CCM kujibu mapigo dhidi ya CHADEMA?

CCM kujibu mapigo dhidi ya CHADEMA?

Baada ya Chadema kufanya mikutano ya hadhara mbalimbali katika mikoa, wilaya, kata na vijiji nchini, hali ambayo imekivuruga chama cha mapinduzi, kuna tetesi kuwa CCM nayo imeanza kujipanga kuijibu CDM kwa kupitia maeneo yote ambako viongozi wa kitaifa wamepita. Habari zinaongeza kuwa viongozii wa ngazi ya Taifa, watapita maeneo yote waliyopita viongozi wa taifa wa CDM wakati viongozi wa mikoa yote nchini, wataendesha ziara katika kila wilaya kurudisha wanachama wa CCM waliovua gamba na kuchota wanachama kutoka CDM na vyama vingine vya upinzani. Katika harakati hizo, viongozi wa wilaya nao watatakiwa kufanya ziara (baada ya viongozi wa mkoa kupita) kila kata na kijiji ili kuhakikisha CCM haiendelei kupoteza wanachama.

Nadhani kwa mkakati huu, CCM inaweza kujaribu kurudisha imani yake kwa wananchi. Inagawaje, ni kama WAMECHELEWA

Tusubili tuone ngoma itakavyochezwa



CCM ni chama Tawala kinachomiliki Dola. Hivyo hakipaswi kufanya mikutano ya hadhara ili kuwaeleza wananchi nini inakifanya.

Wanatakiwa wafanye vitu katika kutimiza Ilani na Ahadi za Chama ili wananchi waone hii inatosha.

lakini wakienda Jukwaani na kuongea, wananchi watawadharau kwa sababu watu hawataki propaganda bali vitendo.

Na uwezo wa kufanya vitendo vitakavyoonekana, CCm wanao isipokuwa wanakumbatia Ubinafsi na kukosa Fikra za kufikiria wafanye nini ili kurudisha Imani ya Chama kwa Wananchi wa Tanzania.

Ni wakati sasa kwa Viongozi wa CCM kuamka toka usingizini vinginevyo................


View attachment 54939

............ Yangu macho!!!!!!!!!!!!!


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
kuna tetesi kuwa CCM nayo imeanza kujipanga kuijibu CDM kwa kupitia maeneo yote ambako viongozi wa kitaifa wamepita. Habari zinaongeza kuwa viongozii wa ngazi ya Taifa, watapita maeneo yote waliyopita viongozi wa taifa wa CDM wakati viongozi wa mikoa yote nchini, wataendesha ziara katika kila wilaya kurudisha wanachama wa CCM waliovua gamba na kuchota wanachama kutoka CDM na vyama vingine vya upinzani.

Hapo ikiwa kweli PATAMU kwani tutajua kwa uhakika nani Mbabe kwa sasa katika siasa za Tanzania hususani Tanganyika.
 
Ni kwa kasi isiyotarajiwa ya kwamba CDM inafahamika kwa kiasi kikubwa mingoni mwa watanzania huku CCM kikionekana kuwa chama cha vikundi....Katika hili tunaomba nacho/CCM kifanye mikutano Arusha, Dar na maeneo mengine yote ambayo CDM imepita ili nasi kuwaonyesha watanzania ya kuwa tupo hai na tunakubalika bado.


naomba awepo Raisi,Katibu mkuu, Nappe na baadhi ya wabunge kama ambavyo CDM wanafanya.Hapa tutajipima vyema. Mkutano huu usiwe wa kiserikali ila wakichama katika kuhamasisha maendeleo na uelewa wa demakrasia haki na wajibu.


AKSANTEEEEEEEEEEEEEEE


Otherwise PEOPLES'S POWER ITATAWALA
Umesema raisi ahudhurie halafu isiwe mkutano wa serikali!!??
Kweli magamba wameishiwa hoja, hawana la kufanya.
Unawashauri wapambanishe mikutano, kwani CDM wanavyofanya mikutano wanapambanisha na nani?
Hata hivyo mikutano ya ccm ni vigumu mno au haiwezekani kutoa tathmini ya support ya wananchi kwani mikutano yao inavutwa na nguvu ya ziada kama kusafirisha wananchi kutoka sehemu mbalimbali kwenda kwenye mkutano, kugawa posho ya kwenda mkutanoni, kugawa kanga, t-shirt, kofia. Kwahiyo mkutano wa ccm hata ufurike watu namna gani, sio rahisi kujua wenye mapenzi na chama, tofauti na CDM ambapo wananchi wanajitolea wenyewe kwa moyo wa dhati ikiwa ni pamoja na kukichangia chama.
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....



Ni kwa kasi isiyotarajiwa ya kwamba CDM inafahamika kwa kiasi kikubwa mingoni mwa watanzania huku CCM kikionekana kuwa chama cha vikundi....Katika hili tunaomba nacho/CCM kifanye mikutano Arusha, Dar na maeneo mengine yote ambayo CDM imepita ili nasi kuwaonyesha watanzania ya kuwa tupo hai na tunakubalika bado.


naomba awepo Raisi,Katibu mkuu, Nappe na baadhi ya wabunge kama ambavyo CDM wanafanya.Hapa tutajipima vyema. Mkutano huu usiwe wa kiserikali ila wakichama katika kuhamasisha maendeleo na uelewa wa demakrasia haki na wajibu.


AKSANTEEEEEEEEEEEEEEE


Otherwise PEOPLES'S POWER ITATAWALA
 
Hatuhitaji kumtumia Rais
kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya
vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM
huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa
Chadema.....

Mwenyekiti wenu yupi? Huyuhuya anayeangukaanguka mbele za watu? Huna upeo tu kisingekuwa chama cha siasa kingeisha futwa kitambo!
Tabia zenu za kuropoka bila kufiri ndizo zinakizika chama chenu cha magamba.
 
Ni kwa kasi isiyotarajiwa ya kwamba CDM inafahamika kwa kiasi kikubwa mingoni mwa watanzania huku CCM kikionekana kuwa chama cha vikundi....Katika hili tunaomba nacho/CCM kifanye mikutano Arusha, Dar na maeneo mengine yote ambayo CDM imepita ili nasi kuwaonyesha watanzania ya kuwa tupo hai na tunakubalika bado.


naomba awepo Raisi,Katibu mkuu, Nappe na baadhi ya wabunge kama ambavyo CDM wanafanya.Hapa tutajipima vyema. Mkutano huu usiwe wa kiserikali ila wakichama katika kuhamasisha maendeleo na uelewa wa demakrasia haki na wajibu.


AKSANTEEEEEEEEEEEEEEE


Otherwise PEOPLES'S POWER ITATAWALA

katika watu amabao hawafikirii duniani wewe nimmoja wapo .
kunajambo moja tu linaweza irudisha ccm kwa watu nalo ni uadilifu . hiyo mikutano unayosema labda kama kimekua chama chaupinzani .
1. kwanza kikifanya mkutano watatoa seragani ?
2. kumbuka ahadi kibao jk alizitoa wakati wa uchaguzi katekeleza ngapi mpaka sasa ?
3. akirudi atawaambia nini ?
4. wameshidwa ku control mfumuko wabei . nimikutano wataiweza? tenawatapigwa mawe
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....
Wewe Nnauye Jr ni kiongozi wa ngazi ya juu lazima uwe na adabu kidogo unapo respond posts za watu, majibu ya aina hii waachie wasaidizi wako kina ritz, Rejao, Kamati ya Katiba na wengine. Jibu kama hili linakuonyesha ni kwa kiasi gani unawahofia hao unaowaita waganga njaa.

Ungeonekana mtu wa busara kama ungekuja na hiyo mikakati badala ya kuanza kumdharau counterparty wako, hicho kikundi unachokiita ni cha wanaharakati ndicho kinakufanya uhangaike usiku na mchana.
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....

Wala hamuhitaji kuwaleta wazee wa mkoa wa Dar es Salaam ambao mmezoea kuwatoa Kiburugwa na maeneo mengine kwenye mkutano huo.
Wala hamuhitaji kuwadangaya wakereketwa kuwa mtawatafutia magari kuja na kuondoka, huku mkijua kuwa wakishaletwa kuondoka watajiju.
Wala hamuhitaji makundi ya waganga njaa wakati wewe unalo kundi llako ambalo unalitumia kupata chochote ili kuganga njaa yako, ndio maana ulishindwa hata kuhudhuria mazishi ya rafiki yake baba yako ambaye ni kama baba yako.
Wala hamuhitaji mahudhurio makubwa kama ya waganga njaa kwa kuwa kila Mtanzania ameridhika na maisha ya kila siku.
Kumbe wewe huna tofauti na mtu wa huko Dar aitwaye Didas anayesema watu wanafikiri kutumia.............
 
Baada ya Chadema kufanya mikutano ya hadhara mbalimbali katika mikoa, wilaya, kata na vijiji nchini, hali ambayo imekivuruga chama cha mapinduzi, kuna tetesi kuwa CCM nayo imeanza kujipanga kuijibu CDM kwa kupitia maeneo yote ambako viongozi wa kitaifa wamepita. Habari zinaongeza kuwa viongozii wa ngazi ya Taifa, watapita maeneo yote waliyopita viongozi wa taifa wa CDM wakati viongozi wa mikoa yote nchini, wataendesha ziara katika kila wilaya kurudisha wanachama wa CCM waliovua gamba na kuchota wanachama kutoka CDM na vyama vingine vya upinzani. Katika harakati hizo, viongozi wa wilaya nao watatakiwa kufanya ziara (baada ya viongozi wa mkoa kupita) kila kata na kijiji ili kuhakikisha CCM haiendelei kupoteza wanachama.

Nadhani kwa mkakati huu, CCM inaweza kujaribu kurudisha imani yake kwa wananchi. Inagawaje, ni kama WAMECHELEWA

Tusubili tuone ngoma itakavyochezwa


labda naomba msaada, unaposema viongozi wa kitaifa na mkoa na wilaya unamaanisha nini? kama unamanisha Wenyeviti na makatibu wa taifa mpaka wilaya wa ccm upo sahihi lakini kama unamaanisha, rais, mawaziri marc na madc hapo ndipo mnapokosea na kutumia vibaya kodi zetu.
 
Programme hizo zitakifilisi chama kutokana na gharama kubwa ambazo chama kitaingiia ili kushawishi watu na gharama za rais kuwepo mahali ni kubwa siyo kama Dr. Slaa.

Chama cha Mapinduzo ndiyo kipo madarakani hakiitaji kujikita kwenye siasa za majukwaa zaidi ya utekelezaji wa ilai yake ambayo ndiyo kampeni kubwa kuliko kushinda kwenye majukwaa.


Kinadharia uko sawa lakini ukiangalia kwa makini utaona katika mikutano ile CCM inapoteza wanachama kwa maelfu! mikutano ya majukwaani pengine ingewarudisha waliotoroka! Utekelezaji wa ahadi za CCM unasuasua mahali pengi kiasi cha kukatisha tamaa. Kila mdharau mwiba miguu huota matende!
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....


Ndugu Nape,

Kwa mara nyingine tena naona jinsi busara yako ilivyo ndogo, niliwahi kukushauri na leo narudia, wewe ni kiongozi wa ccm taifa unatakiwa kutafakari kabla ya kuandika hapa, sikutegemea wewe uandike pumba hii hata kama maneno haya yamekuchoma onyesha walau umekomaa kuweza kupewa hicho cheo lakini kama wewe unaejibu hivi ndio umekoamaa na kupewa nafasi hiyo ccm basi ccm kimekwisha.

RUDIA KUSOMA ULICHO ANDIKA HUKU UKITAFAKARI KWA KINA.
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....

Nakufagilia sana bwana mdogo kwa kujiamini kwako, lakini KAMA UNA MASIKIO YA KUSIKIA BASI SIKILIZA! Uwe mwepesi wa kusoma alama za nyakati! Upepo bwana mdogo umegeuka! Mikakati ya akili inahitajika sana kuliko kudhani wale watu mliozoea kuwaburuza jana ndo wale wa leo! Dharau zako zitakufanya utembee kwa aibu Nchi nzima kwani ulijijengea heshima kubwa sana kabla hujavishwa hilo "lemba "! Waganga njaa wanakubalika kwa waganga njaa wenzao, na ushahidi unaonekana viwanjani na katika chaguzi ndogo! Mafisidi mtajibeba!
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....

Nimekudharau sana kwa majibu yako ya kijinga na kitoto.Labda kama wewe si Nape.Hivi chama chako hakihangaiki usiku na mchana kuwazuia hao unaoita waganga njaa ili wasiwaeleze watu ukweli wa maisha magumu?Hakika sasa naamini kuwa ccm haina watu.Hivi unaweza kumlinganisha huyo kikwete wako na Dr Slaa?Kikwete hata kuongea kwa lugha ya kigeni ni tatizo,mlimpataje?Hajui matatizo ya watanzania.Umaskini wa nchi yake unatokana na nini hajui.Wewe bado unatamba una Rais.Nimemdharau sana Kikwete kwa udhaifu wake.Sijui elimu yake darasani alikuwa anapata ngapi katika masomo yake.Hivi nikuulize kati ya Tundu Lissu unayedhani mwanaharakati na Kikwete mwenye ubongo unaofanya kazi ni nani?Cheo kimekupofusha.Nyie mpo madarakani kama mnaona chadema ni kikundi na si chama cha siasa kwanini hamkifuti?Majibu ni kama yale ya Ghadaf kuwa waasi ni panya na mende.
Ipo siku kauli hiyo utaikumbuka watakapokutoa madarakani.Mlevi wa madaraka wewe.Wewe ndio msemaji wa ccm?Halafu umejigamba humu leo kuwa umesoma na hata ukitolewa ccm una uwezo wa kufanya kazi nyingine.Huu ndio usomi wako wa India?Una makengeza.Unajifanya kujitune kuongea kama mwenyekiti wako.Huna lolote.
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....
Nape ndugu yangu, majibu yako yawe yanafanana na wadhifa wako wa kitaifa. Majibu ya kihuni waachie wahuni na sio wewe! Ukijibu, sisi tunatumia majibu yako kama rejea kama hujui hilo basi kuna walakini mkubwa juu ya uwezo wako wa kiuongozi!
 
Imani ya wananchi kwa ccm ni kutimiza ahadi tu za kwenye ilani yao,na si kufanya mikutano ya kisiasa kama chadema vinginevyo labda waende kuwasalimia tu wananchi, lakini wajihadhali kupigwa mawe na zomeazomea kwa sababu sasa hivi wananchi wanahasira kupita wakati wowote
 
CHADEMA waliona muda wa kampeni hautoshi wakaamua kuanza mapema. Akili zao zinawatuma kuwa Watanzania walio wengi watawapa madaraka 2015. Maawee!
 
Hatuhitaji kumtumia Rais kujibu yanayosemwa na makundi ya wanaharakati waganga njaa kwa kujifanya vyama vya siasa, tutajibu wenyewe! Mwenyekiti wa CCM huwezikumlinganisha na Mwenyekiti wa kikundicha wanaharakati wa Chadema.....

Hivi kwa nini huwa unashindwa kujibu hoja wewe VUVUZELA,sema tunaogopa kufata nyayo za simba,mtaumizwa na kuumbuka
 
Pole yao! Kwa Arusha siwashauri, labda watumie yale mazingaombwe yao ya kutoa hela kwa wasikilizaji wake na kubeba wengine kwa malori kujaza uwanja.
 
Back
Top Bottom