Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Nijuavyo mimi chama cha siasa chochote kile, kinaundwa na sera zake na wala siyo viongozi. Kwa mantiki hiyo sera za CCM kamazilivyokuwa zimebuniwa na waasisi wa chama hicho zilikuwa zimejikita katika kupambana na dhuluma za aina yote katika jamii. Katika miaka ya karibuni chama hicho kiligeuka na badala ya kuwa katika mstari wa mbele kupambana na dhuluma katika jamii kikawa chenyewe ndicho chanzo cha dhuluma hizo. Hali hiyo ndiyo imesababisha kipoteze mvuto wake kwa wananchi. Hivyo ikiwa maudhui ya kujivua ghamba yanayozungumzwa yanalenga katika kurejesha mvuto kichokuwa nao chama hicho huko nyuma, basi zoezi hilo halipashwi kuishia kwenye kubadilisha sura za viongozi, bali pia linapashwa liusishe na sera ya chama.