CCM mnachanja mbuga kwenda kichakani

CCM mnachanja mbuga kwenda kichakani

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,446
Reaction score
829,812
Mada yangu moja ya mwezi May ilizungumzia hofu ya CCM juu ya UKAWA na Lowassa kwamba yeyote atakayeshika madaraka itakuwa ni kiama kwao.

Mwelekeo ulikuwa dhahiri kuwa mgombea na hatimaye rais atakuwa Lowassa kwa upande wa CCM huku UKAWA wakichukua viti vingi sana vya Ubunge Udiwani nk. Hapa ingetengenezwa colabo nzuri sana kwakuwa kuna mfanano na kushabihiana fulani kati ya Lowassa na UKAWA.

Hii imeendelea kuwa hofu kwa kundi la CCM maslahi, wameangalia mbele wakaona wazi nini kitatokea iwapo wawili hao wataukamata uongozi wa nchi.

Fitina ikatengenezwa na 'KITENGO' kwanza kumpiga chini Lowassa kwa namna yoyote ile kisha kufitinisha upinzani wafarakane ili nguvu ipungue.

Wamefanikiwa kwa Lowassa japo kwa sasa, wanaweza kufanikiwa upinzani japo kwasasa lakini mwendo wao huu hauwapeleki barabara iliyonyooka bali wanachanja mbuga kuingia chaka wasilolijua.

Lowassa ana nguvu ana haiba ya uongozi, ana rasilmali watu ya kutosha, upinzani nao hivyohivyo, kutaka kuyadhoofisha na hatimaye kuyauwa kabisa haya makundi mawili na ukabaki salama sio kitu cha mchezomchezo tu...kuna kubwa tena baya kabisa litatokea.

Lowassaa yuko kimya kwasasa, sio mpuuzi na si kama kashindwa mapambano anajipanga, anatafakari anajiweka vizuri ana kundi kubwa mno linalosubiri kauli yake atakachosema ndicho watakachotenda liwe baya liwe zuri.

Upinzani nao sio wa kudharau kuna kundi kubwa sana la wananchi waliochoshwa na CCM wana imani kubwa na upinzani, wanataka mabadiliko hawako tayari tena kuona CCM inarudi madarakani wamewekeza nguvu na rasilmali zao pale, CCM wasione hiii ni segere la yamoto bendi.

Hicho 'KITENGO' Kiache ujuha kitaiangamiza nchi kwa ajili ya kulinda maslahi ya wachache ambo hata hivyo hawajai yutong tano....! Huu ni mustakabali wa taifa wafanye upuuzi wao lakini amani na ustawi wa Taifa visiathirike .

Pesa waliyowekeza kufitinisha upinzani ni wendawazimu mtupu mabadiliko yanapofika hakuna wa kuyazuia hata awe nani yaliyotokea mashariki ya kati na kwingineko Afrika hayashindwi kutokea hapa.

Tutafakari.
 
Mkuu mimi binafsi nilikuwa team Lowasa!

Lkn siwezi nikawa na mapenzi kwa mtu kupitiliza!

Kwasababu CCM haikumpitisha Lowasa, sina sababu ya kutokumsapoti Magufuli!

Na ni team Lowasa wengi tu wenye msimamo kama wangu!

Kamwe Lowasa hawezi kunishawishi niwapigie kura Ukawa hata yeye akijiunga nao!

CCM bado ni imara sana na pia yanayotokea ukawa asaivi ni madhaifu yao wenyewe na CCM has nothing to do with them!!
 
Sasa mkuu hao watu wanaominywa si waungane, maana unasema wote wana nguvu na wanapendwa. . . . .ugumu uko wapi??!!!

Bati inapovuja badala ya kusogeza kitanda we unalaumu bati. . . . .Inasaidia nini??!!!
 
Sasa mkuu hao watu wanaominywa si waungane, maana unasema wote wana nguvu na wanapendwa. . . . .ugumu uko wapi??!!!

Bati inapovuja badala ya kusogeza kitanda we unalaumu bati. . . . .Inasaidia nini??!!!
OLESAIDIMU hivi vitu si vya kukurupuka
 
Last edited by a moderator:
Nakubaliana na wewe ndugu,hata huku niliko watu wanasubiri tamko lake tu na wanasononeka sana na ukimya wa Lowassa. Siku Magufuri anatangazwa baadhi walikubaliana na matokeo lakini baada ya siku mbili watu wamebadiri msimamo na kuanza kuhofia mfumo uliopo CCM (SI MAGUFURI, HAWANA TATIZO NA MAGUFURI), wanasema haijawahi kutokea Watanzania walivyoweka imani kwa Kikwete na kumpa ushindi mkubwa,leo hii ni majuto ambayo wanaamini hata Magufuri atapita humo humo hivyo lao ni kuiweka pembeni CCM na Magufuri wao. Niko Geita Nyakumbu.
 
Kapige mswaki kwanza.... Maneno yanaonekana mdomo sio mfasi.... Unawaza kama kingunge ww
 
Nakubaliana na wewe ndugu,hata huku niliko watu wanasubiri tamko lake tu na wanasononeka sana na ukimya wa Lowassa. Siku Magufuri anatangazwa baadhi walikubaliana na matokeo lakini baada ya siku mbili watu wamebadiri msimamo na kuanza kuhofia mfumo uliopo CCM (SI MAGUFURI, HAWANA TATIZO NA MAGUFURI), wanasema haijawahi kutokea Watanzania walivyoweka imani kwa Kikwete na kumpa ushindi mkubwa,leo hii ni majuto ambayo wanaamini hata Magufuri atapita humo humo hivyo lao ni kuiweka pembeni CCM na Magufuri wao. Niko Geita Nyakumbu.
Imekula kwenu!!!
Magufuli is the president of United Republic of Tanzania for 2015 - 2025!
 
Imekula kwenu!!!
Magufuli is the president of United Republic of Tanzania for 2015 - 2025!

Akipita Magufuri au asipopita atanisaidia nini? Huyu ni waziri wa ujenzi lakini alielekeza nguvu kwake Chato huku akitaka hata makao makuu ya mkoa wa Geita yawe Chato hadi akajenga na maofisi ya wizara mbali mbali hadi Pinda akabatirisha.

Fika Nyakumbu kuja Bukoli hadi Kakola mgodini then uelekee Kahama uone sehemu ambayo imezugukwa migodi (Geita-GEITA GOLD MINE GGM, KAKOLA-BULYANHULU GOLD MINE NA KAHAMA BUZWAGI GOLD MINE) au tuite "Triangle Gold mine areas" lakini hakuna hata barabara ya lami.

Ukifika Kakola unaweza tokwa machozi kwa huruma ya vumbi linalotimka barabarani huku dhahabu kila siku ikibebwa pasipo hata huduma ya maji ya kunywa ambayo maji ya ziwa Victoria yameishia mgodini kwa akili ya kupunguza vumbi mgodini,kupozea mitambo na kuoshea dhahabu.

Je Magufuri hakufahamu hili na kukimbilia kuweka hadi taa za usalama barabarani Chato huku magari hapo Chato hayazidi hata 15!! Tulikuwa CCM kwa sababu ya mtu imara na mwenye huruma kama Lowassa.

Alipambana kuleta maji Kahama na Shinyanga wakati yeye yuko Monduli Umasaini. Magufuri hana uwezo wa kuongoza isipokuwa ni mtendaji mzuri na asiyechoka bila kusahau na majigambo yake huku nikikukumbusha mwaka huu alikuwa hapiti ubunge na ashukuru kwa mbeleko ya makundi ya Lowassa na Membe.
 
mshana Jnr,umeeleza ukweli lakini wengi watakubeza.Lakini kwa uhakika hizo pesa wangenunua madawati au dawa za mahospitali.

Lakini ninachokiona wengi wa wanaCCM hawajui maana ya upinzani wanaona UPINZANI ni uadui,wengi wa wanachama wa CCM hata UTAIFA umewatoka kabisa,wanakumbatia wizi na rushwa imeonekana ni haki.

Sijui tunakoelekea na dhana hii ya pesa kununua madaraka.Watanzania bila kujali itikadi zetu ilibidi tujiulize kwanini watu watumie pesa nyingi kugombea madaraka.

Ninajiuliza kwanini CCM itenge hizo milioni kuwalipa vifungu vya wachache waliopo upinzani ili kuusambaratisha upinzani,kama ni kweli basi ningependa kujua sababu zake.Na kwanini wanaolipwa hizo pesa wasijiulize kwanini wananunuliwa?
 
Umezunguuuuka kumbe lengo ni kuonyesha Lowasa aonekane hajatendewa haki. Ye si ana rasilimali watu basi aanzishe Chama chake au unavyosema nchi itayumba Ina maana Bila Ccm nchi hii haiwez kwenda? Acha mawazo ya kikoloni hayo
 
Hivi mkuu ilikuwa ni Lowassa tu ndio apitishwe kugombea urais na ccm?? Unataka kuniambia Lowassa ni msafi sana kupita Magufuli??

Tuongee ukweli na tuache unafiki, hivi kati ya Lowassa na Magufuli nani ni mtendaji mzuri?

Kati ya hawa wawili nani ni Fisadi??? Utaniambia hakuna binadamu mkamilifu, lakini tuache unafiki, kati ya hawa wawili ni nani basi mwenye nafuu?

Tuache siasa, tuache upambe, Magufuli ananafuu zaidi ya Lowassa mara elfu.

Mimi niliwaambia marafiki zangu, binafsi mimi sio mwana "CCM", lakini kwa kitendo cha CCM kumpitisha Magufuli, kura yangu ya urais itaenda kwa Magufuli.

Utendaji wa Magufuli ni zaidi hata ya utendaji wa Kikwete mara milioni moja!

Tukumbuke huu msemo "jasiri haachi asili" Magufuli hawezi kubadilika, Magufuli atakuwa moto wa kuotea mbali. Tusubiri tuone, Time will tell.
 
Cock n bull story. Nawe mtazamo wako umekuwa hauna tofaut na huyu mzee Kingunge. Ccm itaendelea kuwepo coz Magufuli nae ana rasilimali watu tena wale wapigaji kura ambao wanaiangalia siasa katika mtazamo wenye mashiko. Tuna imani na Magufuli, hopin atasimama kama inavyotakiwa.
 
Mkuu mimi binafsi nilikuwa team Lowasa!

Lkn siwezi nikawa na mapenzi kwa mtu kupitiliza!

Kwasababu CCM haikumpitisha Lowasa, sina sababu ya kutokumsapoti Magufuli!

Na ni team Lowasa wengi tu wenye msimamo kama wangu!

Kamwe Lowasa hawezi kunishawishi niwapigie kura Ukawa hata yeye akijiunga nao!

CCM bado ni imara sana na pia yanayotokea ukawa asaivi ni madhaifu yao wenyewe na CCM has nothing to do with them!!
Mkuu,
Ni kweli taratibu zilikiukwa na KITENGO kikachagua tano bora badala ya CC?
If so, demokrasia ipo wapi ndani ya chama na ikizingatiwa kwamba Nape alitangaza kwamba hakuna nafasi ya kukata rufaa?
 
mshana Jnr,umeeleza ukweli lakini wengi watakubeza.Lakini kwa uhakika hizo pesa wangenunua madawati au dawa za mahospitali.

Lakini ninachokiona wengi wa wanaCCM hawajui maana ya upinzani wanaona UPINZANI ni uadui,wengi wa wanachama wa CCM hata UTAIFA umewatoka kabisa,wanakumbatia wizi na rushwa imeonekana ni haki.

Sijui tunakoelekea na dhana hii ya pesa kununua madaraka.Watanzania bila kujali itikadi zetu ilibidi tujiulize kwanini watu watumie pesa nyingi kugombea madaraka.

Ninajiuliza kwanini CCM itenge hizo milioni kuwalipa vifungu vya wachache waliopo upinzani ili kuusambaratisha upinzani,kama ni kweli basi ningependa kujua sababu zake.Na kwanini wanaolipwa hizo pesa wasijiulize kwanini wananunuliwa?
Ni jambo la ajabu kwamba maCCm hawahawa wanamwita Lowassa fisadi ndio hawahawa walimuita gamba lakini bado ni mwanachama wao..........Hivi Fisi anaweza kukaa na Kondoo kweli? Mbona hawawezi kumfukuza fisadi?

Wote ni mafisi au wote ni kondoo au wote ni Kambale......
Lowassa afanye maamuzi magumu sasa tuone kama CCM itabaki salama, aache kumbwelambwela!
 
Kapige mswaki kwanza.... Maneno yanaonekana mdomo sio mfasi.... Unawaza kama kingunge ww

Michango mingi hapa itategemea nani ana mtazamo gani kwenye nini na ni wa kundi la nani, hayo pengine ni matusi ya kawaida sana yapo muhimu tujadili hoja iliyopo mezani
 
Ni jambo la ajabu kwamba maCCm hawahawa wanamwita Lowassa fisadi ndio hawahawa walimuita gamba lakini bado ni mwanachama wao..........Hivi Fisi anaweza kukaa na Kondoo kweli? Mbona hawawezi kumfukuza fisadi?

Wote ni mafisi au wote ni kondoo au wote ni Kambale......
Lowassa afanye maamuzi magumu sasa tuone kama CCM itabaki salama, aache kumbwelambwela!

Bigirita,alikosea toka mwanzo ,angeachia mapema impact yake ingekuwa kubwa ,na si kuhama chama kususia tu ule mkutano mkuu lazima wengine wangeondoka naye na pale ndipo ngoma ilipoishia,kwa sasa anacheza ngoma ya mwenyekigoda.

Pili anajua hatari itakayomfika pindi akiondoka sasa,kukaa kwake kimya ni dawa zaidi kuliko kuongea.Maana hata mwenyekigoda anatamani ajue nini akifikiriacho.

Kwa uhakika Lowassa hawezi kuhama CCM ,sababu ndiko kuliko mlea,ndiko kwenye madogoli yao (yeye na wenzake) wanajuana siri zao wote,yeye ni mshindwa zaidi kuliko aliye madarakani sasa.Wote waliokwenye uongozi CCM kwa sasa wanacheza ngoma ya mwenyekigoda.

Kuna wale waliomback Lowassa hawa wanahatari ya kwenda na maji ndiyo maana kwa sasa Mzee hana marafiki tena,wamemuacha,yuko peke yake akiliwazwa na familia yake.Ameshapoteza vingi,pesa,ubinadamu (UTU) wake,SIFA yake,uungwana wake,marafiki zake ndiyo maana move yoyote atakayochukua lazima awe makini vinginevyo maisha yake yataondoka kama mshumaa uwakao............
 
Michango mingi hapa itategemea nani ana mtazamo gani kwenye nini na ni wa kundi la nani, hayo pengine ni matusi ya kawaida sana yapo muhimu tujadili hoja iliyopo mezani

Hana HOJA ndiyo maana kaja na KIHOJA..........
 
Bigirita,alikosea toka mwanzo ,angeachia mapema impact yake ingekuwa kubwa ,na si kuhama chama kususia tu ule mkutano mkuu lazima wengine wangeondoka naye na pale ndipo ngoma ilipoishia,kwa sasa anacheza ngoma ya mwenyekigoda.

Pili anajua hatari itakayomfika pindi akiondoka sasa,kukaa kwake kimya ni dawa zaidi kuliko kuongea.Maana hata mwenyekigoda anatamani ajue nini akifikiriacho.

Kwa uhakika Lowassa hawezi kuhama CCM ,sababu ndiko kuliko mlea,ndiko kwenye madogoli yao (yeye na wenzake) wanajuana siri zao wote,yeye ni mshindwa zaidi kuliko aliye madarakani sasa.Wote waliokwenye uongozi CCM kwa sasa wanacheza ngoma ya mwenyekigoda.

Kuna wale waliomback Lowassa hawa wanahatari ya kwenda na maji ndiyo maana kwa sasa Mzee hana marafiki tena,wamemuacha,yuko peke yake akiliwazwa na familia yake.Ameshapoteza vingi,pesa,ubinadamu (UTU) wake,SIFA yake,uungwana wake,marafiki zake ndiyo maana move yoyote atakayochukua lazima awe makini vinginevyo maisha yake yataondoka kama mshumaa uwakao............
Nakubaliana nawe kwamba ameshindwa kufanya TIMING.....lakini nyuma ya pazia yapo mengi yanayoendelea. Hata ujasiri wa Kingunge kusema hadharani kwamba CC haijachagua tano bora bali imetoka/kulazimishwa na KITENGO ni muendelezo wa kumomonyoka.

Lowassa anaweza asitoke CCM, lakini watu wake wachace wanaweza kutoka. Ninaamini ana watu wanaomuamini sana, na wapo wanaompenda kwasababu ya fedha alizonazo (wanapata chenji kidogo).

Kumbuka pia kwamba hawezi kutoka bila mazungumzo na sehemu anayotaka kwenda....yeye hataki kuhama chama akawe mwanachama wa kawaida. Hii ni swala la kulifikiri sana.
 
Nakubaliana nawe kwamba ameshindwa kufanya TIMING.....lakini nyuma ya pazia yapo mengi yanayoendelea. Hata ujasiri wa Kingunge kusema hadharani kwamba CC haijachagua tano bora bali imetoka/kulazimishwa na KITENGO ni muendelezo wa kumomonyoka.

Lowassa anaweza asitoke CCM, lakini watu wake wachace wanaweza kutoka. Ninaamini ana watu wanaomuamini sana, na wapo wanaompenda kwasababu ya fedha alizonazo (wanapata chenji kidogo).

Kumbuka pia kwamba hawezi kutoka bila mazungumzo na sehemu anayotaka kwenda....yeye hataki kuhama chama akawe mwanachama wa kawaida. Hii ni swala la kulifikiri sana.

Kuna mengi sana yatatokea kati ya mwezi huu na October, na yanaweza kuchagizwa zaidi na kauli zozote atakazotoa LOWASSA
 
Back
Top Bottom