GE2025 CCM mlione hili na kulitolea uamuzi wa busara, Mchakato wa kuchuja watia nia Ubunge na Udiwani

GE2025 CCM mlione hili na kulitolea uamuzi wa busara, Mchakato wa kuchuja watia nia Ubunge na Udiwani

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
1,289
Reaction score
2,190
Wananchama wengi wa CCM wametia nia ya kugombea nafasi za Udiwani na Ubunge. Moja ya sharti lililowekwa na CCM ni kuwa watia nia wote kwa nafasi za Udiwani na Ubunge kwanza watachujwa na Kamati za Wilaya na Mikoa na hatimaye majina yote kupelekwa Makao Makuu ya CCM - Dodoma kila mmoja akipewa alama na Kamati za Wilaya na Mikoa.

Utaratibu huu ni mzuri lakini kwangu siyo nzuri kwa sababu zifuatazo:-
(1) Utaratibu huu unachochea upendeleo kwa wachache ambao watapata upendeleo kutoka kwenye Kamati za Wilaya na Mikoa na hata Taifa.
(2) Utaratibu huu unachochea RUSHWA . Kwa wale wanaotaka kupitishwa majina yao wanapitisha rushwa kwa Kamati za Wilaya na Mikoa na hata Taifa.
(3) Utaratibu huu unaleta uonevu. Kwa yule mgombea ambaye hana ndugu kwenye Kamati zilizotajwa ataonewa pasipo sababu.

USHAURI WANGU. Ninashauri kuwa wale wote waliotia nia ya kugombea Udiwani na Ubunge majina yao yarudishwe yote kwa wajumbe ili wapigiwe kura ili mshindi/washindi wapatikane kwa njia ya haki bila upendeleo. Kurudisha majina matatu ili waje wapigiwe kura na wajumbe kutaleta manung'uniko makubwa na upendeleo kitu ambacho kinaweza kuchafua Chama chetu.

Nawasilisha.
 
Wananchama wengi wa CCM wametia nia ya kugombea nafasi za Udiwani na Ubunge. Moja ya sharti lililowekwa na CCM ni kuwa watia nia wote kwa nafasi za Udiwani na Ubunge kwanza watachujwa na Kamati za Wilaya na Mikoa na hatimaye majina yote kupelekwa Makao Makuu ya CCM - Dodoma kila mmoja akipewa alama na Kamati za Wilaya na Mikoa.

Utaratibu huu ni mzuri lakini kwangu siyo nzuri kwa sababu zifuatazo:-
(1) Utaratibu huu unachochea upendeleo kwa wachache ambao watapata upendeleo kutoka kwenye Kamati za Wilaya na Mikoa na hata Taifa.
(2) Utaratibu huu unachochea RUSHWA . Kwa wale wanaotaka kupitishwa majina yao wanapitisha rushwa kwa Kamati za Wilaya na Mikoa na hata Taifa.
(3) Utaratibu huu unaleta uonevu. Kwa yule mgombea ambaye hana ndugu kwenye Kamati zilizotajwa ataonewa pasipo sababu.

USHAURI WANGU. Ninashauri kuwa wale wote waliotia nia ya kugombea Udiwani na Ubunge majina yao yarudishwe yote kwa wajumbe ili wapigiwe kura ili mshindi/washindi wapatikane kwa njia ya haki bila upendeleo. Kurudisha majina matatu ili waje wapigiwe kura na wajumbe kutaleta manung'uniko makubwa na upendeleo kitu ambacho kinaweza kuchafua Chama chetu.

Nawasilisha.
NRNE
 
Siasa za nchi ni ajabu sana.

Yaani CHADEMA wameacha ajenda zao na sasa wanapigania mabadiliko ndani vyama vingine.

CHADEMA sasa rasmi kwenye mfumo
 
Siasa za nchi ni ajabu sana.

Yaani CHADEMA wameacha ajenda zao na sasa wanapigania mabadiliko ndani vyama vingine.

CHADEMA sasa rasmi kwenye mfumo
Mimi naona ccm ndio wamejaa kwenye mifumo ya Chadema ya kudai Reform na kukemea utekaji 🤔
 
Back
Top Bottom