MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Kwa yakini ya moyo wangu kabisa, leo nilipokua nikitazama sherehe za kuwatunuku nishani wapiganaji wetu wa JWTZ Arusha nimeshuhudia baadhi ya mambo ya ajabu yaliyofanyika ndani ya uwanja na nasema yaweza kua ni historia yangu ya kwanza na ya kustaabisha maishani mwangu.Hakika najaribu kupiga picha ya huko tunakoelekea taswira nimeikosa kabisa, tunakoelekea si kuzuri nadhani.
Nadhani CCM kama chama tawala mnayo kila sababu ya kutumia busara tu ya kukutana na mwenyekiti wenu wa taifa kumwomba walao itoshe tu kuongoza taifa kwa kipindi cha miaka mitano,emeshatenda mengi na makubwa mno,hayo yote yanatosha kumiminia sifa za kutosha, itoshe kufanya hivyo kwani kunaweza pengine kuwajengea sheshima na historia nzuri zaid.
Kitendo cha mh Rais kukiri hadharani kabisa kwa kinywa chake kua hakua na nia ya kugombea Urais ispokua alisukuiziwa tu, nadhani hii itawafanya watanzania walio wengi kuanza kuingiwa na hofu juu ya Dhamira yake ya kuwakomboa mahali walipo, kwa tafsiri ya haraka haraka ni kwamba ni uongozi alioupata mimi bila kutegemea ndio maana amekiri kua ni kazi ngumu.
Kitu kiingine ambacho kimenishtua mimi ni kugeuza sherehe iliyokua imeandaliwa kwa ajili ya kuwatunuku nishani wapiganaji wetu na kuifanya kua ya kupokea wanachama wanachama vyama viingine na kujiunga na CCM,hiki si kitu cha kawaida kushudia kwangu mimi!Matendo haya kikatiba ni kosa kubwa sana, haya mambo hufanyika kwenye shughuli za kichama na sio shughuli za kiserikali, hivi CCM hamjui nini?
Kitendo kiingine ambacho nimeshuhudia live kabisa bila kupepesa macho ni kusema kua wakati anaingia madarakani kilo moja ya sukari ilikua ikiuzwa kwa shillingi 5000 na sasa imeshuka na itaendelea kuchukua zaidi. Jamani, hiyo bei mbona mimi sijawahi kuisikia wala kuiona ndio nimeisikia leo? Hiyo bei binafsi sina kumbukumbu kama imeshawahi kufika huko popote nchini.
Napata hofu kubwa kabisa kwamba nilihisi huenda ugumu wa maisha unaopaa hivi sasa ni kwa bahati mbaya au ni kipindi cha mpit ttu napata hofu kua huenda ikawa ndio hali halisi wala sio mpito. Huenda tumefikia huku kwa sababu tu ya kukosekama kwa mbinu na mikakati madhubuti ya kuendesha uchumi wa taifa letu. Kwa haya niliyoyashuhudia leo Arusha tena kwa bahati nzuri nimeshuhudia kwa macho yangu, kwa mambo hayo yote kwanini tusihofngumu na ndivyo iwavyo kwenye hali halisi ya maisha yetu jamani?
Kwanini wenzangu ndani ya CCM wasijitokeze baadhi ya wenzenu wakapeleka pendekezo la kumuomba chairman walao aongoze kwa kipindi kimoja tuu? Bado tuna imani kua wapo watanzania wengine wenye nia njema kama yake na wataendelea kulisukuma gurudumu. Kwasababu hata kama akiendelea hadi muhula wa pili bado itakua ndio mwisho wa uongozi wake na hatomaliza mambo yote maana bado kua wengine wakuja wataendeleza alikoishia,hivyo ni bora kwa sababu ameshasema mapema kua kazi ile ni ngumu mzee wetu apumzike akiwa bado angali ana nguvu za kutosha.
Ni maoni yangu Hutu!!
Nadhani CCM kama chama tawala mnayo kila sababu ya kutumia busara tu ya kukutana na mwenyekiti wenu wa taifa kumwomba walao itoshe tu kuongoza taifa kwa kipindi cha miaka mitano,emeshatenda mengi na makubwa mno,hayo yote yanatosha kumiminia sifa za kutosha, itoshe kufanya hivyo kwani kunaweza pengine kuwajengea sheshima na historia nzuri zaid.
Kitendo cha mh Rais kukiri hadharani kabisa kwa kinywa chake kua hakua na nia ya kugombea Urais ispokua alisukuiziwa tu, nadhani hii itawafanya watanzania walio wengi kuanza kuingiwa na hofu juu ya Dhamira yake ya kuwakomboa mahali walipo, kwa tafsiri ya haraka haraka ni kwamba ni uongozi alioupata mimi bila kutegemea ndio maana amekiri kua ni kazi ngumu.
Kitu kiingine ambacho kimenishtua mimi ni kugeuza sherehe iliyokua imeandaliwa kwa ajili ya kuwatunuku nishani wapiganaji wetu na kuifanya kua ya kupokea wanachama wanachama vyama viingine na kujiunga na CCM,hiki si kitu cha kawaida kushudia kwangu mimi!Matendo haya kikatiba ni kosa kubwa sana, haya mambo hufanyika kwenye shughuli za kichama na sio shughuli za kiserikali, hivi CCM hamjui nini?
Kitendo kiingine ambacho nimeshuhudia live kabisa bila kupepesa macho ni kusema kua wakati anaingia madarakani kilo moja ya sukari ilikua ikiuzwa kwa shillingi 5000 na sasa imeshuka na itaendelea kuchukua zaidi. Jamani, hiyo bei mbona mimi sijawahi kuisikia wala kuiona ndio nimeisikia leo? Hiyo bei binafsi sina kumbukumbu kama imeshawahi kufika huko popote nchini.
Napata hofu kubwa kabisa kwamba nilihisi huenda ugumu wa maisha unaopaa hivi sasa ni kwa bahati mbaya au ni kipindi cha mpit ttu napata hofu kua huenda ikawa ndio hali halisi wala sio mpito. Huenda tumefikia huku kwa sababu tu ya kukosekama kwa mbinu na mikakati madhubuti ya kuendesha uchumi wa taifa letu. Kwa haya niliyoyashuhudia leo Arusha tena kwa bahati nzuri nimeshuhudia kwa macho yangu, kwa mambo hayo yote kwanini tusihofngumu na ndivyo iwavyo kwenye hali halisi ya maisha yetu jamani?
Kwanini wenzangu ndani ya CCM wasijitokeze baadhi ya wenzenu wakapeleka pendekezo la kumuomba chairman walao aongoze kwa kipindi kimoja tuu? Bado tuna imani kua wapo watanzania wengine wenye nia njema kama yake na wataendelea kulisukuma gurudumu. Kwasababu hata kama akiendelea hadi muhula wa pili bado itakua ndio mwisho wa uongozi wake na hatomaliza mambo yote maana bado kua wengine wakuja wataendeleza alikoishia,hivyo ni bora kwa sababu ameshasema mapema kua kazi ile ni ngumu mzee wetu apumzike akiwa bado angali ana nguvu za kutosha.
Ni maoni yangu Hutu!!