CCM Mbeya: RPC anatukandamiza sana CCM!

CCM Mbeya: RPC anatukandamiza sana CCM!

ndo magamba walivyo, kaszi kulalamika tu. 'ku***ya anye kuku aki***ya bata kaharisha'!!lingekuwa ni kambi la CHADEMA ndo limesababsha hili sokomoko, magamba wangedai ni kambi la mafunzo ya ugaidi. RPC nakupongeza sana kwa kazi yako nzuri yenye kufuata Sheria na Taratibu za Jeshi la Polisi bila kubagua nani aliyekosea. Ni vema sasa magamba wakatambua kuwa Sheria ni msumeno ambao unakata pande zote mbili badala ya kumshushia lawama huyu RPC.:A S 576:
 
CCM imekwisha kabisa.
Na ole wake walete fujo siku ya Uchaguzi, jumapili ya 16/June.

Nape, Nchemba na makada wote wa CCM msijaribu kabisa kucheza na maisha ya watanzania, na mkijaribu tu mtakiona cha moto.
 
Huu ni ujinga uliovuka mipaka, hata kama ni Chama Tawala, sheria ipi inawapa ruksa ya kutoa mafunzo ya kijeshi kwa wanachama wake?. Serikali inajua hili ila inafumbia macho madhara yake ni makubwa sana huko mbeleni. Tukumbuke hata ITALAHAMWE kule Rwanda ililkuwa hivihivi, mimi nadhani kuna watu wanajiaandaaaa kufanya ubazazi wa kufa mtu huko tuendako, SErikali ichukue hatua sasa. Vinginevyo tunaelekea njia ya Rwanda ya 1994
 
-pole yao wanaccm kwa kukandamizwa.Ombi langu tu makambi yao yasifundishe vijana wao kuwa watekaji na wauaji kwa wale wasiokuwa upande wao

Watuhurumie this time watuchome ganzi kwanza kabla ya kungoa meno na kucha
 
"...Wameshindwa majukwaani..." asante RPC Diwani.

Ila huyo RPC nadhani ajiandae kwa uhamisho kwa vile CCM hawataki kabisa mtu mwenye kutumia weledi ktk utendaji au utumishi wa umma
 
Ukiona ccm wanailalamikia polisi ujue kwamba baada ya kushindwa kuhimili vishindo vya Chadema jukwaani wamekimbilia polisi kuomba msaada lakini wametoswa. Kama RPC Diwani Athuman ataendelea kufanya kazi yake kwa kufuata sheria ni dhahiri kuwa ccm watamtupia lawama kwa kushindwa kwao uchaguzi kata ya Iyela.
Lakini bahati nzuri kwa RPC Diwani Athumani atambue kuwa akisimamia sheria na haki kwa kila chama na kila mtu wananchi watamuunga mkono na hawatamuacha ccm wamvuruge.
 
Ni kweli kuna kambi ya Maninja wa CCM Ivumwe sekondari wakijiandaa na vurugu wakati wa uchaguzi wa Udiwani jumapili kata ya Iyela.

Wanavaa mizula inayofunika nyuso zao.
Kwa asiwe amini aende Ivumwe na Itende Sekondari atayaona haya ninayosema.

da! kumbe na Itende nako, hawa watu vp vp????
 
da! kumbe na Itende nako, hawa watu vp vp????
Ila sasa hivi wameshikwa pabaya.Hawana njia nyingine zaidi ya kufanya uhuni kama huo.Ni ngumu kuamini.
Sijui kama wameulizwa kuhusu lengo la makambi hayo na aina ya mafunzo wanayotoa.Na baada ya uchaguzi wa madiwani hao vijana watafanya kazi gani zaidi ya wizi.
 
RPC Diwani Athumani ni mmoja wa makamanda makini, asiyrkurupuka katika mambo mengi. Hii ndo raha ya usomi. Anafahamu ni kitu gani anafanya na kwa weledi wa kiwango gani. Ni vizuri makamanda wengine wafahamu wigo wa kazi zao badala ya kugeuka makada.
 
RPC Diwani Athumani ni mmoja wa makamanda makini, asiyrkurupuka katika mambo mengi. Hii ndo raha ya usomi. Anafahamu ni kitu gani anafanya na kwa weledi wa kiwango gani. Ni vizuri makamanda wengine wafahamu wigo wa kazi zao badala ya kugeuka makada.

nakuunga mkono mkuu! kama mapungufu basi sio kiasi kama walivyo wengine kama akina KAMUHANDA, huyu wa Mbeya anaweledi zaidi katika utendaji!
 
Nikiwa ndani ya daladala, kupitia Radio IbonyFm Habari nimemsikia katibu wa CCM mkoa wa Mbeya akilalamika kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya RPC DIWANI ATHUMAN amekuwa akifanya kazi kwa upendeleo hasa tangu CCM KUANZISHA KAMBI ya mafunzo kwa vijana wake maeneo ya Ivumwe jijini Mbeya!

Aidha, katibu huyo bila kusita, amemtaja RPC kuikandamiza CCM na kuipendelea CHADEMA hasa kwa kuwakamata vijana kadhaa wa CCM kufuatia kutekwa na kuteswa kwa kiongozi mmoja wa CHADEMA aliyekuwa anakatiza eneo ilipo kambi hiyo ya mafunzo ya CCM. namnukuu "haiwezekani mtu apite KAMBINI kwetu huku amevalia mzura wa CHADEMA na banghi mfukani halafu sisi tumuangalie tu, tena anaanza kuleta ubishi"!

Kwa upande wake RPC amesikika akisema yeye anafanya kazi kwa utafiti lakini anashangaa vyama vyote vikilalamika juu ya jeshi la polisi! pia akijibu kuhusu katibu wa CCM kumlaumu, RPC amejibu "huu ni uzushi...tena kama unaweza kuandika hii andika lakini nasema huu ni uzushi, kama wao wameshindwa majukwaani shauri zao lakini wasije kupotosha watu huku mitaani" alimalizia RPC!

chanzo: Ibony Fm Habari saa 13:00.

wana jamii! huu mtindo wa kuanzisha makambi ya mafunzo ya kujilinda mimi napata wasiwasi nayo!
Mmh
 
Msipoichagua ccm sileti maendeleo,hii ni kauli ya mwendazake akiwaambia wana tunduma.Kauli ya kukwaza kama hii hushangiliwa na vilaza.
 
Back
Top Bottom