Siasa za Mwalimu Nyerere za Ujamaa wa kujitegemea na itikadi yake ya Azimio la Arusha ndio chanzo cha umaskini wa Tanzania

Boi Manda

JF-Expert Member
Oct 26, 2023
381
497
Leo Oktoba 14, 2024 tunakumbuka kifo cha muasisi wa Tanzania Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyefariki siku na mwezi kama leo mwaka 1999 takribani miaka 25 sasa imepita

Baada ya Tanzania kupata uhuru wake mwaka 1961 Mwalimu Nyerere alipata kufanya ziara nchini Marekani (USA) alikutana na Rais wa 35 wa nchi hiyo John F. Kennedy maarufu kama JFK

Mwalimu alivutiwa sana na siasa za Marekani na aina ya uongozi wa Rais Kennedy na aliporejea nchini Tanzania akawa na mawazo ya kufuata siasa hizo za Marekani za ubepari.

Ikumbukwe kuwa Mwl. Nyerere baadaye akaja kuwa rafiki mkubwa na mpenzi wa uongozi na siasa za Kennedy na JFK naye akavutiwa na Nyerere wakawa maswahiba.

Haikuchukua muda mwaka 1963 Rais huyo wa USA akauawa kwa kudunguliwa na risasi na walenga shabaha. Mwalimu alihuzunishwa sana na kifo hicho akamlilia rafiki yake Kennedy.

Baada ya kifo cha Kennedy Mwalimu Nyerere alifanya ziara nchini China huko pia akavutiwa na siasa za nchi hiyo na uongozi wa Mao Zedong.

Mahaba ya mwalimu yakahamia kwenye siasa za "ukomonisti" akaona ndio siasa kistaarabu zenye kuleta umoja wa nchi na kuheshim utu wa mtu

Baadaye Mwalimu Nyerere akawashawishi wenziye na chama chake cha TANU na kuanzisha siasa zinazoendana na ukomonisti akaziita siasa za Tanzania ni siasa za ujamaa na kukitegemea

Hapo ikawa Mwalimu amebadilika kabisa kutoka kufikiria siasa za ubapari za rafiki yake Kennedy na kufuata siasa za Ujamaa

Mnamo mwaka 1967 Mwalimu akiongoza chama chake cha TANU wakakutana Arusha wakapitisha azimio la Arusha hapo ndipo nchi ilipoanza kuzama jahazi lake na kutopea kwenye umaskini wa kutupa mpaka sasa

Siasa za ujamaa na kujitegemea za Mwalimu Nyerere na itikadi ya Azimio la Arusha hazitaki utajiri wala watu kufanyabiashara kubwa na kupata utajiri na kujirimbikidhia utajiri

Ile sera yake ya binadamu wote ni sawa ndio walitaka hata kwenye kipato watu wote wawe sawa kusiwe na matajiri na maskini.

Hatuwezi kuendelea kwa sera hiyo ya Azimio la Arusha na siasa za kijamaa za aina hiyo za Mwalimu Nyerere

Kuthibitisha hilo miaka ya 80 mwalimu alimtuma waziri mkuu wake Edward Moringe Sokoine kuwakamata wafanyabiashara wote wakubwa na kuwaita majina mabaya "wahujumu uchumi"

Matokeo yake wafanyabiashara wakatiwa ndani wengine wakakimbia nchi na hao waliotiwa ndani walipoachiwa huru wakataifishiwa mali zao

Nchi za Magharibi na Mashirika ya fedha ya kimataifa IMF na Banki ya Dunia yakaiwekea vikwazo Tanzania na kunyimwa misaada hali ya kiuchumi ikazidi kuwa ngumu

Laiti kama Kennedy asingeuawa pengine Mwalimu Nyerere angefuata siasa za kiliberali za Magharibi ingekuwa Tanzania inamaendeleo makubwa ya kiviwanda kama jirani zao Kenya ambao tangu wapate uhuru wao siasa zao ni za kibepari

Baadaye Mwalimu Nyerere aliona siasa zake za ujamaa na kujitemea na itikadi yake ya Azimio la Arusha vimeshindwa kukwamua hali ya chumi wa Tanzania akaamuua kung'atuka na kuachia ngazi akampisha Rais Ally Hassan Mwinyi

Rais Mwinyi alipoingia madarakani haraka sana akatengua Pole pole siasa za ujamaa na kuingiza siasa za kibepari kuruhusu uwekezazi, ubinafishaji na ushiriki wa sekta binafsi kwenye kuchechemua uchumi wa nchi

Baadaye rais Mwinyi akapewa jina la mzee Ruksa akaenda mbali zaidi na kuanzisha Azimio la Zanzibar ambalo kimsingi limelifuta azimio la Arusha la Mwalimu Nyerere

Nisiwachoshe, Kesho nitaendelea kuwaletea siasa za Mwalimu zilivyogonga mwamba na kudidimiza uchumi wa nchi hii nitaendelea kuonyesha sehemu ambazo Mwalimu amefeli na sehemuambazo amefanikiwa

Comasa
 
🤣🤣🤣 bongo bna sjui tumelogwa na nan yaan mtu alisha fark bdo unasema amesababsha umaskn n iv bb yako amekuzaa umejielewa ukiaza maisha ya mafanikio utaangalia njia ya bb yako ya kzaman au utaendana na mfumo ambayo iliyopo kwa wakat uliopo?
Hii mifumo utaibadilisha bila wahusika kukubali? mfano tu matumizi ya hovyo misafara kuanzia DC kwenda juu na wizi wa mali za umma, wewe una mahakama ako?
 
Siasa za ujamaa na kujitegemea za Mwalimu Nyerere na itikadi ya Azimio la Arusha hazitaki utajiri wala watu kufanyabiashara kubwa na kupata utajiri na kujirimbikidhia utajiri
Sii kweli, China ni wajamaa na ni matajiri
le sera yake ya binadamu wote ni sawa ndio walitaka hata kwenye kipato watu wote wawe sawa kusiwe na matajiri na maskini.
Sii kweli, alitaka the gap between the haves
and the havenot iwe small.
Hatuwezi kuendelea kwa sera hiyo ya Azimio la Arusha na siasa za kijamaa za aina hiyo za Mwalimu Nyerere
Kulikuwa na mistake moja kubwa kwenye ujamaa wa Nyerere.
Kuthibitisha hilo miaka ya 80 mwalimu alimtuma waziri mkuu wake Edward Moringe Sokoine kuwakamata wafanyabiashara wote wakubwa na kuwaita majina mabaya "wahujumu uchumi"
Sii kweli, waliokamatwa ni wahujumu uchumi
Matokeo yake wafanyabiashara wakatiwa ndani wengine wakakimbia nchi na hao waliotiwa ndani walipoachiwa huru wakataifishiwa mali zao
Sii kweli bali ni baadhi
Nchi za Magharibi na Mashirika ya fedha ya kimataifa IMF na Banki ya Dunia yakaiwekea vikwazo Tanzania na kunyimwa misaada hali ya kiuchumi ikazidi kuwa ngumu
True
Laiti kama Kennedy asingeuawa pengine Mwalimu Nyerere angefuata siasa za kiliberali za Magharibi ingekuwa Tanzania inamaendeleo makubwa ya kiviwanda kama jirani zao Kenya ambao tangu wapate uhuru wao siasa zao ni za kibepari
Si kweli
Baadaye Mwalimu Nyerere aliona siasa zake za ujamaa na kujitemea na itikadi yake ya Azimio la Arusha vimeshindwa kukwamua hali ya chumi wa Tanzania akaamuua kung'atuka na kuachia ngazi akampisha Rais Ally Hassan Mwinyi
True
Rais Mwinyi alipoingia madarakani haraka sana akatengua Pole pole siasa za ujamaa na kuingiza siasa za kibepari kuruhusu uwekezazi, ubinafishaji na ushiriki wa sekta binafsi kwenye kuchechemua uchumi wa nchi
True
Baadaye rais Mwinyi akapewa jina la mzee Ruksa akaenda mbali zaidi na kuanzisha Azimio la Zanzibar ambalo kimsingi limelifuta azimio la Arusha la Mwalimu Nyerere
True
Nisiwachoshe, Kesho nitaendelea kuwaletea siasa za Mwalimu zilivyogonga mwamba na kudidimiza uchumi wa nchi hii nitaendelea kuonyesha sehemu ambazo Mwalimu amefeli
Sii kweli
na sehemuambazo amefanikiwa

Comasa
Asante
P
 
Kwani baada ya Mwinyi kufanya uchumi uwe huria, na kulifuta azimio la Arusha na kuweka azimio la Zanzibar Mbona bado hali ya uchumi ni mbaya.

Nyerere anahusikaje na hii hali ya uchumi wetu mkuu, na mambo yalibadilishwa na Mwinyi na pia aling’atuka zake bila hata kuchukua wala kufuja mali za umma?
 
Sii kweli, China ni wajamaa na ni matajiri

Sii kweli, alitaka the gap between the haves
and the havenot iwe small.

Kulikuwa na mistake moja kubwa kwenye ujamaa wa Nyerere.

Sii kweli, waliokamatwa ni wahujumu uchumi

Sii kweli bali ni baadhi

True

Si kweli

True

True

True

Sii kweli

Asante
P
Sio kweli ujamaa umeshindwa kuleta maendeleo duniani kote ulikokuwa unahubiriwa China wenyewe wameendelea baada ya kuweka siasa za kijamaa pembeni

Ujamaa China upo midomoni tu kwa watu lakini sera zake za kiuchumi na uzalishaji zinafuata mfumo wa kibepari

Ujamaa ulishindwa siku nyingi baada ya kusambaratika kwa Soviety Union (Urusi) Gorbachev aliingiza siasa zake za perestroika

Hakuna nchi inayofuata siasa ya kijamaa yenye maendeleo mazuri ya kiuchumi ni siasa ya hovyo
 
Kwani baada ya Mwinyi kufanya uchumi uwe huria, na kulifuta azimio la Arusha na kuweka azimio la Zanzibar Mbona bado hali ya uchumi ni mbaya.

Nyerere anahusikaje na hii hali ya uchumi wetu mkuu, na mambo yalibadilishwa na Mwinyi na pia aling’atuka zake bila hata kuchukua wala kufuja mali za umma?
Mwalimu aliweka misingi mipovu ya kiuchumi kutokana na siasa zake za kijamaa kibaya zaidi sera hizo na siasa hizo mpaka sasa viongozi wakuu waliomrithi wanaogopa kzibadilisha bado wanaugopa mzimu wq Nyerere
 
Sio kweli ujamaa umeshindwa kuleta maendeleo duniani kote ulikokuwa unahubiriwa China wenyewe wameendelea baada ya kuweka siasa za kijamaa pembeni

Ujamaa China upo midomoni tu kwa watu lakini sera zake za kiuchumi na uzalishaji zinafuata mfumo wa kibepari

Ujamaa ulishindwa siku nyingi baada ya kusambaratika kwa Soviety Union (Urusi) Gorbachev aliingiza siasa zake za perestroika

Hakuna nchi inayofuata siasa ya kijamaa yenye maendeleo mazuri ya kiuchumi ni siasa ya hovyo
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anatembea na vitabu viwili , Bible na Azimio la Arusha, tatizo ni utekelezaji tuu wa ujamaa wetu.
P
 
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anatembea na vitabu viwili , Bible na Azimio la Arusha, tatizo ni utekelezaji tuu wa ujamaa wetu.
P
Yeye (Mwalimu) ndiye rais aliyekaa madarakani kwa kipindi kirefu kuliko rais yoyote nchini alishindwaje ku Imorement ujamaa wake ma hilo Azimio lake la Arusha?

Matokei yake kaikimbia nchi ikiwa hoi bin taabani kiuchumu kabakia na kijitabu chake cha Azimio la Arusha mfukoni
 
Leo Oktoba 14, 2024 tunakumbuka kifo cha muasisi wa Tanzania Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyefariki siku na mwezi kama leo mwaka 1999 takribani miaka 25 sasa imepita

Baada ya Tanzania kupata uhuru wake mwaka 1961 Mwalimu Nyerere alipata kufanya ziara nchini Marekani (USA) alikutana na Rais wa 35 wa nchi hiyo John F. Kennedy maarufu kama JFK

Mwalimu alivutiwa sana na siasa za Marekani na aina ya uongozi wa Rais Kennedy na aliporejea nchini Tanzania akawa na mawazo ya kufuata siasa hizo za Marekani za ubepari.

Ikumbukwe kuwa Mwl. Nyerere baadaye akaja kuwa rafiki mkubwa na mpenzi wa uongozi na siasa za Kennedy na JFK naye akavutiwa na Nyerere wakawa maswahiba.

Haikuchukua muda mwaka 1963 Rais huyo wa USA akauawa kwa kudunguliwa na risasi na walenga shabaha. Mwalimu alihuzunishwa sana na kifo hicho akamlilia rafiki yake Kennedy.

Baada ya kifo cha Kennedy Mwalimu Nyerere alifanya ziara nchini China huko pia akavutiwa na siasa za nchi hiyo na uongozi wa Mao Zedong.

Mahaba ya mwalimu yakahamia kwenye siasa za "ukomonisti" akaona ndio siasa kistaarabu zenye kuleta umoja wa nchi na kuheshim utu wa mtu

Baadaye Mwalimu Nyerere akawashawishi wenziye na chama chake cha TANU na kuanzisha siasa zinazoendana na ukomonisti akaziita siasa za Tanzania ni siasa za ujamaa na kukitegemea

Hapo ikawa Mwalimu amebadilika kabisa kutoka kufikiria siasa za ubapari za rafiki yake Kennedy na kufuata siasa za Ujamaa

Mnamo mwaka 1967 Mwalimu akiongoza chama chake cha TANU wakakutana Arusha wakapitisha azimio la Arusha hapo ndipo nchi ilipoanza kuzama jahazi lake na kutopea kwenye umaskini wa kutupa mpaka sasa

Siasa za ujamaa na kujitegemea za Mwalimu Nyerere na itikadi ya Azimio la Arusha hazitaki utajiri wala watu kufanyabiashara kubwa na kupata utajiri na kujirimbikidhia utajiri

Ile sera yake ya binadamu wote ni sawa ndio walitaka hata kwenye kipato watu wote wawe sawa kusiwe na matajiri na maskini.

Hatuwezi kuendelea kwa sera hiyo ya Azimio la Arusha na siasa za kijamaa za aina hiyo za Mwalimu Nyerere

Kuthibitisha hilo miaka ya 80 mwalimu alimtuma waziri mkuu wake Edward Moringe Sokoine kuwakamata wafanyabiashara wote wakubwa na kuwaita majina mabaya "wahujumu uchumi"

Matokeo yake wafanyabiashara wakatiwa ndani wengine wakakimbia nchi na hao waliotiwa ndani walipoachiwa huru wakataifishiwa mali zao

Nchi za Magharibi na Mashirika ya fedha ya kimataifa IMF na Banki ya Dunia yakaiwekea vikwazo Tanzania na kunyimwa misaada hali ya kiuchumi ikazidi kuwa ngumu

Laiti kama Kennedy asingeuawa pengine Mwalimu Nyerere angefuata siasa za kiliberali za Magharibi ingekuwa Tanzania inamaendeleo makubwa ya kiviwanda kama jirani zao Kenya ambao tangu wapate uhuru wao siasa zao ni za kibepari

Baadaye Mwalimu Nyerere aliona siasa zake za ujamaa na kujitemea na itikadi yake ya Azimio la Arusha vimeshindwa kukwamua hali ya chumi wa Tanzania akaamuua kung'atuka na kuachia ngazi akampisha Rais Ally Hassan Mwinyi

Rais Mwinyi alipoingia madarakani haraka sana akatengua Pole pole siasa za ujamaa na kuingiza siasa za kibepari kuruhusu uwekezazi, ubinafishaji na ushiriki wa sekta binafsi kwenye kuchechemua uchumi wa nchi

Baadaye rais Mwinyi akapewa jina la mzee Ruksa akaenda mbali zaidi na kuanzisha Azimio la Zanzibar ambalo kimsingi limelifuta azimio la Arusha la Mwalimu Nyerere

Nisiwachoshe, Kesho nitaendelea kuwaletea siasa za Mwalimu zilivyogonga mwamba na kudidimiza uchumi wa nchi hii nitaendelea kuonyesha sehemu ambazo Mwalimu amefeli na sehemuambazo amefanikiwa

Comasa
Watu mnao andika mada kana hizi ..tuseme tu hamna akili hata kidogo nikikuuliza maswali lazima utashindwa kujibu hata moja ...tatizo lenu wengi mnadhani mkoloni alikuwa kaiacha tanzania kama nchi tena yenye muelekeo kumbe mgejua kuwa kutoka dar hadi kigoma au mwanza ilikuwa ni sawa na kutoka dar hadi nigeria kwa gari asilimia zaidi ya 90 ya watanzania walikuwa awajui chochote si kusoma wala kuandika ...swali je hadi Nyerere anaondoka madarakani ni nchi gani ya afrika isiyofuata siasa za ujamaa na kujitegemea iliyo kuwa tajiri hata hiyo saudi arabia na dubai kipindi hicho zilikuwa mavumbi matupu hata china ilikuwa masikini je china ilifuata siasa gani hadi kufikia maendeleo ? Mfano malawi ni nchi iliyo kuwa mtihifu kwa mabeberu je uchumi wake upoje je zaire uchumi wake upoje ...wengi mnaleta mada kwa kutumia akili zenu finyu mno ...wapo wapumbavu wanasema wakati wa nyerere tulivaa nguo za viraka nitsjie nchi za africa silizo kuwa nje ya siasa za ujamaa na kujitegemea ambazo walikuwa awavai viraka kwa kipindi kile ....kosa la Nyerere ni moja tu kuhusu ujamaa na ubepari...ukitaka kujua kosa la Nyerere lilipo lazima ujue na makosa ya marais walio mfuatia yalipo na kujua wapi tulipo kusea hadi sasa na kujua tunatakiwa kufanyeje ...ni lazima....

👉ujue kuna mifumo 4 ya ujamaa na ubepari nayo ni ....
1)SERIKALINI YA KIJAMAA NA UMMA WA KIJAMAA

2)SERIKALINI YA KIBEPARI NA UMMA WA KIBEPARI

3)SERIKALINI YA YA KIBEPARI NA UMMA WA KIJAMAA

4)SERIKALI YA KIJAMAA NA UMMA WA KIBEPARI.

Sasa hapo mfumo aliotumia Nyerere ni mfumo NO 1 hivyo nyerere alijikwamisha mwenyewe kwenye jitiada yake ya kuiletea nchi maendeleo kwa sababu ya huo mfumo NO 1.

Baada ya Nyerere kutoka madarakani akaja Mwinyi yeye akatumia mfumo NO2 ...marais walio tumia mfumo No2 ni MWINYI, KIKWETE, MKAPA, NA sasa SAMIA ...Mfumo huo No2 ni mbaya pia kwa kuwa unafanya Serikali kuwa kama mali binafsi au kampuni binafsi ya wahuni wachache dhidi ya wananchi walio wengi ..kikundi kidogo kinakuwa kinamiliki serikali kwa maslai yao na familia zao ....lakini Rais JPM alipo shika nchi alifanya jitiada ya kututoa kwenye huo mfumo na kutupeleka kwenye mfumo uliko sahihi kuliko yote nao ni mfumo NO 4 huu mfumo no 4 unafanya serikali kuwa mali ya uma kwa maslai ya uma na siyo kikundi kidogo pia unasimamia kwa haki ubebari wa sekta binafsi.....HIVYO UKIMSIKIA MTU ANA SEMA UJAMAA NDIYO BEST JUA HUYO NI MPUMBAVU NA UKIMSIKIA MTU ANASEMA UBEPARI NDIYO BEST JUA NA HUYO NI MPUMBAVU kwa maana Ujamaa na Ubepari vyote vinatakiwa kuwepo kwa pamoja ila katika mfumo ulio sahihi ambao ndiyo huo MFUMO NO 4 WA👉

💥💥💥4)SERIKALI YA YA KIJAMAA NA UMMA WA KIBEPARI 💥💥💥🐈‍⬛

Jifunzeni kwetu watu wenye akili siyo hao magreat thinker uchwara wasio weza kupambanua mambo 🤫
 
Huko kwenye Azimio la 1977 ni mbali sana, alituingiza kwenye umaskini mwaka mmoja tu baada ya kupata Uhuru alipofuta Vyama vya Upinzani.

Alitaka kuiendesha nchi kwa mawazo ya mlengo mmoja bila kushauriana au kukosolewa na mtu ndo maana wote waliokuwa wakimkosoa au aliowahofia watamsumbua waliondolewa nje ya mfumo.. Yaani huu mfumo wa CHAMA TAWALA sasa yeye ndo aliutengeneza..

Kwahiyo wale mnaomsifu kwa kushinikiza mwaka 1992 turudie mfumo wa Vyama Vingi hawajui wanachosema au ni Wanafki...
 
Yeye (Mwalimu) ndiye rais aliyekaa madarakani kwa kipindi kirefu kuliko rais yoyote nchini alishindwaje ku Imorement ujamaa wake ma hilo Azimio lake la Arusha?

Matokei yake kaikimbia nchi ikiwa hoi bin taabani kiuchumu kabakia na kijitabu chake cha Azimio la Arusha mfukoni
We jamaa unachuki binafsi Na Nyerere, kwani Mo na Bakhresa sio watanzania?

We tafuta hela Acha lawama.
Nyerere Hausiki kwenye shida zako, yani we ushindwe kujitengeneza kimaisha umlaumu Nyerere.
Hakuna nchi isoyo na maskini, wajinga wala wagonjwa duniani, kila mtu anapambania maisha yake wala hakuna mtu wa kulaumiwa mkuu.

Baba ako akikizaa katika unaskini na akikulea katika umasikini na ukikua Ukiacha kutafuta maisha na kujitoa katika umaskini ukiishia kumlaumu yeye kama sababu ya umaskini wako je utakuwa na akili timamu?.
 
Back
Top Bottom