CCM na itikadi ya ujamaa na kujitegemea

CCM na itikadi ya ujamaa na kujitegemea

Hata mimi niliwasikia Adui yao namba moja ni Chadema kila mwana CCM anatema cheche kuimaliza CDM na DR.Slaa,patamu kweli hapo siasa inogile
 
Hivi ccm ni ya kijamaa?Au ni ya kibepari?Je ni chama cha wakulima au wafanyabiashara?Kwa sababu hawa watu siwaelewi kabisa,kama waliachana na sera ya ujamaa walichukua sera ipi?Kawa walia sera ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi je kimekuwa chama cha nani?Ccm ndo ina wabunge wengi,hivyo ndo inaunda serikali kama ccm haieleweki sera yake inamaana serikali nayo pia haieleweki hata watu wa nje ya nchi hawaijui Tanzania ni nchi ya aina gani,Nape ni katibu uenezi wa ccm,huyu mtu anaeneza nini?Watu wa ccm naombeni majibu
 
I got this for you. Itikadi ya ccm ni kutengeneza "Generational Ufisadi Opportunities for their ccm Families" Lengo kuu la ccm na hata mara moja hawakufikirii wewe Mtanzania.

IMG_0383.jpg


new+blood.jpg
 
Sera ya CCM ni "kudanganya". Udanganyifu, hila na ujanja ujanja.

Unafikiri natania?

...CCM ni chama cha Nyerere

Mwenye chama ameliona hilo.

Halmashami Kuu ya Taifa(ya CCM) iliketi Unguja ikabadili Azimio la Arusha bila kwanza kutafuta maoni ya wananchi. Na walikuwa na haki kufanya hivyo, maana sera ni yao. Ubaya wao ni kwamba jambo lenyewe walilifanya kwa hila na 'janja janja", na mpaka sasa wanaendelea kudanganya wananchi kwamba sera ya CCM bado ni Ujamaa na Kujitegemea. Uk 18

Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)
 
Hivi ccm ni ya kijamaa?Au ni ya kibepari?Je ni chama cha wakulima au wafanyabiashara?Kwa sababu hawa watu siwaelewi kabisa,kama waliachana na sera ya ujamaa walichukua sera ipi?Kawa walia sera ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi je kimekuwa chama cha nani?Ccm ndo ina wabunge wengi,hivyo ndo inaunda serikali kama ccm haieleweki sera yake inamaana serikali nayo pia haieleweki hata watu wa nje ya nchi hawaijui Tanzania ni nchi ya aina gani,Nape ni katibu uenezi wa ccm,huyu mtu anaeneza nini?Watu wa ccm naombeni majibu

Ibara ya 4(3) ya Katiba ya CCM inasema kuwa "Chama Cha Mapinduzi kinaamini kwamba Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru." Ibara ya 5(3) inasema "kwa hiyo Malengo na Madhumuni ya CCM yatakuwa" ni pamoja na "Kuhimiza ujenzi wa Ujamaa na Kujitegemea kwa mujibu wa Azimio la Arusha."
 
Ibara ya 4(3) ya Katiba ya CCM inasema kuwa "Chama Cha Mapinduzi kinaamini kwamba Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru." Ibara ya 5(3) inasema "kwa hiyo Malengo na Madhumuni ya CCM yatakuwa" ni pamoja na "Kuhimiza ujenzi wa Ujamaa na Kujitegemea kwa mujibu wa Azimio la Arusha."

Je huo ujamaa wa ccm upo wapi,je ujamaa unaruhusu watu kujirundikia mali kama walivyofanya Ridhiwan,Mkapa,Sumaye?Je ujamaa unaruhusu ufisadi kama wa dowans,richmond,epa,meremeta,kagoda,iptl..... akhhh kwanza nahisi hasira nikikumbuka hayo yote,ndugu hebu jaribu kuwa muungwana na nchi yako!!
 
Who benefited from Ujamaa na Kujitegemea zaidi ya familia za wahuni?
 
Je huo ujamaa wa ccm upo wapi,je ujamaa unaruhusu watu kujirundikia mali kama walivyofanya Ridhiwan,Mkapa,Sumaye?Je ujamaa unaruhusu ufisadi kama wa dowans,richmond,epa,meremeta,kagoda,iptl..... akhhh kwanza nahisi hasira nikikumbuka hayo yote,ndugu hebu jaribu kuwa muungwana na nchi yako!!

Mkuu uliuliza kama ccm ni ya kijamaa au kibepari? Mie nikupa kifungu cha katiba ya CCM. Hata kama CCM kingekuwa kinafuata siasa za kibepari haina maana kuwa kikumbatie ufisadi. Lakini hivi karibuni JK alisema kuwa Watanzania tunaogopa ubepari. fuatilia hii thread: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/129114-kikwete-adai-tatizo-ni-ujamaa.html
 
Nchi yetu kwa nje inavutia inatamanisha, kwani ina madini ya kutosha,mbuga za wanyama,maziwa makuu,mito mizuri,majumba ya kale nk,lakini kwa ndani inanuka inatoa harufu mbaya kwa sababu inatafunwa na mdudu anaeieanya inuke,mdudu huyo anaitwa CCM,mdudu huyu ameifanya nchi yetu kuwa kama gari moshi,haijulikani mbele wapi,haina dira wala uelekeo,wageni wanapoisikia tz wakiwa huko kwao hutaman kuja,wakifika wanaishia kushangaa,shime watz tumtoe huyu mdudu hatari asieijali nchi yetu!
 
Nchi yetu kwa nje inavutia inatamanisha, kwani ina madini ya kutosha,mbuga za wanyama,maziwa makuu,mito mizuri,majumba ya kale nk,lakini kwa ndani inanuka inatoa harufu mbaya kwa sababu inatafunwa na mdudu anaeifanya inuke,mdudu huyo anaitwa CCM,mdudu huyu ameifanya nchi yetu kuwa kama gari moshi,haijulikani mbele wapi,haina dira wala uelekeo,wageni wanapoisikia tz wakiwa huko kwao hutaman kuja,wakifika wanaishia kushangaa,shime watz tumtoe huyu mdudu hatari asieijali nchi yetu!
 
Wakuu wa CCM na wakereketwa wote, naomba mnisaidie mwenzenu namna itikadi ya UJAMAA NA KUJITEGEMEA inavyotekelezwa na chama na serikali hapa nchini sasa hivi ili niondoe mshangao wangu! Nakumbuka sana miaka ya nyuma kuanzia shule za msingi hadi sekondari itikadi hiyo ilitafsiliwa kwa vitendo kupitia kitu kilichoitwa "Education for self Reliance" au "Elimu ya Kujitegemea" shule zilikuwa na miradi chini ya mpango huo. Tulifundishwa kuipenda na kuiheshimu kazi. Tulifundishwa kilimo na ufugaji. Tulilelewa na kuamini kwamba kazi ni utu nani vibaya kuwa mzembe na mzururaji. Iweje leo watu bila aibu wasimame na kutangaza bila aibu kuwa wanaishi kimjinimjini? iweje watu wategemee bahati nasibu za makampuni ya simu kuwa ndio chanzo cha maisha bora na mafanikio? jirushe, chizika, kuwa mjanja,nufaika..... jee tunapotegemea wafadhiri kwenye kila kitu hata kujenga vyoo vya shimo ktk shule zetu ndio kujitegemea huko? Tunapo imba wimbo wawawekezaji kila siku bila kuimarisha sekta ya kilimo ambayo ndio muajiri mkubwa, ndio kujitegemea huko? Yanapo tolewa mamilioni ya JK kuimarisha tabaka au kundi la wachuuzi nchini ndio kujitegemea huko! Nielimisheni mwenzenu tafadharini.
 
Mukama alistaafu kwa heshima serikalini. Amekwenda kujichafua huko CCM wakati yeye sio mwanasiasa na chama chenyewe kimeoza nje ndani, kushoto kulia, nyuma na mbele!
 
Back
Top Bottom