gidamulida
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 286
- 95
SHIKAMOOO MAGUFULI.
Nchi imeanza kurudi kwenye misingi yake.
Watumishi wa UMMA wote si vyema hata kidogo kutofautiana na ilan ya CCM ama kutokukubaliana na mtizamo wa RAIS.
kama wapo baadhi ni wale Malofa na mbumbumbu wasiotaka kukubali ukweli unaowazunguka.
Si busara kukaa kijiweni unakosoa utendaji kazi wa serikali wakati wewe ni mtumishi wa UMMA ambaye ni sehemu ya Serikali.
Kama kuna matatizo ama changamoto zinazokukwaza katika utekelezaji wa majukumu yako tumia vikao, weka mikakati ya utekelezaji na tumia vizuri hekima uliyopewa ili kuishauri serikali. Kuwa m-bunifu. Acha kukaa kijiweni ili uonekane mzunguzaji kwa kukosoa serikali.
Endapo kijiweni kwako imetokea watu wanakosoa serikali, ni wajibu wako kuitetea serikali kwa nguvu zote maana mtumishi wa UMMA ni sehemu ya Serikali ya CCM.
Kinachonikera ni pale ninapowasikia watumishi wa UMMA wamekazania kuikosoa serikali wakati wananchi wanapokuwa wanailalamikia serikali kwa kutowapatia huduma fulani. Mara nyingine huenda inatokea kati ya huduma inayolalamikiwa mtumishi wa UMMA huyo anakuwa ni sehemu ya watumishi wanaotakiwa kuelezea au kutetea utoaji huduma. Badala yake anajitoa ufahamu ( hapa ndo unajitwika ulofa au umbumbumbu) anaanza kuikandia serikali ya CCM.
Si bure mara nyingi watumishi ya jinsi hii ni wabadhilifu sana kwa mali za UMMA. hupenda kutumia kivuli cha kuilaumu serikali ya CCM ili kuwapofusha wananchi wasitambue wizi wao.
Ubovu wa Serikali ya Ccm unachangiwa na mtumishi mmoja mmoja siyo "lumpsum" wa ngazi zote kuanzia kitongoji hadi Ikulu ama kuanzia Ikulu hadi kitongoji. Kwa hiyo unapopindisha utaratibu wa utoaji huduma fulani unakuwa wewe ni msingi wa kulaumiwa kwa Serikali ya CCM.
Na watumishi wa UMMA wachache wanaofanya kazi katika misingi ya utaratibu wanakuwa wao ni sehemu kubwa ya mafanikio ya serikali ya CCM.
Nchi imeanza kurudi kwenye misingi yake.
Watumishi wa UMMA wote si vyema hata kidogo kutofautiana na ilan ya CCM ama kutokukubaliana na mtizamo wa RAIS.
kama wapo baadhi ni wale Malofa na mbumbumbu wasiotaka kukubali ukweli unaowazunguka.
Si busara kukaa kijiweni unakosoa utendaji kazi wa serikali wakati wewe ni mtumishi wa UMMA ambaye ni sehemu ya Serikali.
Kama kuna matatizo ama changamoto zinazokukwaza katika utekelezaji wa majukumu yako tumia vikao, weka mikakati ya utekelezaji na tumia vizuri hekima uliyopewa ili kuishauri serikali. Kuwa m-bunifu. Acha kukaa kijiweni ili uonekane mzunguzaji kwa kukosoa serikali.
Endapo kijiweni kwako imetokea watu wanakosoa serikali, ni wajibu wako kuitetea serikali kwa nguvu zote maana mtumishi wa UMMA ni sehemu ya Serikali ya CCM.
Kinachonikera ni pale ninapowasikia watumishi wa UMMA wamekazania kuikosoa serikali wakati wananchi wanapokuwa wanailalamikia serikali kwa kutowapatia huduma fulani. Mara nyingine huenda inatokea kati ya huduma inayolalamikiwa mtumishi wa UMMA huyo anakuwa ni sehemu ya watumishi wanaotakiwa kuelezea au kutetea utoaji huduma. Badala yake anajitoa ufahamu ( hapa ndo unajitwika ulofa au umbumbumbu) anaanza kuikandia serikali ya CCM.
Si bure mara nyingi watumishi ya jinsi hii ni wabadhilifu sana kwa mali za UMMA. hupenda kutumia kivuli cha kuilaumu serikali ya CCM ili kuwapofusha wananchi wasitambue wizi wao.
Ubovu wa Serikali ya Ccm unachangiwa na mtumishi mmoja mmoja siyo "lumpsum" wa ngazi zote kuanzia kitongoji hadi Ikulu ama kuanzia Ikulu hadi kitongoji. Kwa hiyo unapopindisha utaratibu wa utoaji huduma fulani unakuwa wewe ni msingi wa kulaumiwa kwa Serikali ya CCM.
Na watumishi wa UMMA wachache wanaofanya kazi katika misingi ya utaratibu wanakuwa wao ni sehemu kubwa ya mafanikio ya serikali ya CCM.