CCM na watumishi wa umma

CCM na watumishi wa umma

gidamulida

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
286
Reaction score
95
SHIKAMOOO MAGUFULI.

Nchi imeanza kurudi kwenye misingi yake.

Watumishi wa UMMA wote si vyema hata kidogo kutofautiana na ilan ya CCM ama kutokukubaliana na mtizamo wa RAIS.

kama wapo baadhi ni wale Malofa na mbumbumbu wasiotaka kukubali ukweli unaowazunguka.

Si busara kukaa kijiweni unakosoa utendaji kazi wa serikali wakati wewe ni mtumishi wa UMMA ambaye ni sehemu ya Serikali.

Kama kuna matatizo ama changamoto zinazokukwaza katika utekelezaji wa majukumu yako tumia vikao, weka mikakati ya utekelezaji na tumia vizuri hekima uliyopewa ili kuishauri serikali. Kuwa m-bunifu. Acha kukaa kijiweni ili uonekane mzunguzaji kwa kukosoa serikali.

Endapo kijiweni kwako imetokea watu wanakosoa serikali, ni wajibu wako kuitetea serikali kwa nguvu zote maana mtumishi wa UMMA ni sehemu ya Serikali ya CCM.

Kinachonikera ni pale ninapowasikia watumishi wa UMMA wamekazania kuikosoa serikali wakati wananchi wanapokuwa wanailalamikia serikali kwa kutowapatia huduma fulani. Mara nyingine huenda inatokea kati ya huduma inayolalamikiwa mtumishi wa UMMA huyo anakuwa ni sehemu ya watumishi wanaotakiwa kuelezea au kutetea utoaji huduma. Badala yake anajitoa ufahamu ( hapa ndo unajitwika ulofa au umbumbumbu) anaanza kuikandia serikali ya CCM.

Si bure mara nyingi watumishi ya jinsi hii ni wabadhilifu sana kwa mali za UMMA. hupenda kutumia kivuli cha kuilaumu serikali ya CCM ili kuwapofusha wananchi wasitambue wizi wao.

Ubovu wa Serikali ya Ccm unachangiwa na mtumishi mmoja mmoja siyo "lumpsum" wa ngazi zote kuanzia kitongoji hadi Ikulu ama kuanzia Ikulu hadi kitongoji. Kwa hiyo unapopindisha utaratibu wa utoaji huduma fulani unakuwa wewe ni msingi wa kulaumiwa kwa Serikali ya CCM.

Na watumishi wa UMMA wachache wanaofanya kazi katika misingi ya utaratibu wanakuwa wao ni sehemu kubwa ya mafanikio ya serikali ya CCM.
 
SHIKAMOOO MAGUFULI.

Nchi imeanza kurudi kwenye misingi yake.

("Huu ujumbe ni sehemu pia ya kuwafahamu Malofa na Ma-mbumbumbu")

Watumishi wa UMMA wote si vyema hata kidogo kutofautiana na ilan ya CCM ama kutokukubaliana na mtizamo wa RAIS.

kama wapo baadhi ni wale Malofa na mbumbumbu wasiotaka kukubali ukweli unaowazunguka.

Si busara kukaa kijiweni unakosoa utendaji kazi wa serikali wakati wewe ni mtumishi wa UMMA ambaye ni sehemu ya Serikali.

Kama kuna matatizo ama changamoto zinazokukwaza katika utekelezaji wa majukumu yako tumia vikao, weka mikakati ya utekelezaji na tumia vizuri hekima uliyopewa ili kuishauri serikali. Kuwa m-bunifu. Acha kukaa kijiweni ili uonekane mzunguzaji kwa kukosoa serikali.

Endapo kijiweni kwako imetokea watu wanakosoa serikali, ni wajibu wako kuitetea serikali kwa nguvu zote maana mtumishi wa UMMA ni sehemu ya Serikali ya CCM.

Kinachonikera ni pale ninapowasikia watumishi wa UMMA wamekazania kuikosoa serikali wakati wananchi wanapokuwa wanailalamikia serikali kwa kutowapatia huduma fulani. Mara nyingine huenda inatokea kati ya huduma inayolalamikiwa mtumishi wa UMMA huyo anakuwa ni sehemu ya watumishi wanaotakiwa kuelezea au kutetea utoaji huduma. Badala yake anajitoa ufahamu ( hapa ndo unajitwika ulofa au umbumbumbu) anaanza kuikandia serikali ya CCM.

Si bure mara nyingi watumishi ya jinsi hii ni wabadhilifu sana kwa mali za UMMA. hupenda kutumia kivuli cha kuilaumu serikali ya CCM ili kuwapofusha wananchi wasitambue wizi wao.

Ubovu wa Serikali ya Ccm unachangiwa na mtumishi mmoja mmoja siyo "lumpsum" wa ngazi zote kuanzia kitongoji hadi Ikulu ama kuanzia Ikulu hadi kitongoji. Kwa hiyo unapopindisha utaratibu wa utoaji huduma fulani unakuwa wewe ni msingi wa kulaumiwa kwa Serikali ya CCM.

Na watumishi wa UMMA wachache wanaofanya kazi katika misingi ya utaratibu wanakuwa wao ni sehemu kubwa ya mafanikio ya serikali ya CCM.

SHIKAMOO MAGUFULI.
Endelea kupiga kazi uadilifu unapoanzia IKULU naamini utashuka hadi kitongoji. "Huu ujumbe ni sehemu ya kuwajua Malofa na Ma- mbumbumbu"
haya, ujumbe umefika...subiri wenyewe waje kukujibu...ila mimi nakuuuliza swali moja tu: Hivi LUGUMI ni mmoja wa watumishi wa UMMA?
 
Kuitetea serikali ya CCM kwa nguvu zako zote kwa sababu ni mtumishi wa UMMA ni sawa kabisa mkuu.
Hata hospitalini dawa zikiwa hazipo/hazitoshi, madaktari na wauguzi waitetee serikali.
Shuleni kukiwa sio rafiki kwa kujifunza na kujifunzia, walimu waitetee serikali.
Maslahi ya watumishi wa UMMA yakiwa yamepuuzwa, watumishi hao watetee serikali.
Tunahitaji "Ngoma ya Ng'wanamalundi" kulikomboa taifa hili kifikra
 
Aliyewadanganya kuwa ukiwa mwanachama wa chadema ndio kujitambua ni nani??

Tangu lini Chadema imekuwa kipimo cha mtu kujitambua??

Kweli chama ambacho kinabadilisha gia angani na kuuzwa hovyo , hakina hata ofisi kwa miaka 20 ,ndio kiwe kipimo cha MTU kujielewa??

Bavicha kuna haja ya kupima bongo zenu, huenda mnamtindio wa ubongo.
 
Palipo na kweli lazima pasemwe tu. Mtumishi mzuri wa Umma ni yule anayesema kweli.
Sasa km unakubali kila kitu halafu unasema ''msema kweli ni mpenzi wa Mungu'' haitakuwa haina maana.
Ukisifia kila kitu hata km ni kibaya ww ni sawa na mbeya.
Kama unataka kuendelea lazima ukubali kukusolewa pia
 
Ng'ombe Akikatika Mkia Machungoni Hatumzuii Kuingia Zizini Lakini Wenzake Watamjua Hana Mkia!!
Mleta Mada Ni Ng'ombe
 
Utumishi wa umma sio utumwa kwa chama tawala. Watumishi wa umma hufanya kazi tofauti-wengine majukumu yao ni pamoja kutafuta matundu kwenye sera za serikali na kuyazungumzia hayo. Ni ulofa na umbumbu (nikitumia lugha yako) kama nitaona tatizo halafu nilinyamazie, kisa ni muajiriwa wa serikali. Watumishi pia ni wananchi wana uhuru wa fikra na kusema bora wazingatie sheria zao za kazi ambazo wakati mwingine ziko kuziba watu midomo.
 
Huyu mtoa mada inabidi nae akapimwe akili,inaonekana ni wale wenye vyeti feki haiwezekani serikali ifanye upuuzi alaf ww uitetee kisa ni mtumishi wa uma
Kwa mwelekeo wa mtoa mada, utumishi wa 'umma' naona utanishinda. Huu sasa utakuwa utumishi wa chama.
 
Kuitetea serikali ya CCM kwa nguvu zako zote kwa sababu ni mtumishi wa UMMA ni sawa kabisa mkuu.
Hata hospitalini dawa zikiwa hazipo/hazitoshi, madaktari na wauguzi waitetee serikali.
Shuleni kukiwa sio rafiki kwa kujifunza na kujifunzia, walimu waitetee serikali.
Maslahi ya watumishi wa UMMA yakiwa yamepuuzwa, watumishi hao watetee serikali.
Tunahitaji "Ngoma ya Ng'wanamalundi kulikomboa taifa hili kifikra
Tumia vikao kukosoa au andika write up wasilisha katika menejimenti ya taasisi ya umma uliyipo.
 
kwa hiyo wasiokuwa watumishi wa UMMA ni ruksa kutafuna fedha za UMMA halafu wanalindwa na CCM?
Si ruhusa. Na Lugumi uliyemtaja bado hajathibitika Mahakamani kuwa alitafuna fedha. Ila alipewa kazi na serikali. Anaweza kuchukuliwa hatua kama watanzania wengine tu ili mradi ushahidi unajitishereza.
 
Huyu mtoa mada inabidi nae akapimwe akili,inaonekana ni wale wenye vyeti feki haiwezekani serikali ifanye upuuzi alaf ww uitetee kisa ni mtumishi wa uma
Hata usipotetea waeleze wananchi uhalisia wa huduma unayotoa ktk utumishi wa umma si kuwa kibaraka wa Opposition party. Vyeti mmmh. Kama wenye PHD wanalialia bora kutokuwa na vyeti kabisa ila ukawa mkweli.
 
Si ruhusa. Na Lugumi uliyemtaja bado hajathibitika Mahakamani kuwa alitafuna fedha. Ila alipewa kazi na serikali. Anaweza kuchukuliwa hatua kama watanzania wengine tu ili mradi ushahidi unajitishereza.
kwa hiyo (kwa mujibu wa uelewa wako) Lugumi hana kosa lolote?
 
Kwahali hii itafika kipindi tutaambiwa ukitaka kuajiliwa ni lazima uwe na kadi ya ccm.
 
Back
Top Bottom