujisahihishe walikuwa vijana wa TANU.
Hili ni somo ambalo chama, kwanza kikubali makosa makubwa yalitendeka , pili chama kitamke namna ya kuyasahihisha ili yasirudiwe tena.

Huo ndio utakuwa ukomavu wa kisiasa kwa chama CCM.
Kwaakili yako kabisa unadhani zito ni mpinzani?huyo ni kibaraka...na mzee wa kuhamisha hoja.

#MaendeleoHayanaChama
 
Uchaguzi wa Serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020 CCM ingeshindwa vizuri tu,

Yule shetani akataka kushinda kwa asilimia 99 ili aonekane ameipa CCM ushindi mkubwa kuliko Marais wote, mjinga Sana

Uchaguzi wa 2015 uliokuwa na ushindani mkubwa kuliko zote kuwahi kutokea CCM ilishinda bila wapinzani kuenguliwa, kuuawa Wala mitandao kuzimwa
Ccm haijawahi kushinda..ni wizi wa kura na mabavu...kupitia tume na vyombo vya dola.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nakubaliana na thinking behind , lakini solution ya machafuko ni hatari sana and you cant predict the outcome.
Zambia ya sasa uchumi ni matatizo makubwa baada ya miaka ya unpredictable changes.
War is the way of peace..kuna muda ili mambo yenda sawa kwa haki na usawa..chaos lazima iwe suluhusho pekee.

Njia za kidiplomasia zikifeli njia za mabavu huchukua hatamu.

Vinginevyo wahuni wachache watajineemesha kupitia maumivu na jasho la wengi.

#MaendeleoHayanaChama
 
War is the way of peace..kuna muda ili mambo yenda sawa kwa haki na usawa..chaos lazima iwe suluhusho pekee.

Njia za kidiplomasia zikifeli njia za mabavu huchukua hatamu.

Vinginevyo wahuni wachache watajineemesha kupitia maumivu na jasho la wengi.

#MaendeleoHayanaChama
Internal strife huwa haihakikishi upande wowote kushinda, na if anything, it might make things worser.
Mapinduzi ya Bolshevik mwaka 1917, yaliingiza ukomunisti katika Urusi, ambao upo hadi leo.
Na leo tunaona wajukuu wa mapinduzi hayo, kina Putin.
 
Back
Top Bottom