CCM mchezo mnaoufanya ni hatari

CCM mchezo mnaoufanya ni hatari

  1. Kila mtu anafahamu wazi kwamba mchezo mnaoufanya mlishaupanga kitambo na sasa mmeanza kuutekeleza kwa awamu Kutumia dola ISIYOJITAMBUA kubambikiza kesi kwa viongozi wa upinzani hasa CHADEMA.
  2. Mnajua wazi kwamba hampo tena kwenye mioyo ya Watanzania na hivyo mmeamua kutumia nguvu kujithibitishia kuitawala nchi hata kama mkishindwa kupitia sanduku la kura kama ilivyowatukia 2010.
  3. Mmeshiindwa kudhibiti mfumuko wa bei kiasi kwamba mlipoamua kupandisha nauli za vyombo vya usafiri mkatafuta kigezo kwa kupandisha bei ya mafuta usiku usiku ili iendane na ongezeko la nauli, na inajulikana wazi kwamba mnawategemea wafanyabiashara wawabebe kugharimia 2015 baada ya mipango yenu ya kuiba kuanza kugundulika mianya kuzibwa kila kona.
  4. Mnaelewa fika kwamba upinzani una nafasi kubwa ya kuchukua hatamu za uongozi kuanzia 2015 na sasa mmeamua kutumia kampeni za udini kwa vitendo kuwagawanya Watanzania ili nchi isitawalike na muweze kuendelea kuwepo madarakani kwa kigezo cha vurugu za kidini.
  5. Viongozi wenu wa juu wameridhia uteswaji, udhalilishwaji na hata kunyofolewa uhai kwa yeyote ambaye anaonekana ni kikwazo kwa chama na hususani anayewaamsha raia kujitambua.

Hii ni hatari kwenu maana kama hatutawaswaga ninyi kwenye mahakama za uhalifu basi wajukuu zenu watasimama kwa niaba.

Usalama wa Taifa utawajibika kikamilifu kwa uvunjifu wa amani na utulivu unaotokea na utakaojitokeza.
Vitendo vinavyofanywa na watu hawa vya kupanga uchochezi na hujuma dhidi ya wapinzani ni uhaini dhidi ya taifa na watakuwa na wakati mgumu sana baada ya utawala huu wa kidhalimu kuondoka madarakani.
Upo ushahidi tosha kabisa wa kuwahusisha wahuni hawa katika gamba la " usalama wa Taifa" na uvunjifu wa amani uliopo na nawashauri CHADEMA kukusanya ushahidi huu wa waziwazi kwa matumizi wakati muafaka. Haiwezekani mtu mwenye cheo na madaraka akapanda jukwaani akatangaza kifo cha chama cha siasa akataja na muda (miezi 3) na akaachwa hivihivi bila hata ya kuulizwa jinsi hayo yatakavyotimia. Hivi ingetokea nini endapo kiongozi wa upinzani angepanda jukwaani na kutabiri kifo cha CCM au kiongozi yeyote?
 
Ni ukweli usiopingika kuwa ccm inapendelea dini moja. Hata sera zake toka 2005 zilikuwa ni kuanzisha mahakama ya kadhi kitu ambacho ni kinyume na katiba ya nchi. Leo hii wakristo wanaposema kuwa ccm inawapendelea waislam, viongozi wa ccm wanakataa. Naomba warejee sera yao ya 2005,iliyowaweka madarakani sio ya udini?
 
Hata enzi za Farao walipuuzia hivi hivi lakini mwishowe walipata stahiki yao

Tatizo lako wewe ndugu haueleweki kama kina Lukosi. Hamjui kushika moja. Majuzi tu ulikuwa unasapoti magamba na leo yanakukera
 
dhambi hii wanayoifanya itawatafuna kabla hata ya uchaguzi mkuu -- amini nakwambia mchakato wa kumpata mgombea urasi wa tiketi ya ccm 2015 hapo ndipo itakuwa hitimisho (RIP) ya chama hiki.

Mwalimu aliwahi kusema, "ukila nyama ya mtu basi utaendelea tu", sasa hii dhambi wanayoifanya kwa CDM, pia imo ndani ya chama, inakula taratibu, chama hakiko salama kabisa, itafikiana wakati wataanza kutoana kucha wao kwa wao. tutaona mengi before 2015.

Hata hizi habari za eti mwakyembe katoa tenda kinyemela kwa kampuni ya ccm unafikiri zinafikaje CDM? wao hao hao wanakimbilia upande wa pili na kutoa data zote.
 
CCM hivi sasa kinaendeshwa na vijitoto akina Ludovick na Mwigulu nyuma ya kompyuta zao bila hata ya kupata ridhaa ya wazee ndani ya chama hicho kikongwe hivyo mambo mengi kuonekana wa ovyo, kukosa busara na sawa na mchezo wa watoto wadogo kwenye vumbi.
 
tuseme labda ni kweli uliyoyandika. sasa ndo muanze kuteka na kujeruhi watu?

  1. Kila mtu anafahamu wazi kwamba mchezo mnaoufanya mlishaupanga kitambo na sasa mmeanza kuutekeleza kwa awamu Kutumia dola ISIYOJITAMBUA kubambikiza kesi kwa viongozi wa upinzani hasa CHADEMA.
  2. Mnajua wazi kwamba hampo tena kwenye mioyo ya Watanzania na hivyo mmeamua kutumia nguvu kujithibitishia kuitawala nchi hata kama mkishindwa kupitia sanduku la kura kama ilivyowatukia 2010.
  3. Mmeshiindwa kudhibiti mfumuko wa bei kiasi kwamba mlipoamua kupandisha nauli za vyombo vya usafiri mkatafuta kigezo kwa kupandisha bei ya mafuta usiku usiku ili iendane na ongezeko la nauli, na inajulikana wazi kwamba mnawategemea wafanyabiashara wawabebe kugharimia 2015 baada ya mipango yenu ya kuiba kuanza kugundulika mianya kuzibwa kila kona.
  4. Mnaelewa fika kwamba upinzani una nafasi kubwa ya kuchukua hatamu za uongozi kuanzia 2015 na sasa mmeamua kutumia kampeni za udini kwa vitendo kuwagawanya Watanzania ili nchi isitawalike na muweze kuendelea kuwepo madarakani kwa kigezo cha vurugu za kidini.
  5. Viongozi wenu wa juu wameridhia uteswaji, udhalilishwaji na hata kunyofolewa uhai kwa yeyote ambaye anaonekana ni kikwazo kwa chama na hususani anayewaamsha raia kujitambua.

Hii ni hatari kwenu maana kama hatutawaswaga ninyi kwenye mahakama za uhalifu basi wajukuu zenu watasimama kwa niaba.
 
Back
Top Bottom