maulaga
JF-Expert Member
- Feb 22, 2009
- 472
- 120
Nimestushwa na kushangazwa sana na kauri ya katibu mkuu mpya wa CCM bwana Wilson Mukama aliyoitoa akiwa Zanzibar akidai CCM ina itikadi ya ujamaa na kujitegemea na kutangaza ati CHADEMA hawana itikadi. Hivi kweli Mukama hajui kwamba itikadi ya ujamaa na kujitegemea iliuwawa hukohuko Zanzibar miaka ya 1990 kwakuliua Azimio la Arusha na kuruhusu ubepari wa kikasino kwa viongozi wa CCM kukusanya na kulimbikiza mtaji kwa njia yoyote ikiwemo ufisadi na kualika wawekezaji uchwara kutoka nje kuja kupora rasilimali zetu? Jamani, kumbe Makamba alikuwa bora kuliko hii takataka. Poleni sana wana CCM maana mmeletewa upupu utakao wawasha mpaka mfe.
SOURCE; Taarifa ya habari ITV saa mbili usiku (18.04.2011)
SOURCE; Taarifa ya habari ITV saa mbili usiku (18.04.2011)