CCM kuibuka kidedea uchaguzi Arusha

Du! Kama moral authority yako inakuruhusu ni sawa kiongozi
Haya sio mambo ya moral authority, haya ni mambo ya survival, kwenye struggle for existence, survival is only for the fittest, kama ili uishi mtu ni lazima ujikombe, then hakuna jinsi, lazima utajikomba tuu, kwa sababu huwezi kula moral authority, huwezi kula integrity, kula ni chakula tuu, ili uishi!.

P.
 
Shonza nimekuelewa kusudio la andishi lako
Mmeisha panga wizi sasa unatengeneza fence
 
Wakati uliopita ilikuwa kununua madiwani. Sasa hivi - kununua shahada!
Strange!
 
Pascal,
Ushauri wangu ni kuwa ngazi ya juu ya kutengeneza mambo ipite
kujikomba ni mtu kufuata nyayo za ''Quisling,'' hii ina uhakika zaidi
kuliko hii ya kujipendekeza ingawa lazima niweke tahadhari kuwa
mwisho wake ni hatari kama historia ilivyodhihirisha.

Mtoto wa Kiyahudi katika kambi ya Manazi Auschwitz anamuuliza
mama yake akielekeza kidole chake kwa Yahudi kibaraka, ''Mama
yule si Myahudi kama sisi? Mbona yeye ana mkabala mzuri na
Wajerumani na ana nguo nzuri tofauti na sisi na anakula chakula
kizuri?''

Mama akamjibu mwananae, ''Kweli yule ni Myahudi kama sisi lakini
kwa sasa kapewa kazi na Wajerumani ya kuwasaidia kutushughulikia
sisi ndugu zake sasa hizo nguo nzuri na chakula safi ndiyo malipo
yake...''

1945 Red Army linakuja kwa vishindo kuingia Poland na Wajerumani
wanarudishwa nyuma ni dhahiri wameshindwa vita.

Hawa Manazi wameua Wayahudi wengi katika matanuri ya gesi ya
sumu Auschwitz Poland na kwengineko na weshajua nini kitawafika
kwa kushindwa vita ile.

Hakika ya vitanzi ni wazi.

Lakini Manazi walikuwa na wasaidizi ndani ya Wayahudi wenyewe
na watu kama Quisling...

Pascal nini ilikuwa hukumu ya watu kama hawa walipofikishwa
Nuremberg?

Historia imebeba mafunzo mengi sana ya kuzingatia.
 
Hakika historia ni mwalimu mzuri
 
Mkuu Maalim Mohammed Said, kiukweli kwa somo hili, dhamira yangu imenishuka, japo mimi sii miongoni wa wakujipendekeza na kujikombakomba tzpe ila ni realist, ninayetambua na kukubali nyakati zimebadilika, na kwa sisi Wakristu, kuliko kujipendekeza, ni bora hata ufe kwa kusulubiwa msalabani, kwa kuufia ukweli, kama Bwana wetu Yesu Kristu, kuliko kujipendekeza kwa wadhambi, hivyo nimesema na hapa narudia, kama the only way for survival ni kujipendekeza, if you want to survive, lazima ujipendekeze, au u perish na kuitwa shujaa.

Zama hizi zimebadilika, hivyo watu wote adaptive for changes, watabadilika na zama hizi kama samaki anavyobadilika na ubaridi wa maji, ndio maana niliwahi kubandika bandiko hili, kuwaasa watu humu kuhusu hii situation
If you can't beat them, join them! He is the ... - JamiiForums

Paskali



 
Paskali,
Yote hayo usemayo yanategemea imani ya mtu.

Ikiwa unadhani binadamu ana uwezo wa kumnufaisha binadamu mwenzake,
basi hiyo itakuwa sawa.
 
Napenda tuu unavyo inua mikono yako!!
 
Paskali,
Sitaki kuamini kuwa una maana kama hakufanya hivyo watamuua.
Hii ndiyo maana yako?
No siamini katika kuuana, nazungumzia katika muktadha wa the struggling for existence, surviving is only for the fittest, sasa to fit you have to be adaptive kwenye mabadiliko yoyote, vinginevyo huwezi ku fit, usipo fit you just perish.
Paskali
 
Ukosefu wa moral authority / integrity / social ethics kumemfanya mwanadamu kusahau kanuni ya "ili ule lazima ufanye kazi" (shughuli yoyote halali ya kumwingizia kipato / kupata mkate wake wa kila siku). Suala la survival of the fittest (law of the jungle) lina maana ya kupambana na hali ngumu katika mazingira magumu ambayo bila hivyo, utaangamia!
Kwa muktadha huo hapo juu, naamini kwamba, kama mwanadamu atafanya kazi halali kwa uadilifu (bila makandokando), hana sababu ya kujikomba! Vinginevyo, awe anataka njia ya mkato ambayo kwa kujikomba atapata anachotaka. Aidha watu wa kujikomba ni hatari kwa sababu mara zote hawaaminiki na uhusiano wao mara zote ni pale unapokuwa na kile anachohitaji. Kikiisha, na mahusiano yake yanakuwa yameisha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…