GreenCity
JF-Expert Member
- May 28, 2012
- 5,620
- 4,265
Nikiwa ndani ya daladala, kupitia Radio IbonyFm Habari nimemsikia katibu wa CCM mkoa wa Mbeya akilalamika kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya RPC DIWANI ATHUMAN amekuwa akifanya kazi kwa upendeleo hasa tangu CCM KUANZISHA KAMBI ya mafunzo kwa vijana wake maeneo ya Ivumwe jijini Mbeya!
Aidha, katibu huyo bila kusita, amemtaja RPC kuikandamiza CCM na kuipendelea CHADEMA hasa kwa kuwakamata vijana kadhaa wa CCM kufuatia kutekwa na kuteswa kwa kiongozi mmoja wa CHADEMA aliyekuwa anakatiza eneo ilipo kambi hiyo ya mafunzo ya CCM. namnukuu "haiwezekani mtu apite KAMBINI kwetu huku amevalia mzura wa CHADEMA na banghi mfukani halafu sisi tumuangalie tu, tena anaanza kuleta ubishi"!
Kwa upande wake RPC amesikika akisema yeye anafanya kazi kwa utafiti lakini anashangaa vyama vyote vikilalamika juu ya jeshi la polisi! pia akijibu kuhusu katibu wa CCM kumlaumu, RPC amejibu "huu ni uzushi...tena kama unaweza kuandika hii andika lakini nasema huu ni uzushi, kama wao wameshindwa majukwaani shauri zao lakini wasije kupotosha watu huku mitaani" alimalizia RPC!
chanzo: Ibony Fm Habari saa 13:00.
wana jamii! huu mtindo wa kuanzisha makambi ya mafunzo ya kujilinda mimi napata wasiwasi nayo!
Aidha, katibu huyo bila kusita, amemtaja RPC kuikandamiza CCM na kuipendelea CHADEMA hasa kwa kuwakamata vijana kadhaa wa CCM kufuatia kutekwa na kuteswa kwa kiongozi mmoja wa CHADEMA aliyekuwa anakatiza eneo ilipo kambi hiyo ya mafunzo ya CCM. namnukuu "haiwezekani mtu apite KAMBINI kwetu huku amevalia mzura wa CHADEMA na banghi mfukani halafu sisi tumuangalie tu, tena anaanza kuleta ubishi"!
Kwa upande wake RPC amesikika akisema yeye anafanya kazi kwa utafiti lakini anashangaa vyama vyote vikilalamika juu ya jeshi la polisi! pia akijibu kuhusu katibu wa CCM kumlaumu, RPC amejibu "huu ni uzushi...tena kama unaweza kuandika hii andika lakini nasema huu ni uzushi, kama wao wameshindwa majukwaani shauri zao lakini wasije kupotosha watu huku mitaani" alimalizia RPC!
chanzo: Ibony Fm Habari saa 13:00.
wana jamii! huu mtindo wa kuanzisha makambi ya mafunzo ya kujilinda mimi napata wasiwasi nayo!