yohana charles
Senior Member
- Mar 21, 2013
- 134
- 10
Kutokana na agizo la TFF kwa baadhi ya viwanja kwamba lazima vifanyiwe ukarabati,kiwanja kimojawapo kikiwa ni SAMORA MEMORIAL STADIUM cha mjini Iringa kiwanja ambacho ni miongoni mwa viwanja nchini ambavyo CCM inadai ni mali yake.,ccm Iringa ikatangaza kuwa itafanyia ukarabati uwanja ule...kwa akili yangu nilidhan ile pitch nzima ingelimwa kwa greda then ingepigwa haro ili kupata level ndo nyasi mpya zingepandwa..nilishangaa kwa chama tawala,chenye miradi tele ya kuingiza pesa ETI pitch ya uwanja inakatuliwa kwa jembe la mkono, nilicheka saaana,kwa kuwa mbavu zilikuwa zinaniuma kwa kucheka ikabidi niondoke...USHAURI WA BURE KWENU CCM IRINGA,NENDENI MKAJIFUNZE KWA WENZENU CCM MBEYA NAMNA WANAVYOKARABATI UWANJA WA SOKOINE.!